JE, UNATATIZO LA KUMALIZA PESA MAPEMA BILA MPANGILIO MAALUMU? SOMA HAPA UJIELIMISHE.

Njia pekee ya kutunza pesa ni
 kupunguza matumizi 
yasiyo ya lazima.
Unachohitaji ni kujua pesa unatumia 
zaidi kwenye nini,
hapo ndipo utakapojua ufanye nini ili kupunguza matumizi.

Kila mara
 weka akilini kuwa yawezekana 
unanunua kitu kwa bei rahisi
 lakini 
jiulize ufanisi wake una umuhimu wowote 
au ni kutimiza wajibu tu.

Tambua mahitaji yako 
halafu 
fanya hesabu za namna ya kutumia unachokipata kwa uangalifu.
Tambua kuwa
 ili kupunguza matumizi kufanikiwe ni lazima ubadilishe mfumo wako wa maisha na namna unavyofikiria.

Zifuatazo ni hatua unaweza kuzitumia kupunguza matumizi:

1.TAMBUA UNATUMIA PESA ZAKO KATIKA NINI ZAIDI

 Kama mpaka sasa hujui pesa 
zako unazitumia 
zaidi kwenye nini zoezi
 hili litakushinda.
Ukiwa hujui pesa yako 
unatumia kwenye nini hasa,
kila mara utakuwa mtu wa kushangaa tu 
kuwa hela yako imepungua.
Na wengine
 wanaweza kuwalaumu watu wao
 wa karibu kuwa wamewachukulia 
kumbe ni yeye mwenyewe ndiye aliyefanya matumizi.


2.EPUKA MATUMIZI YASIYO YA LAZIMA

Kuna matumizi
 mengine hata wewe unayaona kabisa
 kuwa hayana ulazima 
lakini kwa kuwa 
ushazoea ndio unaona ni 
kitu cha kawaida.
Na hivi ndio
 vitu mbavyo unanunua hapa
 baada ya dakika tano ukimaliza kukitumia ushasahau kama hata ulitumia.

3.WEKA KIPAUMBELE CHA UNUNUZI

Weka mkakati wa muda mfupi
 wa kutunza pesa unayopata kwa ajili ya kununua kitu fulani ndani ya muda uliojiwekea.
 Kama kuna kitu 
unataka kununua ijue bei yake halafu anza mkakati wa kutunza pesa kwa ajili ya kukimiliki.
Hii itakusaidia kuepuka matumizi yasiyo ya lazima.

4.PUNGUZA MATUMIZI YA SIMU

Mawasiliano 
siku hizi ndio yamekuwa yanaongoza kwa matumizi makubwa ya pesa.
Ukiwa hujui muda gani  wa kupiga,
 na muda gani wa kutuma 
meseji utakuwa 
unajimaliza mwenyewe.
Unaweza ukaweka vipaumbele vya watu wa kuwasiliana nao.
Kama unafanya simu za biashara ni kitu kizuri lakini 
kama ni stori tupu hapo
 lazima ujizuie.


5.TENGENEZA ORODHA YA VITU VYA KUNUNUA

Unapoamua
 kuwa unataka kwenda kununua 
vitu fulani ni lazima uwe na orodha maalumu itakayokuongoza ili 
usitumie zaidi ya uliyopanga.
Usijiroge ukatoka nyumbani kwenda kununua vitu huku hujui nini hasa unaenda kununua na gharama yake ni shilingi ngapi?
Utakuja kujuta wakati ushafikia nyumbani ukiwa huna pesa kabisa.

PESA INAYOTUMIKA TU BILA KUJIONGEZA NI SAWA NA KUJIFILISI MWENYEWE.

ANZA LEO KUTUNZA KIDOGO UNACHOPATA ILI KESHO USIJE KUJILAUMU 
ZITAKAPOKWISHA KABISA.

Share this post:

Digg it StumbleUpon del.icio.us Google Yahoo! reddit

0 comments:

Post a Comment

 
Copyright 2013-2017 Lisha Ubongo
| Branded by www.pixelbase.co.tz