Siku hizi limekuwa ni jambo la kawaida,
kukutana na kijana au mtu mzima
 mwenye alama fulani mwilini.

 Anaonekana ana alama ya michoro mwilini maarufu kama tatuu.
Hapo mwanzo,
 ilikuwa ni michoro maalumu kwa watu wa aina fulani,
 mathalani wahuni, lakini siku hizi michoro hiyo mwili inawekwa na mtu yeyote hata wenye heshima zao.



Kwa siku za karibuni watu wengi wanatumia michoro hiyo 
kuelezea hisia zao.
 Kuwasilisha hisia zao kwa watu wengine,
 kwa kuchora mchoro wa 
aina fulani mwilini mwake.

Yawezekana hata wewe umetamani kuweka alama hii mwilini mwako,
lakini kabla hujafanya hivyo kuna vitu kwanza unapaswa kuvifahamu.

MCHORO WA MWILINI(TATTOO) NI NINI?

Ni alama inayotokea mwilini
 baada ya ngozi kutobolewa
 mpaka ndani,
halafu yale matobo yanajazwa wino maalumu ambao unaonyesha 
alama ya mchoro.

Kuna alama nyingine zinafanywa kienyeji kwa kutumia
 sindano ya kawaida,
na nyingine za siku 
hizi zinatumia mashine maalumu ambayo inapotoboa ngozi inaingiza
 wino moja kwa moja.

Na kitendo hiki kinafanyika bila 
kutumia ganzi,
 kwa hiyo tarajia maumivu 
na damu kutoka.

Kinachoifanya alama hiyo kukaa muda mrefu,
 ni kwa kuwa ngozi 
imetobolewa mpaka ndani.

Ngozi zetu binadamu zina safu mbili za juu zinazofikiwa na sindano wakati wa kuweka alama:

Yakwanza,
 yajuu ambayo ndio huwa ina tabia ya kukua na ndio maana ukiumia bado 
inakuja kufunika lile eneo kwa kuotesha nyingine.

Ya pili,
 ambayo ni ya ndani kabisa ambayo seli zake ni imara sana kwa hiyo, 
inapotobolewa hii na kujazwa wino sio rahisi kufutika.

Mwanzo kabisa waweka hizi alama walikuwa wanatumia sindano kutoboa
 ngozi halafu baadaye 
wanaweka wino kwa juu 
kwa mkono ili alama itokee.

JE, HUWA INAUMA?

Hakuna ubishi kwamba zoezi la kuweka alama mwilini linauma,
 kwasababu ngozi yako inatobolewa mara kibao na sindano ya
 mashine hiyo.

JE, UNAFIKIRIA KUWEKA?
Kama una wazo,
 la kwenda kuweka alama hii mwilini mwako, unapaswa kujua 
katika akili yako
 kuwa lazima ufanye 
katika mazingira salama.

Kwani unapaswa utambue kuwa unachoweka mwilini ni kidonda kilichojazwa wino,
usipokuwa makini kuitunza ndio utakuwa umefungua mlango kwa maradhi mwilini mwako.

Kama una matatizo ya moyo,
 aleji, kisukari, matatizo ya ngozi,
 matatizo ya kinga za 
mwili au ukiwa mjamzito ni vyema ukakwepa kuweka alama hii.

MADHARA YAKE
*Matatizo ya aleji:
 Wino unaoingia ndani ya ngozi yako uwe wa rangi nyekundu, kijani, njano au bluu unaweza ukakusababishia aleji ya ngozi.
Unaweza ukatokwa na vipere vinavyowasha katika eneo uliloweka alama yako.
Na hali hii inaweza kukutokea hata mwaka mmoja baada ya kuweka alama hiyo.

*Ugonjwa wa ngozi:
Uambukizo katika ngozi unaweza ukaleta wekundu katika ngozi yako, kuvimba kwa ngozi,  au maumivu ya muda mrefu, yanaweza kukutokea ukiwa umeweka alama hii.

*Tetenasi:
 Magonjwa ya kuambukiza kwa damu:
Ikiwa sindano iliyotumiwa na muweka hiyo alama ilikuwa ina chembe za damu 
za mtu mwenye maambukizi au 
haijasafishwa kwa muda 
mrefu utakuwa katika
 hatari ya kuambikizwa.  

KWA WEWE UNAYETAMANI KUWEKA ALAMA HII MWILINI MWAKO,
UNAPASWA UWE MAKINI NA UAMUZI WAKO.

KWANI,
UKISHAIWEKA MWILINI GHARAMA YA KUIONDOA NI KUBWA SANA.


JE, UNAWEKA ILI IWEJE?
UNAPASWA KUJIULIZA HILI SWALI.


Share this post:

Digg it StumbleUpon del.icio.us Google Yahoo! reddit

2 comments:

Post a Comment

 
Copyright 2013-2017 Lisha Ubongo
| Branded by www.pixelbase.co.tz