Ukamilifu ni uzuri, wazimu ni fikra na ni heri kuwa na kejeli kuliko kuchosha watu.
WEWE, rafiki yangu ni mtu kamili na mwenye uwezo binafsi wenye kushangaza watu wengine.
Je, umeshasahau wewe ni nani?
Ikiwa umejisahau kutokana na mihangaiko ya dunia hii, basi ngoja nikukumbushe mambo ya ukweli ambayo unapaswa uanze kuiambia nafsi yako.

1."Sina muda wa kutulia"

Katika hali ya kawaida unaweza ukawa ulikutana na mambo yaliyokufanya uache kuwa mchakalikaji, mbishi na usiyekubali kushindwa katika kupigania mafanikio.
Nakuambia anza sasa kuamsha upya hisia za kupambana na vikwazo vyote vinavyokuzuia wewe kutimiza malengo yako na ukizingatia muda haukusubiri wewe.

2."Nina kila sababu ya kuiamini nafsi yangu"

Umeishi muda mrefu kwa kusikiliza sauti za watu wakikuambia wewe unapaswa uweje kulingana na mitazamo yao.
Unapaswa ujue kuwa unapotaka kufanya jambo lolote mtu wa kwanza kumsikiliza ni nafsi yako ambayo siku zote haina muda wa kukudanganya.
Si kwamba usisikilize ushauri kutoka kwa watu wengine, rahasha, ila unapaswa utangulize nafsi yako kwanza.

3."Upekee wangu ndio nguvu yangu kuu"

Ndio hujakosea, upekee wako ndio utakao kutofautisha wewe na mtu mwengine.
Yawezekana mazingira yalikuwa yanakufanya utake kuwa na tabia kama za fulani na hivyo ukajikuta unapoteza uhalisia wako.
Anza sasa kuishi wewe na sio mtu mwengine.

4. "Nitatumia changamoto zangu kujiimarisha na sio kuniangusha"

Hakuna mafanikio yasiyo na changamoto na ukiona changamoto inakuwa kubwa basi ukkishinda na mafanikio 
yake yanakuwa makubwa.
Yawezekana watu walikutendea uovu lakini wewe ukashikiria upendo dhidi yao.
Badala ya kufunga mlango kuzuia changamoto katika maisha yako fungua ili ukutane nazo zikuimarishe.

5."Bado nina nafasi ya kujifunza zaidi hata kama nimeshindwa baadhi"


Kitu kizuri kwako ni kuwa na moyo wa kutoruhusu anguko la mambo yaliyopita yaendelee kuzuia inuko la mambo yajayo.
Dunia ina fursa nyingi za kujifunza moja, mbili au tatu zinaposhindikana inuka angalia nyingine zaidi na zaidi.
Hakuna jambo kubwa linaweza kukamilika kwa siku chache tu unapaswa uangalie njia mbadala bila kuchoka.

ANZA SASA KUIAMBIA NAFSI YAKO MANENO HAYO
 NAWE UTAONA MABADILIKO UTAKAYO TENGENEZA KATIKA MAISHA YAKO.

NASHUKURU SANA WAFUATILIAJI WA MAKALA ZANGU SABABU MMEKUWA WAVUMILIVU SANA KATIKA KIPINDI CHOTE AMBACHO SIKUWA NA NAFASI YA KUANDIKA NA KUWALETEA MAKALA MPYA LAKINI MMEONYESHA MOYO WA DHATI WA KUTOACHA KUITEMBELEA BLOG YENU.
TUENDELEE KUWA PAMOJA KUELIMISHANA.


1.NINI FAHARI KATIKA MAISHA YANGU?

Ukiwa mtu wa kufuata moyo wako katika kufanya vitu vyako, watu hawatakuwa wanakubaliana na wewe mara kwa mara.
Unapofanikiwa kupata kitu kinachokupa furaha, si kila mtu atakuwa anafurahi kwa ulichogundua.
Ukiwa mkarimu na mnyenyekevu kwa watu bado kuna wengine watakaohoji kwanini unafanya hayo.
Unapokuwa muaminifu kwa watu kuna watu watakaoutumia uaminifu wako kutaka kukuzima.
Ukiamua kuwa msaada kwa watu kuna watu watakaotaka kuutumia msaada huo kukurudisha chini.
Lakini usiruhusu yeyote kati ya watu hawa wakurudishe nyuma kufanya jambo ambalo wewe linakupa fahari na furaha katika maisha yako.
Unachopaswa kujua ni kuwa mwisho wa siku unachopaswa kuangalia ni wewe na furaha yako na si wao.
Itakapofikia wakati ukajiuliza swali, "je, nina fahari na jinsi ninavyoishi?" Jibu liwe ndio.

2.JE, NINALETA MABADILIKO CHANYA KATIKA MAISHA?

