Utoaji wa mimba(Abortion),
 katika jamii yetu siku hizi limekuwa jambo la kawaida sana,
 kiasi kwamba hakuna anayezungumzia madhara tena.
Na jamii inalichukulia kuwa ni sehemu ya maisha ya kila siku.

Tafsiri potofu inayotolewa na watu huko mtaani,
 kwenda kwa wageni wa jambo hili ndio unalifanya liendelee kukithiri.
Mara nyingi,
 wanaofanikiwa kutoa kwa usalama,
madhara wanakuja kukutana nayo siku za mbele sana na hapo ndio hawaoni tatizo katika kitendo hiki.

Lakini,
 leo hapa tuzungumze na wale ambao,
 hawajawahi na wanafikiria, 
au wamewahi na kuna matatizo wanakutana nayo bila kujua chanzo ni nini,
 au wanataka kumshawishi mtu akafanye.

hebu tuangalie matatizo ambayo anaweza kukutana nayo mtu anayefanya utoaji wa mimba:

1.KUTOBOKA KWA KIBOFU CHA MKOJO

Ikiwa,
 mfuko wa uzazi utatobolewa,
 kuna uwezekano mkubwa kabisa na kibofu chako cha mkojo kutobolewa.
Na inaleta maumivu makali sana na matibabu yake ni
 mpaka oparesheni.

2.KUTOBOLEWA KWA UTUMBO MDOGO

Kama mfuko wa uzazi utatobolewa,
 basi pia kuna uwezekano
 mkubwa wa utumbo mdogo kutolewa kwa
 urahisi kabisa.
Na dalili zitakazoonekana ni pamoja na kichefu chefu, kutapika, maumivu ya tumbo, homa, damu katika haja kubwa, 
na hata kifo kama 
isipogundulika mapema.

3.KANSA YA MATITI

Kwa wanawake wanaofanya utoaji wa mimba,
 wako katika hatari kubwa 
ya kupata kansa ya matiti 
siku zijazo 
za maisha yao.

4.MIMBA IJAYO KUTUNGA NJE YA MFUKO WA UZAZI

Kwa wale ambao,
 wanakuwa washafanya utoaji wa mimba 
inakuwa ni rahisi kwa kukamata mimba zinazofuata zikiwa zimetungwa nje ya mfuko wa uzazi.
Na endapo hautagundulika mapema kwamba mimba imetunga nje ya mfuko wa uzazi, 
utapoteza maisha 
kwa kuvuja damu nyingi sana,
 kwa kuwa mimba ya nje ya mfuko wa uzazi ina kawaida ya kupasuka.

Madhara mengine ambayo yanaweza kuja kutokea ikiwa utapata mimba nyingine:

*Kuna uwezekano mkubwa kabisa ukaendelea kupata siku zako kwa muda wa miezi mitatu ya mwanzo.
*Kuna uwezekano mkubwa kabisa kuwa hautazaa kwa kutumia mfumo uliozoeleka.
*Mtoto atakaye zaliwa atakuwa katika hatari ya kupoteza maisha miezi ya mwanzoni kabisa.
*Mtoto ajaye anaweza kuwa na uzito mdogo kuliko kawaida.
*Kuna uwezekano mkubwa kabisa kuwa mtoto ajaye atazaliwa kabla ya muda wake kufika.

5.KUPUNGUKIWA DAMU

Na hili huwa ni tatizo ambalo lina uwezekano mkubwa wa kutokea,
 kwani unapoteza damu nyingi sana wakati wa zoezi hilo.

6.MIMBA KUHARIBIKA

Kwa wale ambao wamefanya utoaji wa mimba zaidi ya mara mbili,
 wako katika hatari ya mimba zao kuwa zinatoka na kuharibika 
kabla ya wakati.

7.VIPANDE VYA MWILI KUBAKIA

Kwa kuwa,
 anayekutoa huwa haoni ndani kuna nini hasa kimebaki, 
zaidi yeye anachojua ni kuingiza kifaa chake na kuanza kuvuta viungo vya kiumbe kimoja kimoja.
Kwa hiyo kuna uwezekano mkubwa kabisa akashindwa kutoa vyote.

8.UTASA

Baaada ya kufanya zoezi hili,
 unaweza usiwe na uwezo wa kupata 
mimba tena.

9.KANSA YA SHINGO YA KIZAZI
Hapa hatari huwa kubwa,
 kwasababu kuna uwezekano mkubwa wakati unafanyiwa shingo ya 
kizazi ikakwanguliwa na hivyo kusababisha kansa siku 
za baadaye.

10.MATATIZO YA SAIKOLOJIA

Mhusika wa utoaji mimba,
 huwa anaweweseka sana pale anapokuwa amefanya tukio hilo kila
 anapoenda kulala.
Japo kwa wale wazoefu hawajali lakini kwa wewe mgeni itakufanya ukose raha muda wote wa maisha yako.

NADHANI TUMEONA BAADHI YA MADHARA AMBAYO YANAWEZA KUMKUTA MUHUSIKA.

BASI TUJITAHIDI KUTUNZA UHAI WA VIUMBE HAO AMBAO HAWANA HATIA.

KWANI JANGA UNALOLIKIMBIA NI DOGO KULIKO UTAKALOLISABABISHA BAADA YA KUFANYA TUKIO HILI.


Share this post:

Digg it StumbleUpon del.icio.us Google Yahoo! reddit

0 comments:

Post a Comment

 
Copyright 2013-2017 Lisha Ubongo
| Branded by www.pixelbase.co.tz