Vijana wengi,
 wanapoona wamepata urefu, 
mabadiliko ya mwili, kupanda kielimu,
 na hata kazi 
wanajiona tayari wameshakua.

Katika mazingira ya elimu kama chuo
au kazini,
vijana wengi wamekuwa kitaaluma na kiujuzi, lakini 
kihisia bado wanakuwa ni wadogo lakini wanashindwa kulitambua hilo.
Jibu linaweza kuja kwa haraka kwamba,
hiki ni kizazi cha vijana wanaojua vitu vingi mapema kabla ya umri wao.

Kiuhalisia kijana anatakiwa apate muda wa kukomaa kihisia ili kukabiliana na 
changamoto za ukubwani.

Vijana wengi siku hizi,
 wanatumia taarifa ambazo hawawezi kuzikabili katika umri wao.

Ubongo unakuwa bado hauja komaa kwa shughuli hiyo yeye anakuwa tayari ameshaianza.
Akili yake,
 inazichukua taarifa hizo na kuzihifadhi lakini hisia zake haziko tayari kuzitumia katika namna inayopaswa.

Jamii huwa inafurahi sana kumuona kijana anajitambua na 
anaonyesha ishara za kukua kihisia,
kwa jinsi anavyokabiliana na changamoto kubwa,
katika namna inayostahili.

ZIFUATAZO NI ISHARA ZA KUKUA KIHISIA:

1.KUWA MVUMILIVU

Hii ni ishara inayomtofautisha mtu ambaye amekua na 
yule ambaye hajakua kihisia.
Sifa moja ya watu ambao hawajakua kihisia ni kutosubiria muda muafaka wa kufanya mambo yake,
yawezekana watu wengine wakaumia lakini kwa kuwa yeye amefurahi, 
ni sawa tu.
Aliyekuwa kihisia hata kama
 hilo jambo ni la kumfurahisha,
 atasubiri tu muda muafaka ufike.


2.HAYUMBISHWI NA KUKOSOLEWA

 Aliyekuwa kihisia anaelewa kabisa kwamba,
kukosolewa ni 
sehemu ya kujifunza.
Watu waliokua kihisia,
 huwa wanapokea kukosolewa bila 
kuruhusu ukosoaji huo uharibu mambo yake mengine.
Wanajielewa wanataka nini na wao ni nani.

3.WANAKUWA NA ROHO YA UNYENYEKEVU

Unyenyekevu huwa unaenda sambamba na ukuaji wa hisia.
Unyenyekevu si kuwafikiria wenzako tu 
kwanza na wewe ukajitelekeza,
hapana.
Wanakuwa si watu wa kujipendelea wao 
tu kwa kila kitu.
Ila ni watu wa kwanza 
kutambua kuwa uwezo waliopewa na Mungu
ni kwa ajili ya viumbe na watu wanaoishi nao.

4.WANASIMAMIA MAAMUZI YAO

Wana misimamo inayotawala maamuzi yao,
wako tayari kufuata
 misimamo yao na kupita njia ya maisha waliyochagua kwa 
ujasiri bila kubabaika na wanakuwa tayari kuwajibika kutokana na 
maamuzi yao.
Tabia zao ndio zinaongoza maamuzi yao ya kila siku.

5.WEPESI WA SHUKRANI

Iko wazi kabisa,
 kuwa unavyozidi kukua ndio kuonyesha shukrani kwa watu na Mungu
 si kitu cha kuficha katika mambo madogo
 hadi makubwa
unayofanyiwa.
Mtu ambaye hajakua anaona yote yanayomtokea anayastahili kwahiyo 
kushukuru hawezi.

6.ANATUMIA HEKIMA KABLA HAJAFANYA JAMBO

Mtu ambaye amekuwa anafundishika, 
hajioni kuwa ana majibu 
ya kila kitu.
Jinsi anavyozidi kujua vitu ndivyo anavyozidi kutafuta hekima.
Huwa hawaoni aibu kufuata ushauri kwa mwalimu, au mzazi 
pale anapoona amekwama.

JARIBU KUJICHUNGUZA,
 KAMA UMEKOSA SIFA HATA MOJA KATI YA HIZO HAPO JUU.

 BASI UJUE BADO HUJAKUA KIHISIA
USI HARAKIE VITU AMBAVYO UNAONA KABISA MUDA WAKE BADO.





Share this post:

Digg it StumbleUpon del.icio.us Google Yahoo! reddit

0 comments:

Post a Comment

 
Copyright 2013-2017 Lisha Ubongo
| Branded by www.pixelbase.co.tz