Hata kama kuna hali ya kukatisha tamaa, jitahidi kufanya jambo sahihi kila siku.
Kila siku ishi kwa kufuata nguvu ya upendo na ukweli.
Kwani kila siku ukweli na upendo ndio huchomoza juu zaidi.
Endelea kuingiza mazuri yako ulimwenguni, kila unapopata nafasi hata kwa jambo dogo.
Ni katika mkusanyiko wa matendo ya vitu vidogo vidogo ndio vinaleta mabadiliko ulimwenguni.
Unaweza ukawa huoni ni kwa jinsi gani matendo yako mema yanavyoleta mabadiliko kwa sasa lakini muda utakapofika utashuudiwa tu na watu.

3.KITU GANI NATAMANI KUWA NACHO, NA KWA NINI?

Ukishajua jibu la hili swali, jikumbushe kila siku katika maisha yako.
Unatakiwa uchambue, bila shaka yoyote, sababu mahsusi kwanini unafanya shughuli unayofanya.
Mafanikio hutokea pale tu ambapo kuna lengo mahsusi na sababu ya kinachofanywa na mtu husika.
Unapokuwa na sababu ya kufanya shughuli fulani unakuwa na lengo kuu nyuma ya nguvu zako unazowekeza.
Unapoweza kuunganisha sababu na matarajio ya unachotaka upate, utaweza kutengeneza nidhamu na uvumilivu kwa kile unachofanya katika shughuli yako.
Jipe mwenyewe sababu za msingi ili uweze kuyafikia mafanikio kwa nguvu zote.

4.VITU GANI NI VIZUIZI KWANGU?

Kufahamu kizuizi chako, ni njia ya kutambua namna ya kukabiliana nacho.
 Kizuizi siku zote huendelea kuwa kizuizi kama  haujakitambua.
Na endapo unatokea kukitambua kizuizi chako kinakuwa ni changamoto tu.
Angalia katika mazingira yako na bainisha vitu gani ni changamoto kwako halafu vitumie kufungua fursa za maendeleo katika maisha yako.
Ukiweza kuvibainisha vyote utakuwa katika nafasi nzuri ya kufanikiwa kwasababu unajua ulipo, wapi unataka kwenda na una nyenzo gani kufanikisha unachotaka.
Kumbuka njia yenye vikwazo ndio siku zote humpeleka mtu kilele cha juu kabisa.
Na kikubwa si kukwepa vikwazo, bali ni kukabiliana navyo mpaka mwisho.

5.MPANGO WANGU MBADALA NI UPI?

Ni wazi kuwa kila mmoja wetu hukosea katika jambo fulani anapolifanya, lakini unachopaswa kufikiria ni vipi utaweza kuibuka na njia mbadala kutatua tatizo lako.
Anza kuchukua hatua mpya mara unapoona hatua za mwanzo zimeshindikana.
Si lazima uanze na hatua kubwa ili ufike haraka, la, unaweza kuanza na hatua ndogo ndogo ambazo zitakuwa zinakupa nafasi ya kutafakari namna ya kuongeza kasi.
Fanya unalotamani kufanya kwa kutumia rasilimali ulizonazo sasa.

JIJENGEE TABIA YA KUJIULIZA MASWALI KWA KILA JAMBO UNALOFANYA ILI KUJUA KAMA UTAWEZA KUFANIKISHA AU LA.

UKIWEZA KUJIULIZA MASWALI YA HAPO JUU NA ZAIDI UTAJITENGENEZEA NAFASI YA KUSHINDA KILA UNACHOFANYA.

Poleni wadau mnaofuatilia makala za blog hii,
kwani kwa kipindi kirefu sijawaletea makala mpya kutokana na kubanwa na majukumu ya kimasomo,
lakini nawaahidi nitakuwa nawaletea makala mpya kadri muda utakaponiruhusu.
Asanteni kwa kuunga mkono blog hii.


Leo naomba nizungumzie tatizo ambalo nahisi vijana wengi tumekuwa watuhumiwa katika kitendo hiki.
Kujichua ni tabia ya kingono ambayo inapofanywa kwa kiwango kikubwa inaleta matatizo ya kiumbo na kisaikolojia kwa anayefanya tendo hilo.
Na katika kipindi cha zama hizi ambazo majarida, vipindi na hata mitandao mingi inaonyesha picha za ngono ndio kunaifanya tabia hii kushamiri kwa kiwango kikubwa.
Kwani vijana wengi wanaingia katika mchezo huu wa kujiridhisha wenyewe bila kujua madhara yatakayokuja baadaye.

