Moja ya sababu ya kutokielewa kitu unachofundishwa au unachosoma
 mwenyewe ni 
kukosa umakini.
Ikiwa umakini wako hauko katika unachojifunza,
yaani unafundishwa au unajisomea lakini unawaza kitu kingine,
unachojifunza kitaingia katika
 kumbu kumbu fupi 
na baada ya muda
 kitaondoka zake.

Unaweza ukawa unasoma muda mrefu kuliko
 mtu yeyote 
lakini umakini 
kama haupo hautapata 
matokeo unayoyahitaji.

Yafuatayo huchangia kukosa umakini wakati wa kujifunza:

1.KUTOKUWA TAYARI KIAKILI KUJIFUNZA

*Kuwa na mawazo lukuki,
 ambayo hayaendani na kitu unachotaka kujifunza.

2.KUKOSA SHAUKU YA SOMO LENYEWE

*Kutovutiwa na namna linavyofundishwa au lina mambo mengi sana.

3.KUSOMA NYENZO NGUMU

*Kusoma somo lenye lugha ngumu kuielewa au maelezo mengi na ambayo mpangilio 
wake huuelewi.

4.KUKOSA HAMASA

*Kutojua baada ya kujifunza hilo somo litakuja kukusaidia nini katika 
maisha ya baadaye.

5.KUKOSA LENGO MAALUMU

*Kutojua katika hilo somo,
 unatakiwa ujue nini hasa 
baada ya 
kumaliza kulisoma.

6.KUSOMA ENEO LISILO NA UTULIVU

*Kukosa utulivu wakati wa kujifunza 
kwasababu ya kelele nyingi na 
usumbufu wa watu.

7.MATATIZO YA HISIA

*Kuwa na maumivu ya kihisia yanayokuzuia kufikiria vizuri.

8.KUCHOKA

*Kuhisi uchovu wa mwili unaokufanya 
utake kupumzika.

9.KUWA NA MLUNDIKANO WA KAZI

*Kuwa na mlundikano wa kazi nyingi za 
kufanya na hivyo kukupotezea 
hamu ya kujifunza.

10.KUWA NA HOFU YA KUSHINDWA
*Hofu ya kushindwa inapokuingia inashusha hamu yako ya 
kujifunza kabisa.

Sababu,
 kubwa ya kukosa umakini
 katika unachojifunza,
 sio 
kukosa kuvutiwa na unachosoma 
bali ukiwa 
na nia ya kukijua 
lazima 
umakini wako utakuwa hapo tu.

Ndio maana,
 sifa moja wapo ya mwanafunzi bora, 
ni yule 
anayesoma kitu hata kama 
kwa mara ya kwanza hakijamvutia ila anachotafuta yeye ni 
kujua taarifa mpya.
Lakini,
 unaposoma kitu ambacho wewe mwenyewe 
unasema moyoni kuwa kinakuchosha 
lazima ukione kigumu.

Kama unajiona umechoka au 
hauko sawa 
kihisia kujifunza ni heri usiingie hicho kipindi au
 usisome hilo somo kwa muda huo hadi utakapokuwa sawa.
Kwasababu,
 ni heri utumie muda mwingi
 kuweka akili yako tayari kwa kujifunza kuliko 
kupoteza muda mwingi 
kujifunza kitu ambacho hautakielewa.
Unapokuwa sawa kiakili,
 unatumia muda mfupi kuelewa unajifunza kuliko unapokuwa hauko sawa.


Haya ndio unaweza ukaanza kuyafanya 
ili kuongeza uwezo 
wako wa umakini wakati wa kujifunza:

1.Chagua eneo ambalo umelipenda kusomea 
na hakuna vitu au shughuli 
zitakazo kuchanganya;

2.Tengeneza ratiba maalumu utakayoifuata
 ili iwe inakukumbusha 
kutimiza wajibu 
wa somo husika;

3.Hakikisha una nyenzo zote muhimu 
ambazo 
zinatakiwa wakati wa 
kujifunza.
Sio ushaingia darasani halafu kalamu 
huna,
utaanza kuingia 
uvivu mapema sana;

4.Weka mawazo ya kuifanya kazi 
uliyonayo vizuri,
kama ni kazi ya darasa 
au mitihani;

5.Jikumbushie malengo yako ya kusoma
 ni nini halafu soma 
kulijibu hilo swali;

6.Jiwekee mapumziko mafupi mafupi 
wakati unajifunza sio kufululiza muda mrefu bila mapumziko;

7.Andika muhtasari wa yale unayojifunza 
na jikumbushie 
mara kwa mara;

8.Jiwekee vituo maalumu wakati wa 
kujifunza wewe mwenyewe.
Kama unasoma mada ndefu 
weka lengo kwamba utaishia sehemu fulani, halafu ukianza tena
 unandelea ulipoishia.

UJINGA SI KITU CHA KUKIFURAHIA KABISA,
KAMA KUNA KITU UNAPASWA 
UKIELEWE HALAFU HAUKIELEWI, 
NI VYEMA UKAFANYIA KAZI MAZINGIRA YAKO YA KUJIFUNZA.

NA KITU PEKEE,
 NI KUAMSHA HAMASA YAKO YA KUJIFUNZA ILI UFIKIE LENGO 
ULILOJIWEKEA.

Share this post:

Digg it StumbleUpon del.icio.us Google Yahoo! reddit

0 comments:

Post a Comment

 
Copyright 2013-2017 Lisha Ubongo
| Branded by www.pixelbase.co.tz