Mtu wa mfano, 
ni yule ambaye tabia yake mbele ya jamii husika inakubalika na 
wengi wanatamani 
kuwa kama yeye.

Mtu huyu,
 huwa anaangaliwa kama mfano pale watu mwengine wanapotaka 
kufanya majukumu fulani;
iwe ya uwanafunzi, urafiki, ujirani, 
kazini, au sanaa na
 hata michezo.

Yawezekana kila mmoja wetu
 ana mtu wake anayemuangalia 
kama mtu wake wa mfano.

Hasa mtu anapokuwa katika rika 
la kuanza kujitambua, 
mara nyingi
 huanza kwanza kuvutiwa na sifa za watu wengine anaowaona
kila siku.

Na ndio maana,
 unatakiwa kuwa makini sana
 mtoto wako kipindi cha ukuaji,
 anachangamana au kuwaangalia watu wa aina gani.
Kwa mtoto,
 haitajalisha huyo mtu aliyevutiwa naye anafanya jambo jema au baya.
 Kama amevutiwa jinsi anavyofanya
 na yeye 
atataka kuwa kama huyo mtu 
kwa kufuata njia zake.

Unapobahatika kuvutiwa na mtu, 
 na ukamchagua kuwa 
mtu wako wa mfano,
 anaweza kuwa 
chanzo cha wewe kufikia mafanikio 
fulani unayotamani
 kuwa nayo.

Ikiwa mtu wako wa mfano yuko 
karibu na mazingira yako 
unaweza ukafanya hili:

1.TAFUTA NAFASI YA KUZUNGUMZA NAYE

Hii ni hatua ya kwanza,
 unaweza kuitumia 
kumfahamu mtu wako wa
 mfano kiundani njia alizopitia 
kuwa hapo alipo.
Usifiche hisia zako kumueleza jinsi gani unavutiwa na tabia yake na 
ungependa kuwa 
kama yeye.
Hiyo itamfanya ajisikie vizuri,
 na akupe ushirikiano, 
kwa kuwa kila binadamu anapenda 
awe anavutia wengine.

*USIMUULIZE MASWALI MAGUMU

Unapopata nafasi,
 ya kuzungumza na mtu wako 
wa mfano haina maana kwamba,
 amekuamini vya kutosha 
kukuelezea kila kitu 
kuhusu njia alizopitia.

Ila,
 kuwa na maswali mepesi 
ambayo yatamfanya yeye wakati anakuelezea aguse 
eneo ambalo wewe haungeweza 
kumuuliza kwa urahisi.
Hata kama haujakutana naye 
uso kwa uso lakini umeweza kuwasiliana naye kwa njia nyingine 
za kieletroniki,
kuwa makini katika 
kuuliza maswali.

*JENGA SHAUKU

Njia yoyote ya kujifunza jambo,
 kwa ufanisi ni kuweka shauku ya 
kutaka kujua zaidi,
wakati unazungumza naye hata kama kuna kipengele unaona hakija 
kuvutia tengeneza shauku ili upate 
kujifunza zaidi 
kutoka kwake.

Yafuatayo ndio unapaswa kufanya baada ya kuchagua mtu wako wa mfano:

1.IGA MEMA ANAYOFANYA/ALIYOFANYA

Usitarajie kwamba,
 kila tendo analotenda mtu wako wa mfano ukilifanya wewe pia 
litakuwa jema.

Yawezekana
 mtu wako wa mfano umesoma 
njia zake alizopitia kupitia 
maandishi na wala sio 
kutoka mdomoni mwake,
 unapaswa utambue
 jamii zinatofauti ya kutafsiri 
matendo.

Kama ni rafiki kwa kila mtu,
 na wewe kuwa hivyo, 
kama ni mtu wa kutabasamu, 
nawe fanya hivyo, 
na kama anasaidia watu na wewe usisite 
kufanya hivyo pale 
unapokuwa na uwezo huo.

2.SOMA WASIFU WAKE MARA KWA MARA

Unapokuwa na tabia ya kusoma
 wasifu wa 
mtu wako wa mfano,
itakusaidia kufahamu kwa nini 
aliweza kufanya 
anachofanya sasa.

3.TAFUTA MTU WAKE WA MFANO ALIKUWA NANI

Hii itakusaidia,
 kujua kuwa yeye aliweza 
kiasi gani kufanikiwa kupitia mtu 
wake huyo wa mfano na 
tofauti yao iko wapi.

Kila mmoja wetu anaweza kuwa mtu wa mfano katika jamii yake kwa kufanya yafuatayo:

1.JITAMBUE

Ukitaka kuwa mtu wa mfano,
 katika jamii yako
 ni lazima kwanza 
uwe wewe umejitambua.
 Unataka kuwa nani na kwa nini.
Hii itakupelekea ufanikiwe katika yule unayetamani kuwa.
Hii itawafanya wanaokuangalia wapate
 shauku ya kutaka kujifunza 
zaidi kupitia wewe.

2.KUWA NA MSIMAMO

Kama umechagua kufanya jambo fulani,
 na jamii ikajua wazi
 kwamba wewe unafanya hilo jambo 
usiwe kigeu geu. 
Utawachanganya watu
 wasijue unataka nini hasa.
Kama ulichagua siasa 
na ukakutana na ugumu 
endelea kupambana mpaka upate suluhisho
 sio ugumu kidogo tu 
ushabadilisha msimamo.
Hakuna mtu atakaye tamani 
kuwa na mtu wa mfano asiyejielewa.

3.ISHI NDOTO ZAKO

Kama ulitamani siku moja 
ukipata kitu fulani ndio 
roho yako itafurahia,
ukipata huo uwezo usisite
 kufanya hilo.
 Kwani 
utawafanya watu 
wengine waone wewe ni 
mfanikishaji ndoto hivyo 
unapaswa kuigwa.

4.SAIDIA WATU WENGINE

Chagua kuwa mtu mzuri,
 na wa msaaada kwa watu wengine.
Wapokee wengine
 maishani mwako.
 Ukipokea watu vile walivyo 
utawafanya wajione wana thamani 
mbele yako nao pia watatamani 
kuwa kama wewe.

5.TIMIZA MAJUKUMU YAKO

Kama ni mzazi,
 fanya mazungumzo na watoto wako
 na kufuatilia maendeleo yake/yao 
ya kila siku na 
pia 
majukumu mengine ya familia
 itawafanya watoto wako 
wasiende nje kutafuta 
watu wengine wa mfano bali
 utakuwa wewe mzazi wao ndio mtu wao wanayetamani kuwa.
Kwani hulka ya binadamu siku zote ni kuwa shujaa.

HEBU TUANZE LEO KUWA AINA YA WATU AMBAO WENGINE WANAWEZA KUIGA
YALE TUNAYOYAFANYA.

USIKUBALI KUIACHA DUNIA HII HUKU WATU WAKISHUKURU KUONDOKA KWAKO.

Share this post:

Digg it StumbleUpon del.icio.us Google Yahoo! reddit

0 comments:

Post a Comment

 
Copyright 2013-2017 Lisha Ubongo
| Branded by www.pixelbase.co.tz