Vijana wengi,
 wanapoona wamepata urefu, 
mabadiliko ya mwili, kupanda kielimu,
 na hata kazi 
wanajiona tayari wameshakua.

Katika mazingira ya elimu kama chuo
au kazini,
vijana wengi wamekuwa kitaaluma na kiujuzi, lakini 
kihisia bado wanakuwa ni wadogo lakini wanashindwa kulitambua hilo.
Jibu linaweza kuja kwa haraka kwamba,
hiki ni kizazi cha vijana wanaojua vitu vingi mapema kabla ya umri wao.

Kiuhalisia kijana anatakiwa apate muda wa kukomaa kihisia ili kukabiliana na 
changamoto za ukubwani.

Vijana wengi siku hizi,
 wanatumia taarifa ambazo hawawezi kuzikabili katika umri wao.

Ubongo unakuwa bado hauja komaa kwa shughuli hiyo yeye anakuwa tayari ameshaianza.
Akili yake,
 inazichukua taarifa hizo na kuzihifadhi lakini hisia zake haziko tayari kuzitumia katika namna inayopaswa.

Jamii huwa inafurahi sana kumuona kijana anajitambua na 
anaonyesha ishara za kukua kihisia,
kwa jinsi anavyokabiliana na changamoto kubwa,
katika namna inayostahili.

ZIFUATAZO NI ISHARA ZA KUKUA KIHISIA:

1.KUWA MVUMILIVU

Hii ni ishara inayomtofautisha mtu ambaye amekua na 
yule ambaye hajakua kihisia.
Sifa moja ya watu ambao hawajakua kihisia ni kutosubiria muda muafaka wa kufanya mambo yake,
yawezekana watu wengine wakaumia lakini kwa kuwa yeye amefurahi, 
ni sawa tu.
Aliyekuwa kihisia hata kama
 hilo jambo ni la kumfurahisha,
 atasubiri tu muda muafaka ufike.


2.HAYUMBISHWI NA KUKOSOLEWA

 Aliyekuwa kihisia anaelewa kabisa kwamba,
kukosolewa ni 
sehemu ya kujifunza.
Watu waliokua kihisia,
 huwa wanapokea kukosolewa bila 
kuruhusu ukosoaji huo uharibu mambo yake mengine.
Wanajielewa wanataka nini na wao ni nani.

3.WANAKUWA NA ROHO YA UNYENYEKEVU

Unyenyekevu huwa unaenda sambamba na ukuaji wa hisia.
Unyenyekevu si kuwafikiria wenzako tu 
kwanza na wewe ukajitelekeza,
hapana.
Wanakuwa si watu wa kujipendelea wao 
tu kwa kila kitu.
Ila ni watu wa kwanza 
kutambua kuwa uwezo waliopewa na Mungu
ni kwa ajili ya viumbe na watu wanaoishi nao.

4.WANASIMAMIA MAAMUZI YAO

Wana misimamo inayotawala maamuzi yao,
wako tayari kufuata
 misimamo yao na kupita njia ya maisha waliyochagua kwa 
ujasiri bila kubabaika na wanakuwa tayari kuwajibika kutokana na 
maamuzi yao.
Tabia zao ndio zinaongoza maamuzi yao ya kila siku.

5.WEPESI WA SHUKRANI

Iko wazi kabisa,
 kuwa unavyozidi kukua ndio kuonyesha shukrani kwa watu na Mungu
 si kitu cha kuficha katika mambo madogo
 hadi makubwa
unayofanyiwa.
Mtu ambaye hajakua anaona yote yanayomtokea anayastahili kwahiyo 
kushukuru hawezi.

6.ANATUMIA HEKIMA KABLA HAJAFANYA JAMBO

Mtu ambaye amekuwa anafundishika, 
hajioni kuwa ana majibu 
ya kila kitu.
Jinsi anavyozidi kujua vitu ndivyo anavyozidi kutafuta hekima.
Huwa hawaoni aibu kufuata ushauri kwa mwalimu, au mzazi 
pale anapoona amekwama.

JARIBU KUJICHUNGUZA,
 KAMA UMEKOSA SIFA HATA MOJA KATI YA HIZO HAPO JUU.

 BASI UJUE BADO HUJAKUA KIHISIA
USI HARAKIE VITU AMBAVYO UNAONA KABISA MUDA WAKE BADO.





