26.JIAMINI KUWA UNAWEZA:

Ukitaka kuwa mjasiliamali 
ni lazima ujiamini wewe 
mwenyewe kuwa unaweza kufanikisha unachotaka kufanya.
Wewe ukijiamini na hata
 ukaweza kusimama mbele
 za watu kuwaeleza kuwa unaweza hata wao watakuamini.

27.SOMA SANA:

Mjasiliamali mzuri ni yule
 anayewekeza muda wake 
katika kutanua uwezo 
wake wa kuelewa mambo.
Kwa njia ya kusoma kila kinachohusu mambo anayoshughulika nayo, 
ndipo anapoongeza ujuzi wa biashara yake na ubunifu.
Hakuna njia itakayokupa
 maarifa makubwa kama
 kujisomea mwenyewe maandiko mbali mbali na si lazima uwe darasani.

28.KUWA JASIRI:

Mjasiliamali wa ukweli huwa ni
 jasiri na yuko tayari kulinda analoliamini ni sahihi kwa 
gharama yoyote.
Yawezekana kuna watu wakataka kubadilisha wazo lako kwa kuwa tu 
wao wanaona halifai,
unapaswa  utoe msimamo wako wa dhahiri mbele yao.

29.IFAHAMU VIZURI BIASHARA YAKO:

Unaweza ukajitolea kufanya kazi bure kwa mtu anayefanya shughuli 
unayopenda kuja kufanya ili kuijua nje na ndani ikoje na 
changamoto zake.
Ukishapata uzoefu kwa kipindi fulani ndio unaweza kutoka na kwenda
 kuanza harakati zako,
na sio kuvamia biashara usiyojua changamoto zake.

30.JITOKEZE:

Kama unataka kuwa mjasiliamali
 ni vyema ukaondoa aibu 
ya kushindwa kusimama mbele za watu wakuone na wakufahamu.

31.CHOCHEA WAZO LAKO:

Jipe mwenyewe mizuka ya 
ndani kuwa hili wazo ni zuri na utafanikiwa kupitia hilo pasipo 
kusubiri maoni ya nje.
Unaweza ukatenga muda 
wako wa kukaa kila siku na kulipalilia wazo lako ndani kwa ndani 
huku ukifikiria zaidi kuwa litafanikiwa.

32.ANZA LEO:

Ni uchizi kukaa chini na 
kusema siku zijazo nitaanza ujasiliamali,
unapaswa utambue kama
 kweli uko ndani yako 
hauhitaji kusubiri kesho ndio uanze, anza leo harakati zako.

33.FANYA UTAFITI WA KINA:

Chunguza soko lako kwa 
makini huku ukiangalia vitu kama mshindani wako ni nani,
na utawezaje kujitofautisha 
naye katika bidhaa au huduma anayotoa.

34.TAMBUA UNACHOWEZA NA USICHOWEZA:

Ukitaka kuwa mjasiliamali 
mzuri ni lazima ujue maeneo gani wewe sio mzuri na maeneo 
gani wewe ni mzuri.
Tumia muda mwingi kufikiria
 zaidi kuboresha maeneo
 ambayo wewe ni mzuri, 
achana na kule ambako uwezo wako ni mdogo patakupotezea muda.

35.KUWA NA NJAA:

Unatakiwa uwe na njaa ya 
kweli kabisa ya kutaka 
kula unachofikiria unastahili kula.
Kama hutokua na njaa y
a kweli ukikutana na 
changamoto utajikuta unarudi nyuma kwa kukosa uvumilivu.

36.TAFUTA WASHIRIKA:

Ukiwa mjasiliamali ni 
lazima utafute watu wa kushirikiana nao ambao unaamini wana
 mtazamo na ari kama yako kibiashara.

37.TENGENEZA WAZO RAHISI KUELEWEKA:

Ikiwa jina la biashara yako ni 
gumu na linampa wakati mgumu 
mteja kuioanisha na bidhaa au huduma unayotoa utapata tabu katika soko.
Hakikisha mteja anapoona 
jina la biashara yako awe 
anapata picha halisi ya nini kinachoendelea katika kampuni yako.

38.ZIJUE FAIDA NA HASARA ZA SOKO:

Unpotaka kufanya ujasiliamali 
ni lazima uangalie kwa
 makini faida na hasara za soko unalotaka kulihudumia.

39.KUWA RAFIKI KWA WATU:

Mjasiliamali wa kweli ni 
lazima anakuwa karibu na watu ambao anawahudumia,
wateja wanapoona mtoa 
huduma yuko karibu nao wanajenga moyo wa kumuamini na kumpenda.

40.TUNZA PESA:

Kama unataka kuwa mjasiliamali 
anza leo kujua namna ya
 kutunza kile kidogo unachopata,
kama unafanya kazi mahali
 jiwekee utaratibu wa 
kuweka kando sehemu ya mshahara wako ili uje uwekeze.

41.FANYA KAZI NA MTU MWENYE UJUZI TOFAUTI:

Kama wewe una ujuzi wa 
aina fulani usitafute mtu 
mwenye ujuzi huo huo mfanye kazi moja, tafuta mtu ambaye unaona
 mmetofautiana ujuzi lakini wote mnataka kuhudumia soko moja.

42.THAMINI WAZO LAKO:

Kuna watu wakati unaelezea wazo lako wanaweza wakakueleza kuwa 
hauna jipya na kwamba wazo kama hilo lako tayari lipo.
Lakini wewe pambana kwasasbabu hata kama mwengine anafanya 
hatoweza kufanya kama
 wewe utakavyofanya,
unachotakiwa wewe ni kujitofautisha tu.

43.UVUMILIVU:

Kuwa mjasiliamali unataka uwe na uvumilivu wa hali ya juu, kwani si 
kila siku utakuwa 
katika hali hiyo hiyo.
Kuna kipindi utakataliwa na wateja wako na uspokuwa mvumilivu
 unaweza ukaacha unachofanya.

44.UNDA TIMU YA UHAKIKA:

Ukiwa na timu ya uhakika ya 
watu wachapakazi na 
wenye mtazamo kama wako,
ukirogwa kumuingiza kundini mtu mwenye mtazamo tofauti na wewe 
mtasumbuana na anaweza kupoteza ari ya kundi kufanya kazi.

45.USIRIDHIKE:

Ukitaka kuwa mjasiliamali,
 ni lazima uwe na moyo wa kuona hauridhishwi na hali iliyopo,
na kwamba unataka kufanya kitu ili ufanye mabadiliko.

ANZA SASA KUFANYIA KAZI WAZO LAKO LA UJASILIAMALI NA UTAONA MAFANIKIO YAKE.



Share this post:

Digg it StumbleUpon del.icio.us Google Yahoo! reddit

0 comments:

Post a Comment

 
Copyright 2013-2017 Lisha Ubongo
| Branded by www.pixelbase.co.tz