Kipindi kilichopita tuliona aina za pasipoti zinazotolewa nchini Tanzania na baadhi ya taarifa unazotakiwa kuwa nazo ili uweze kuipata.

Leo tutaangalia hati zitazokusaidia pia upate pasipoti kwa urahisi endapo utaambatanisha katika maombi yako kutokana na aina ya safari unayotaka kufanya:

1.SAFARI BINAFSI

Maombi yako unatakiwa uambatanishe na:
*Ushahidi wa shughuli unayofanya;
*Barua ya mualiko;
*Tiketi ya kurudi;
*Barua ya ruhusa ya mzazi kama muombaji yuko chini ya miaka 18;
*Barua ya ruhusa kutoka kwa muajiri wako kama umeajiriwa;
*Barua kutoka kwa mjumbe wa eneo unalokaa muombaji.

2.SAFARI YA AJIRA

Unatakiwa uambatanishe na:
*Tangazo la kazi;
*Tiketi ya kurudi;
*Barua kutoka kwa mjumbe wa eneo unaloishi.

3.SAFARI YA KIMASOMO

Maombi yako yaambatane na:
*Barua ya kuchaguliwa na shule/chuo;
*Vyeti vyako vya masomo;
*Barua ya udhamini;
*Ushahidi wa malipo kama unajilipia binafsi;
*Barua ya ruhusa kutoka kwa muajiri wako kama umeajiriwa;
*Barua ya ruhusa kutoka kwa mzazi kama una umri chini ya miaka 18.

4.SAFARI YA KIDINI

Maombi yako yanatakiwa yaambatane na:
*Barua ya mualiko;
*Barua kutoka katika taasisi ya dini iliyoandaa safari.

5.SAFARI YA KIMATIBABU

Maombi yako yaambatane na:
*Barua kutoka kwa mganga mkuu;
*Ushahidi wa barua kutoka kwa daktari aliyekuwa anakutibu;
*Barua kutoka wizara ya Afya.

6.SAFARI YA KIMICHEZO

*Barua kutoka shirikisho la mpira TFF au ZFA;
*Barua kutoka katika chama cha michezo kilichosajiliwa;
*Barua ya kualikwa.

7.SAFARI YA SKAUTI

Maombi yanatakiwa yaambatanishwe na:
*Barua kutoka kwa chama husika cha skauti;
*Barua ya ruhusa kutoka kwa mzazi kama una umri chini ya miaka 18;
*Barua ya mualiko.

8.SAFARI YA KIKAZI

Maombi yako yaambatane na:
*Barua kutoka kwa muajiri;
*Barua ya mualiko;
*Kitambulisho chako.

9.SAFARI YA KIBIASHARA

Maombi yako yanatakiwa yaambatanishwe na:
*Leseni halali ya biashara;
*Tiketi ya kurudi.

10.SAFARI YA UBAHARIA

Maombi yako yanatakiwa yaambatane na:
*Mkataba wa ajira;
*Vyeti vya taaluma;
*Barua kutoka kwa umoja wa mabaharia.

MAHITAJI YANAYOTAKIWA ILI UPATE HATI YA KUSAFIRIA:

1.HATI YA KUSAFIRIA YA DHARURA
Maombi yako yanatakiwa yaambatane na:
*Picha nne ndogo za pasipoti

2.CHETI CHA UTAMBULISHO
Muombaji wa cheti cha utambulisho anatakiwa awe na:
*Ripoti maalumu ya polisi ikiwa hakuna ubalozi;
*Picha mbili za pasipoti.

3.HATI YA KUSAFIRIA YA AGANO LA GENEVA
Muombaji wa hati hii anatakiwa awe na:
*Barua kutoka kwa mkurugenzi anayesimamia idara ya wakimbizi;
*Nakala ya kitambulisho cha ukimbizi;
*Picha mbili za pasipoti.

MAOMBI YA KUBADILISHIWA PASIPOTI NA HATI ZA KUSAFIRIA ZILIZOHARIBIKA:

Ikiwa pasipoti au hati yako ya kusafiria imeharibika kabisa au 
iko katika hali ambayo ni 
lazima ibadilishwe, 
muombaji anatakiwa 
atume maombi kwenda kwa 
kamishna wa huduma za uhamiaji.

1.KUBADILISHIWA PASIPOTI
Muombaji anatakiwa awe na:
*Pasipoti iliyoharibika;
*Picha nne za pasipoti.

2.KUBADILISHIWA HATI YA KUSAFIRIA
Muombaji anatakiwa awe na:
*Hati za kusafiria zilizoharibika;
*Picha mbili za pasipoti.

MAOMBI YA KUTENGENEZEWA PASIPOTI MPYA KWA ILIYOPOTEA AU KUIBWA:

Ikiwa pasipoti imepotea au kuibiwa maombi ya kutengenezewa mpya 
yanatakiwa yaambatane 
na kiapo pamoja 
ripoti ya mamlaka ambayo
 muombaji alitoa taarifa ya kupotelewa au kuibiwa.

Muombaji anatakiwa awe na:
*Ripoti kutoka katika kituo cha polisi alichopeleka taarifa ya kuibiwa;
*Taarifa uliyotoa kupotelewa na pasipoti katika gazeti la kila siku.

KUBATILISHWA PASIPOTI AU HATI YA KUSAFIRIA

Kamishna wa idara ya uhamiaji katika muda wowote ana mamlaka ya 
kubatilisha pasipoti au 
hati ya kusafiria kwa aliyepewa ikiwa aliyenayo amefanya yafuatayo:

*Ameruhusu pasipoti yake itumiwe na mtu mwengine;
*Amefukuzwa nchini na serikali;
*Ikiwa aliyenayo amesitisha uraia wake wa Tanzania;
*Ikiwa aliyenayo amejihusisha na biashara ya madawa ya kulevya, 
utengenezaji wa hela bandia, kuingiza isivyo halali wahamiaji, 
amejihusisha na ugaidi, 
na hata uhamishaji wa hela kimagendo;
*Ikiwa kwa ajili ya kulinda usalama wa nchi.

ADA YA MAOMBI YA PASIPOTI NA HATI ZA KUSAFIRIA:
1.Pasipoti ya kawaida-50,000/=

2.Pasipoti ya kidiplomasia-50,000/=

3.Pasipoti ya huduma-50,000/=

4.Pasipoti ya afrika Mashariki-15,000/=

5.Hati ya kusafiria ya dharura-10,000/=

6.Chet cha utambulisho-10,000/=

7.Hati ya kusafiria ya agano la Geneva-20,000/=

SASA KAZI INABAKI KWAKO,
 KUWA NA MAHITAJI HAYO MUHIMU WAKATI UNAOMBA PASIPOTI AU HATI YA KUSAFIRIA ILI USIJE KUSUMBUKA.






Share this post:

Digg it StumbleUpon del.icio.us Google Yahoo! reddit

1 comments:

Unknown

mdau uko juu saana ntaktafta unpe uzoefu katka kuendeleza blog

Post a Comment

 
Copyright 2013-2017 Lisha Ubongo
| Branded by www.pixelbase.co.tz