Kisukari,
ni ugonjwa unaotokea katika mfumo wa mmeng'enyo wa chakula, 
ambapo kiwango cha sukari rahisi(glucose) kinazidi katika damu.
Kawaida, kiwango cha sukari katika damu kinarekebishwa na kemikali 
inayoitwa insulini inayotolewa na
 kongosho.
Hebu tazama video ya mfumo wa chakula ulivyo hapa:

Sasa inapotokea kemikali ya insulini kutoka katika kongosho,
utengenezaji wake ni duni au seli za mwili zinashindwa kuifanyia 
kazi kemikali hiyo 
kama inavyotakiwa,
na hivyo kuruhusu sukari kuongezeka katika damu.

Kuna dalili kadhaa zinazotokea pale sukari inapokuwa imezidi katika damu:

1.Kupatwa na haja ndogo mara nyingi;
2.kiu kali ya maji;
3.kuhisi njaa kali.

Aina za kisukari:

1.KUTOTENGENEZWA KWA INSULINI
Mwili unashindwa kutengeneza kemikali ya insulini,
kwahiyo mhusika huwa ana 
hitaji la kujiwekea 
kemikali hiyo mwilini.
Aina hii inaweza kumpata mtu kabla hajafikisha miaka 40,
sana sana ni kipindi cha ujana.

Asilimia 10 ya wagonjwa wa kisukari wanaugua aina hii ya kwanza.
Mgonjwa atatakiwa ajichome sindano ya kemikali ya insulini 
katika maisha yake yote.
Na mara nyingi huwa
 wanatembea na kifaa 
maalumu cha kupimia kiwango cha sukari katika damu,

mara anapoona imezidi 
anatakiwa ajichome 
sindano ya insulini 
ili kuipunguza katika kiwango maalumu.

2.KIWANGO KIDOGO CHA INSULINI
Katika 
aina hii mwili unashindwa kutengeneza kemikali ya 
insulini ya kutosha,
au mwili unashindwa kuitumia kemikali hiyo.
Asilimia 90 
ya wagonjwa wa kisukari wanaugua aina hii ya pili.

Aina hii inaweza kuzuiwa kwa:
1.Kupunguza uzito;
2.Chakula kamili;
3.Mazoezi mengi;
4.Kufuatilia kiwango cha sukari katika damu.

Na ikiwa aina hii itashindwa kuzuiwa na mgonjwa,
itampeleka katika hatua 
ya kujiwekea kemikali 
ya insulini sana sana kwa njia ya kunywa vidonge.

Tazama video ya aina ya pili ya kisukari hapa:



3.KISUKARI WAKATI WA UJAUZITO
Inawapata sana wakina mama 
wakati wakiwa 
wajawazito,
na kuwafanya wawe na kiwango kikubwa sana cha sukari katika damu.

Inaweza kuzuiwa kwa 
mazoezi na chakula kamili.
Inaposhindwa 
kuzuiwa kwa mama mjamzito inamsababishia matatizo wakati wa kujifungua,
mwili wa mtoto unaweza kuwa mkubwa kuliko unavyopaswa kuwa.

Uchunguzi 
unaonyesha kuwa wanawake wengi ambao lishe yao kabla hawajawa 
wajawazito ilikuwa na 
kiwango kikubwa cha mafuta ya wanyama na chenye kolesto wanakuwa katika 
hatari ya kupata aina hii ya kisukari.

Vitu gani vinaweza kusababisha ugonjwa huu wa kisukari:

1.UZITO KUPITILIZA
Unapokuwa na uzito mkubwa,
unajiweka katika hatari 
ya kupata ugonjwa
 wa kisukari.
Uzito wa mwili kupitiliza unaufanya mwili kutengeneza kemikali 
ambayo inaenda kuvuruga 
mfumo wa mmeng'enyo 
wa chakula.

2.KIWANGO KIDOGO CHA HOMONI ZA TESTOSTERONE
Ikiwa 
mtu atakuwa na 
kiwango kidogo cha utengenezwaji wa homoni hii kutoka katika korodani za mwanaume 
na ovari za mwanamke, 
basi 
kiwango chake 
katika damu kikishuka
kinamuweka mtu katika 
hatari ya kupata aina 
ya pili ya kisukari.

