JE, UNA UFAHAMU UGONJWA WA KISUKARI? SOMA HAPA UJIELIMISHE.

Kisukari,
ni ugonjwa unaotokea katika mfumo wa mmeng'enyo wa chakula, 
ambapo kiwango cha sukari rahisi(glucose) kinazidi katika damu.
Kawaida, kiwango cha sukari katika damu kinarekebishwa na kemikali 
inayoitwa insulini inayotolewa na
 kongosho.
Hebu tazama video ya mfumo wa chakula ulivyo hapa:

Sasa inapotokea kemikali ya insulini kutoka katika kongosho,
utengenezaji wake ni duni au seli za mwili zinashindwa kuifanyia 
kazi kemikali hiyo 
kama inavyotakiwa,
na hivyo kuruhusu sukari kuongezeka katika damu.

Kuna dalili kadhaa zinazotokea pale sukari inapokuwa imezidi katika damu:

1.Kupatwa na haja ndogo mara nyingi;
2.kiu kali ya maji;
3.kuhisi njaa kali.

Aina za kisukari:

1.KUTOTENGENEZWA KWA INSULINI
Mwili unashindwa kutengeneza kemikali ya insulini,
kwahiyo mhusika huwa ana 
hitaji la kujiwekea 
kemikali hiyo mwilini.
Aina hii inaweza kumpata mtu kabla hajafikisha miaka 40,
sana sana ni kipindi cha ujana.

Asilimia 10 ya wagonjwa wa kisukari wanaugua aina hii ya kwanza.
Mgonjwa atatakiwa ajichome sindano ya kemikali ya insulini 
katika maisha yake yote.
Na mara nyingi huwa
 wanatembea na kifaa 
maalumu cha kupimia kiwango cha sukari katika damu,

mara anapoona imezidi 
anatakiwa ajichome 
sindano ya insulini 
ili kuipunguza katika kiwango maalumu.

2.KIWANGO KIDOGO CHA INSULINI
Katika 
aina hii mwili unashindwa kutengeneza kemikali ya 
insulini ya kutosha,
au mwili unashindwa kuitumia kemikali hiyo.
Asilimia 90 
ya wagonjwa wa kisukari wanaugua aina hii ya pili.

Aina hii inaweza kuzuiwa kwa:
1.Kupunguza uzito;
2.Chakula kamili;
3.Mazoezi mengi;
4.Kufuatilia kiwango cha sukari katika damu.

Na ikiwa aina hii itashindwa kuzuiwa na mgonjwa,
itampeleka katika hatua 
ya kujiwekea kemikali 
ya insulini sana sana kwa njia ya kunywa vidonge.

Tazama video ya aina ya pili ya kisukari hapa:



3.KISUKARI WAKATI WA UJAUZITO
Inawapata sana wakina mama 
wakati wakiwa 
wajawazito,
na kuwafanya wawe na kiwango kikubwa sana cha sukari katika damu.

Inaweza kuzuiwa kwa 
mazoezi na chakula kamili.
Inaposhindwa 
kuzuiwa kwa mama mjamzito inamsababishia matatizo wakati wa kujifungua,
mwili wa mtoto unaweza kuwa mkubwa kuliko unavyopaswa kuwa.

Uchunguzi 
unaonyesha kuwa wanawake wengi ambao lishe yao kabla hawajawa 
wajawazito ilikuwa na 
kiwango kikubwa cha mafuta ya wanyama na chenye kolesto wanakuwa katika 
hatari ya kupata aina hii ya kisukari.

Vitu gani vinaweza kusababisha ugonjwa huu wa kisukari:

1.UZITO KUPITILIZA
Unapokuwa na uzito mkubwa,
unajiweka katika hatari 
ya kupata ugonjwa
 wa kisukari.
Uzito wa mwili kupitiliza unaufanya mwili kutengeneza kemikali 
ambayo inaenda kuvuruga 
mfumo wa mmeng'enyo 
wa chakula.

2.KIWANGO KIDOGO CHA HOMONI ZA TESTOSTERONE
Ikiwa 
mtu atakuwa na 
kiwango kidogo cha utengenezwaji wa homoni hii kutoka katika korodani za mwanaume 
na ovari za mwanamke, 
basi 
kiwango chake 
katika damu kikishuka
kinamuweka mtu katika 
hatari ya kupata aina 
ya pili ya kisukari.

Ndio maana watu wenye umri mkubwa
 hatari inakuwa kubwa 
kwasababu, 
kiwango cha utengezaji wa homoni hii unapungua kiasili,
na kuzuia insulini isifanya kazi yake sawa sawa.

Matatizo yanayoweza kutokea ikiwa utashindwa kuzuia ongezeko la sukari katika damu:

1.Matatizo ya Macho
Glaucoma-kuharibika 
kwa mishipa kuona na 
inaweza kutibiwa kwa 
dawa ya matone ya macho.

Cataracts-ukungu katika macho unazuia kuona vizuri ambao unaweza
 kuondolewa kwa oparesheni
 maalumu ikiwa kuna ulazima.

2.Matatizo ya miguu
3.Matatizo ya ngozi
4.Matatizo ya moyo
5.Matatizo ya kusikia
6.Matatizo ya nguvu za kiume
7.Matatizo ya tumbo
8.Kiharusi
9.Michubuko kushindwa kupona haraka
10.Matatizo ya fizi za meno

Tazama video ya jumla hapa:



HUO NDIO UGONJWA WA KISUKARI KWA UFUPI.


Share this post:

Digg it StumbleUpon del.icio.us Google Yahoo! reddit

0 comments:

Post a Comment

 
Copyright 2013-2017 Lisha Ubongo
| Branded by www.pixelbase.co.tz