Waelimisha rika wengi wamekuwa wakiwaambia vijana kwamba kujichua ndio njia salama ya ngono kwani hatari ya kupata magonjwa kwako haipo na wanaongezea kuwa wafanye kwa kiwango kidogo pale wanapojisikia hamu ya tendo.
Lakini wanasahau kuwaeleza madhara yake pindi inapofanywa kwa kiwango kikubwa na pia wanajua wazi kuwa mara mtu anapoanza tabia hii kuitawala kwa kiwango inakuwa ngumu.

Baadhi ya madhara ambayo unaweza ukayapata ukifanya kwa muda mrefu:
1.Maumivu ya mgongo kwa chini;
2.Kupoteza nywele;
3.Kupungua nguvu za kiume;
4.Kuwahi kumaliza wakati wa tendo; 
5.Kupoteza uwezo wa kuona vizuri;
6.Maumivu ya kende;
7.Maumivu ya nyonga;
8.Kuchoka sana;
9.Msongo wa mawazo;
10.Kupoteza kumbukumbu kwa haraka

Dhumuni la makala hii ni kumsaidia yule mtu ambaye tayari anafanya mchezo huu atambue madhara yake na pia afahamu namna ya kujinasua kabla mambo hayajawa mabaya.
Kwa wewe muhusika unatakiwa kuwa na hakika kuwa unaweza ukajinasua katika tatizo lako hili. 
Wengi wanaume kwa wanawake waliojaribu kujisaidia kuondokana na hili tatizo wameweza,  hata wewe kwako ni hivyo hivyo ikiwa utajitambua tu.
Kujitambua ni hatua ya kwanza katika safari yako ya kuacha.
Unatakiwa uamue kuwa sasa unaacha na pindi unapoweka uamuzi huo utakuwa unasaidia kujipunguzia ukubwa wa tatizo.
Lakini inatakiwa uwe na zaidi ya tumaini au tamanio la kutambua kuwa uamuzi wa kuacha ni muhimu kwako.
Ni uamuzi tu.
Ukiweka kweli kabisa mawazo yako katika kuliondoa hili tatizo utakuwa na nguvu ya kuweza kuliondoa kabisa na kujiweka pembeni na vishawishi vya kukurudisha katika hiyo tabia.

Utakapo kuwa ushafanya uamuzi wa kuacha anza kufanya yafuatayo:
1.Usiguse wala kuchezea maeneo yako ya siri kwa muda mrefu labda uwe unajisafisha wakati wa kuoga.

2.Tengana na rafiki au marafiki zako ambao unajua wazi kabisa kuwa nao wana tabia hizo kwani usijidanganye kuwa mtaacha wote kwa pamoja kwani mara nyingi kuacha ni juhudi na maamuzi binafsi.

3.Unapokuwa unaoga usikae muda mrefu maeneo hayo jifute na utoke haraka.

4.Lala na nguo inayozifunika sehemu za siri kiasi kwamba sio rahisi kwa wewe kuzigusa mpaka uivue hiyo nguo, hapa itakusaidia kupata muda wa kutafakari kabla hujafanya tendo lolote.

5.Endapo upo kitandani na mawazo ya tendo hilo yakakujia ,nyanyuka na ujaribu kutembea tembea ili kuyapoteza hayo mawazo kichwani mwako.

6.Usisome majarida ya ngono, na kuangalia picha za ngono kwani vitakuchochea urudi katika tatizo.

7.Anza kusoma majarida na makala za mambo mazuri na yenye kuelimisha na itakusaidia kuulisha ubongo taarifa nzuri. 
Mathalani unaweza ukaanza tabia ya kusoma vitabu vya dini itakuasidia sana.

8.Sali, lakini wakati wa kusali usiwe mara kwa mara unalifikiria hili tatizo kwani utaendelea kuliweka mawazoni mwako.

Mtazamo wa mtu mwenyewe ndio unaosaidia kuliondoa hili tatizo kwa haraka.
Ukiweza kutambua kwanini umeingia katika hii tabia, 
na kuyafahamu mazingira yanayokuchochea wewe kuingia huko unatengeneza uwezo wa kuishinda kwa haraka.

 Tabia hii ya kujiridhisha mwenyewe itakufanya uwe mtu kwa kujisikia na hatia kila mara, kutojiheshimu mwenyewe na kukufanya uendelee pindi unapopatwa na msongo wa mawazo.
Na inapelekea unaanza kujiona mdhambi hata kuhudhuria nyumba za ibada kwako inakuwa ngumu.

UAMUZI WA KUACHA UNAWEZA KUUFANYA SASA
KWAAJILI YA AFYA YAKO YA UZAZI NA AKILI.

ANZA JUHUDI NA UTAONA JINSI UNAVYOWEZA KUISHI BILA TABIA HIYO AMBAYO HAINA FAIDA YOYOTE SIKU ZA BAADAYE.

 
Copyright 2013-2017 Lisha Ubongo
| Branded by www.pixelbase.co.tz