Haya ni makosa ambayo 
tunayafanya bila kujua, 
kwasababu
 katika muda huo,
 tunakuwa hatuna njia ya kumfanya aliyeondokewa na mali au mtu ajisikie tuko pamoja naye katika machungu.

Na kwakuwa 
ni vigumu kwa muhusika kukueleza kwamba nataka kufanyiwa
 au kuambiwa kitu fulani ndio nitajisikia vizuri,
 inakubidi utumie ujuzi wako binafsi
 kutafuta njia ya kumfanya
 ajisikie vizuri.

Hapo sasa balaa ndio linaanza,
kwani mara nyingi
 maneno tunayochagua kumwambia
 aliyepotelewa hayamfanyi ajisikie poa
 bali yanamfanya aanze kutafakari ulikuwa na maana gani.

Na hii inatokana
 na si wote wana uwezo wa kutafakari 
kauli zinazotolewa 
na watu wengine katika 
mtazamo chanya.

Hebu tuangalie maneno ambayo hupaswi kuyasema  kwa muhusika:

1."Shukuru (ameishi/umeishi nacho) miaka mingi"

Unapoongea kauli kama hii inampa picha 
mtu huyo,
 kwamba jambo hilo 
lilipaswa kutokea kwake,
na hivyo hapaswi kuhuzunika.
Yawezekana kuna ukweli ndani yake,
 lakini 
unapoongea mbele ya muhusika haitamfanya ajisikie vizuri.

2."Muda wake ulifika"

Hata kama umekosa la kuongea hii kauli 
sio kabisa,
itamfanya akuone umefurahia 
tukio hilo.

3."Alikosea/Ulikosea sana ku.... "

Ikiwa tukio lilikuwa la ajali, 
hata kama liliempata alisababisha 
usiongee kauli kama hii 
kwa muhusika,
itaonekana kana kwamba alifanya uzembe na alistahili kupatwa na hilo.

4."Kuna sababu ya kila kitu"

Hii  kauli kweli ina maana,
 unapofikiria kwa kina lakini si nzuri kuizungumza 
kwa mtu aliye kwenye
 majonzi.

5."Usihofu utampata mwengine tu"

Ikiwa mtu amepoteza mtoto,
 mume au mke, 
kauli ya kumwambia kwamba 
asihuzunike na kuwa 
atapata mwengine tu,
itamfanya aone hukuwahi kuona umuhimu wa aliyeondokewa naye,
na ulikuwa unaombea hilo litokee.

Mara nyingi maneno haya yanapotamkwa na muhusika yanakuwa na 
matumaini zaidi kuliko yanapotamkwa na mtu mwengine wa pembeni. 

Ni heri utumie maneno kama:

1."Pole sana kwa yaliyotokea" 

2."Natamani ningekuwa na maneno mazuri ya kukueleza ujisikie vizuri"

3."Niko pamoja nawe katika hili"

4."Niko pamoja nawe katika sala"

5."Tulimpenda wote"

6."Ukihitaji msaada, niko hapa kwa ajili yako"

TABIA YA KUWAFARIJI WENZETU WANAPOPATWA
 NA MATATIZO,
NI NZURI SANA NA ITAWAFANYA 
WAJISIKIE VIZURI.

KWELI YAWEZEKANA UNA TAFSIRI YAKO 
MOYONI JUU YA TUKIO 
LILILOTOKEA,
 LAKINI IWEKE MOYONI UKIONA HAITAMFARIJI MUHUSIKA.

WOTE TUNAWEZA KUWA TUMAINI KWA WENGINE 
PALE WANAPOPATWA NA
 MATATIZO 
KWA KUTUMIA MANENO NA NJIA SAHIHI 
KUELEZEA HISIA ZETU PIA.

Share this post:

Digg it StumbleUpon del.icio.us Google Yahoo! reddit

0 comments:

Post a Comment

 
Copyright 2013-2017 Lisha Ubongo
| Branded by www.pixelbase.co.tz