Mwanafunzi ni mtu yeyote
 aliye katika mazingira ya 
kujifunza kitu fulani
 katika maisha,
iwe kazini, 
shuleni au hata mtaani.

Lakini tabia za mwanafunzi mmoja zinatofautiana na tabia 
za mwengine katika 
namna wanavyopokea mafundisho 
na kuyafanyia 
kazi kwa vitendo.

Kuna sifa ambazo duniani kote
 zinatumika kumtambulisha mwanafunzi 
bora ni yupi.

Ni kitu kizuri ikiwa kila mtu 
ambaye yupo katika 
mazingira ya kujifunza akafahamu 
sifa za mtu anayejifunza 
ni zipi.
Uwe popote pale katika 
mazingira ya dunia hii bado 
kuna kitu cha 
wewe kujifunza.

Jinsi utakavyokielewa na kukitumia 
itatokana na wewe mwenyewe 
utakavyoweka mawazo na 
akili yako mahali hapo.

Sifa za mwanafunzi bora ni kama zifuatazo:

1.TABIA YA KUJIFUNZA VIPYA

Haina shaka yoyote kuwa 
mwanafunzi bora ana tabia 
ya kuwa tayari kujifunza 
kitu kipya hata kama 
hakijamvutia kwa mara ya kwanza.

2.UWEZO WA KUTENDA

Mwanafunzi bora ni yule mwenye 
uwezo wa kuchukua 
alichojifunza na kukiweka 
katika matendo katika 
hali ya ubunifu wake.

3.MTAZAMO CHANYA

Mwanafunzi bora ni yule mwenye 
mtazamo chanya juu ya
 mambo anayojifunza, 
na ambaye anajijengea uwezo 
mkubwa wa kutafsiri na 
kuhoji mafundisho katika 
namna ya kutaka 
kuelewa zaidi.

4.NIDHAMU BINAFSI

Mwenye uwezo wa kutawala muda wake, 
anakuwa na sifa ya 
kuwasilisha kazi kwa 
wakati uliopangwa.


5.KUTAKA KUELEWA

Mwanafunzi mzuri ni yule 
anayejifunza na 
kuelewa na 
si kukariri maandishi na 
maelezo tu.

Vitu gani ufanye ili uwe mwanafunzi bora:

1.TAFUTA VICHOCHEO
Ili uwe mwanafunzi mzuri 
ni lazima utafute kitu 
cha kukuchochea.
Na hii itakuja kichwani 
mwako ikiwa utakuwa unajiuliza swali la
 "ili iweje?" 
Kama unasoma kwa bidii halafu 
hujui unataka upate nini
 baada ya hapo,
utakuwa unajiweka katika 
wakati mgumu.
Na utakuwa katika mazingira 
ya popote utakapoangukia 
kwako ni sawa tu.

2.WEKA MKAZO
Kuweka mkazo kwenye kujifunza 
kunatokana na shauku unayoweka
katika
 maisha yako.
Ukiweka mkazo katika 
kile unachojifunza utakuwa 
unajitengezea 
mazingira ya 
kutaka kujua zaidi.


3.TABIA
Moja kati ya vitu vitakavyoamua kesho
 uwe wapi ni tabia 
yako unayofanya leo.
Heshimu wakubwa, 
na usiwe unanyanyasa wanafunzi au 
watu wengine wa karibu.
Ukiwa na tabia ya kutowatendea wengine 
vile ambavyo wewe 
hupendi kutendewa utafanya mazingira yako ya kujifunza kuwa bora.
Kuwa msaada kwa wenzako pale wanapokwama kwani hilo ndilo 
watakalo likumbuka kwako,
usifanye ili usifiwe
 ila fanya ukijua unalomtenda 
leo mwenzako na wewe utakuja 
kutendewa hivyo hivyo.

KILA MMOJA WETU ANA NAFASI YA KUWA MWANAFUNZI BORA KATIKA YALE ANAYOJIFUNZA.

 KINACHOTAKIWA NI UJUE TU UNATAKIWA UFANYE NINI NA KWA WAKATI GANI.

Share this post:

Digg it StumbleUpon del.icio.us Google Yahoo! reddit

2 comments:

Anonymous

Asante sana mwandixhi

Post a Comment

 
Copyright 2013-2017 Lisha Ubongo
| Branded by www.pixelbase.co.tz