Ndio maana watu wenye umri mkubwa
 hatari inakuwa kubwa 
kwasababu, 
kiwango cha utengezaji wa homoni hii unapungua kiasili,
na kuzuia insulini isifanya kazi yake sawa sawa.

Matatizo yanayoweza kutokea ikiwa utashindwa kuzuia ongezeko la sukari katika damu:

1.Matatizo ya Macho
Glaucoma-kuharibika 
kwa mishipa kuona na 
inaweza kutibiwa kwa 
dawa ya matone ya macho.

Cataracts-ukungu katika macho unazuia kuona vizuri ambao unaweza
 kuondolewa kwa oparesheni
 maalumu ikiwa kuna ulazima.

2.Matatizo ya miguu
3.Matatizo ya ngozi
4.Matatizo ya moyo
5.Matatizo ya kusikia
6.Matatizo ya nguvu za kiume
7.Matatizo ya tumbo
8.Kiharusi
9.Michubuko kushindwa kupona haraka
10.Matatizo ya fizi za meno

Tazama video ya jumla hapa:



HUO NDIO UGONJWA WA KISUKARI KWA UFUPI.


Siku hizi limekuwa ni jambo la kawaida,
kukutana na kijana au mtu mzima
 mwenye alama fulani mwilini.

 Anaonekana ana alama ya michoro mwilini maarufu kama tatuu.
Hapo mwanzo,
 ilikuwa ni michoro maalumu kwa watu wa aina fulani,
 mathalani wahuni, lakini siku hizi michoro hiyo mwili inawekwa na mtu yeyote hata wenye heshima zao.



Kwa siku za karibuni watu wengi wanatumia michoro hiyo 
kuelezea hisia zao.
 Kuwasilisha hisia zao kwa watu wengine,
 kwa kuchora mchoro wa 
aina fulani mwilini mwake.

Yawezekana hata wewe umetamani kuweka alama hii mwilini mwako,
lakini kabla hujafanya hivyo kuna vitu kwanza unapaswa kuvifahamu.

MCHORO WA MWILINI(TATTOO) NI NINI?

Ni alama inayotokea mwilini
 baada ya ngozi kutobolewa
 mpaka ndani,
halafu yale matobo yanajazwa wino maalumu ambao unaonyesha 
alama ya mchoro.

Kuna alama nyingine zinafanywa kienyeji kwa kutumia
 sindano ya kawaida,
na nyingine za siku 
hizi zinatumia mashine maalumu ambayo inapotoboa ngozi inaingiza
 wino moja kwa moja.

Na kitendo hiki kinafanyika bila 
kutumia ganzi,
 kwa hiyo tarajia maumivu 
na damu kutoka.

Kinachoifanya alama hiyo kukaa muda mrefu,
 ni kwa kuwa ngozi 
imetobolewa mpaka ndani.

Ngozi zetu binadamu zina safu mbili za juu zinazofikiwa na sindano wakati wa kuweka alama:

Yakwanza,
 yajuu ambayo ndio huwa ina tabia ya kukua na ndio maana ukiumia bado 
inakuja kufunika lile eneo kwa kuotesha nyingine.

Ya pili,
 ambayo ni ya ndani kabisa ambayo seli zake ni imara sana kwa hiyo, 
inapotobolewa hii na kujazwa wino sio rahisi kufutika.

Mwanzo kabisa waweka hizi alama walikuwa wanatumia sindano kutoboa
 ngozi halafu baadaye 
wanaweka wino kwa juu 
kwa mkono ili alama itokee.

JE, HUWA INAUMA?

Hakuna ubishi kwamba zoezi la kuweka alama mwilini linauma,
 kwasababu ngozi yako inatobolewa mara kibao na sindano ya
 mashine hiyo.

JE, UNAFIKIRIA KUWEKA?
Kama una wazo,
 la kwenda kuweka alama hii mwilini mwako, unapaswa kujua 
katika akili yako
 kuwa lazima ufanye 
katika mazingira salama.

Kwani unapaswa utambue kuwa unachoweka mwilini ni kidonda kilichojazwa wino,
usipokuwa makini kuitunza ndio utakuwa umefungua mlango kwa maradhi mwilini mwako.

Kama una matatizo ya moyo,
 aleji, kisukari, matatizo ya ngozi,
 matatizo ya kinga za 
mwili au ukiwa mjamzito ni vyema ukakwepa kuweka alama hii.

MADHARA YAKE
*Matatizo ya aleji:
 Wino unaoingia ndani ya ngozi yako uwe wa rangi nyekundu, kijani, njano au bluu unaweza ukakusababishia aleji ya ngozi.
Unaweza ukatokwa na vipere vinavyowasha katika eneo uliloweka alama yako.
Na hali hii inaweza kukutokea hata mwaka mmoja baada ya kuweka alama hiyo.

*Ugonjwa wa ngozi:
Uambukizo katika ngozi unaweza ukaleta wekundu katika ngozi yako, kuvimba kwa ngozi,  au maumivu ya muda mrefu, yanaweza kukutokea ukiwa umeweka alama hii.

*Tetenasi:
 Magonjwa ya kuambukiza kwa damu:
Ikiwa sindano iliyotumiwa na muweka hiyo alama ilikuwa ina chembe za damu 
za mtu mwenye maambukizi au 
haijasafishwa kwa muda 
mrefu utakuwa katika
 hatari ya kuambikizwa.  

KWA WEWE UNAYETAMANI KUWEKA ALAMA HII MWILINI MWAKO,
UNAPASWA UWE MAKINI NA UAMUZI WAKO.

KWANI,
UKISHAIWEKA MWILINI GHARAMA YA KUIONDOA NI KUBWA SANA.


JE, UNAWEKA ILI IWEJE?
UNAPASWA KUJIULIZA HILI SWALI.


Kipindi kilichopita tuliona aina za pasipoti zinazotolewa nchini Tanzania na baadhi ya taarifa unazotakiwa kuwa nazo ili uweze kuipata.

Leo tutaangalia hati zitazokusaidia pia upate pasipoti kwa urahisi endapo utaambatanisha katika maombi yako kutokana na aina ya safari unayotaka kufanya:

1.SAFARI BINAFSI

Maombi yako unatakiwa uambatanishe na:
*Ushahidi wa shughuli unayofanya;
*Barua ya mualiko;
*Tiketi ya kurudi;
*Barua ya ruhusa ya mzazi kama muombaji yuko chini ya miaka 18;
*Barua ya ruhusa kutoka kwa muajiri wako kama umeajiriwa;
*Barua kutoka kwa mjumbe wa eneo unalokaa muombaji.

2.SAFARI YA AJIRA

Unatakiwa uambatanishe na:
*Tangazo la kazi;
*Tiketi ya kurudi;
*Barua kutoka kwa mjumbe wa eneo unaloishi.

3.SAFARI YA KIMASOMO

Maombi yako yaambatane na:
*Barua ya kuchaguliwa na shule/chuo;
*Vyeti vyako vya masomo;
*Barua ya udhamini;
*Ushahidi wa malipo kama unajilipia binafsi;
*Barua ya ruhusa kutoka kwa muajiri wako kama umeajiriwa;
*Barua ya ruhusa kutoka kwa mzazi kama una umri chini ya miaka 18.

4.SAFARI YA KIDINI

Maombi yako yanatakiwa yaambatane na:
*Barua ya mualiko;
*Barua kutoka katika taasisi ya dini iliyoandaa safari.

5.SAFARI YA KIMATIBABU

Maombi yako yaambatane na:
*Barua kutoka kwa mganga mkuu;
*Ushahidi wa barua kutoka kwa daktari aliyekuwa anakutibu;
*Barua kutoka wizara ya Afya.

6.SAFARI YA KIMICHEZO

*Barua kutoka shirikisho la mpira TFF au ZFA;
*Barua kutoka katika chama cha michezo kilichosajiliwa;
*Barua ya kualikwa.

7.SAFARI YA SKAUTI

Maombi yanatakiwa yaambatanishwe na:
*Barua kutoka kwa chama husika cha skauti;
*Barua ya ruhusa kutoka kwa mzazi kama una umri chini ya miaka 18;
*Barua ya mualiko.

8.SAFARI YA KIKAZI

Maombi yako yaambatane na:
*Barua kutoka kwa muajiri;
*Barua ya mualiko;
*Kitambulisho chako.

9.SAFARI YA KIBIASHARA

Maombi yako yanatakiwa yaambatanishwe na:
*Leseni halali ya biashara;
*Tiketi ya kurudi.

10.SAFARI YA UBAHARIA

Maombi yako yanatakiwa yaambatane na:
*Mkataba wa ajira;
*Vyeti vya taaluma;
*Barua kutoka kwa umoja wa mabaharia.

MAHITAJI YANAYOTAKIWA ILI UPATE HATI YA KUSAFIRIA:

1.HATI YA KUSAFIRIA YA DHARURA
Maombi yako yanatakiwa yaambatane na:
*Picha nne ndogo za pasipoti

2.CHETI CHA UTAMBULISHO
Muombaji wa cheti cha utambulisho anatakiwa awe na:
*Ripoti maalumu ya polisi ikiwa hakuna ubalozi;
*Picha mbili za pasipoti.

3.HATI YA KUSAFIRIA YA AGANO LA GENEVA
Muombaji wa hati hii anatakiwa awe na:
*Barua kutoka kwa mkurugenzi anayesimamia idara ya wakimbizi;
*Nakala ya kitambulisho cha ukimbizi;
*Picha mbili za pasipoti.

MAOMBI YA KUBADILISHIWA PASIPOTI NA HATI ZA KUSAFIRIA ZILIZOHARIBIKA:

Ikiwa pasipoti au hati yako ya kusafiria imeharibika kabisa au 
iko katika hali ambayo ni 
lazima ibadilishwe, 
muombaji anatakiwa 
atume maombi kwenda kwa 
kamishna wa huduma za uhamiaji.

1.KUBADILISHIWA PASIPOTI
Muombaji anatakiwa awe na:
*Pasipoti iliyoharibika;
*Picha nne za pasipoti.

2.KUBADILISHIWA HATI YA KUSAFIRIA
Muombaji anatakiwa awe na:
*Hati za kusafiria zilizoharibika;
*Picha mbili za pasipoti.

MAOMBI YA KUTENGENEZEWA PASIPOTI MPYA KWA ILIYOPOTEA AU KUIBWA:

Ikiwa pasipoti imepotea au kuibiwa maombi ya kutengenezewa mpya 
yanatakiwa yaambatane 
na kiapo pamoja 
ripoti ya mamlaka ambayo
 muombaji alitoa taarifa ya kupotelewa au kuibiwa.

Muombaji anatakiwa awe na:
*Ripoti kutoka katika kituo cha polisi alichopeleka taarifa ya kuibiwa;
*Taarifa uliyotoa kupotelewa na pasipoti katika gazeti la kila siku.

KUBATILISHWA PASIPOTI AU HATI YA KUSAFIRIA

Kamishna wa idara ya uhamiaji katika muda wowote ana mamlaka ya 
kubatilisha pasipoti au 
hati ya kusafiria kwa aliyepewa ikiwa aliyenayo amefanya yafuatayo:

*Ameruhusu pasipoti yake itumiwe na mtu mwengine;
*Amefukuzwa nchini na serikali;
*Ikiwa aliyenayo amesitisha uraia wake wa Tanzania;
*Ikiwa aliyenayo amejihusisha na biashara ya madawa ya kulevya, 
utengenezaji wa hela bandia, kuingiza isivyo halali wahamiaji, 
amejihusisha na ugaidi, 
na hata uhamishaji wa hela kimagendo;
*Ikiwa kwa ajili ya kulinda usalama wa nchi.

ADA YA MAOMBI YA PASIPOTI NA HATI ZA KUSAFIRIA:
1.Pasipoti ya kawaida-50,000/=

2.Pasipoti ya kidiplomasia-50,000/=

3.Pasipoti ya huduma-50,000/=

4.Pasipoti ya afrika Mashariki-15,000/=

5.Hati ya kusafiria ya dharura-10,000/=

6.Chet cha utambulisho-10,000/=

7.Hati ya kusafiria ya agano la Geneva-20,000/=

SASA KAZI INABAKI KWAKO,
 KUWA NA MAHITAJI HAYO MUHIMU WAKATI UNAOMBA PASIPOTI AU HATI YA KUSAFIRIA ILI USIJE KUSUMBUKA.






 
Copyright 2013-2017 Lisha Ubongo
| Branded by www.pixelbase.co.tz