Kila siku katika jamii yetu,
 kuna maelfu ya wanafunzi wanaogopa 
kwenda shule.
Uonevu,
 limekuwa ni tatizo kubwa,
 hasa maeneo ya mikusanyiko ya watu wengi 
kama shuleni, vyuoni, 
na hata maeneo ya kutafuta mkate wa kila siku(kazini/kibaruani).

Linaonekana kutokuwa na mwisho,
 kwani wazazi, 
walimu, na hata wakuu wa eneo husika
 bado hawajui kinachoendelea, 
au hawafahamu madhara yake na 
wanayafumbia macho
 matukio kama hayo.

Uonevu ni kitendo cha mtu 
kutendewa isivyostahili 
na mtu au kikundi cha watu 
mara kwa mara, 
kutokana na hali yake  ya kimaumbile, 
nafasi yake, 
au hali yake ya maisha.

Sababu hizi tatu,
 ndio kuu kabisa zinazoongoza kuufanya 
uonevu 
uwepo katika jamii.
Mara nyingi wanaowafanyia wenzao,
 uonevu huu
 huwaona hao wanaowafanyia kuwa 
hawaendani nao;
kwa kuwa tu wengine wana aibu, 
kipato kidogo, 
hawafanyi matukio wanayofanya wao,
 rangi tofauti, 
dini tofauti, 
au hata jinsia tofauti na wao.

Waonevu,
 wanaweza kutumia maneno 
au vitendo 
kwenda kwa wanaowaona 
wanyonge wao 
ambao hata wakiwaonea hawawezi
 kuwafanya kitu.

Kuna njia mbali mbali ambazo waonevu wanazitumia kutimiza azma zao 
kwa mnyonge wao.
Na uonevu ambao
 madhara yake yanaonekana kwa haraka 
ni wa kimwili
 kwani wengine huwapiga 
wanyonge wao na kuwaumiza,
 na wengine huwanyanyasa 
kwa kuwashika maungo.

 Uonevu wa maneno unaonekana 
kuathiri 
zaidi saikolojia ya 
anayefanyiwa na ni mgumu kuonekana na wanajamii wengine.
Hapa waonevu hutumia njia mbali mbali kuwasilisha kwa muhusika 
kwa kumteta, 
kumtumia ujumbe wa kuumiza,
 kumuandika vibaya katika kuta/ubao, 
au kumsambazia 
maneno ya uongo.

Siku za karibuni njia inayoonekana imeshika kasi 
kutumiwa na waonevu ni 
mtandao wa kijamii na 
meseji za elektroniki.

Hivi unadhani anayeonewa anajisikiaje?
Kitu kimoja kikuu,
 ni kuwa uonevu huwa haupokeleki kwa
 yeyote anayefanyiwa.
Anaweza akavumilia siku za mwanzo
 lakini 
hali inapozidi kuwa mbaya 
inawajengea hofu kali.

Anaweza kuvumilia kuitwa jina baya
 au unyanyasaji wa kijinsia 
mbele za watu siku za mwanzoni 
lakini 
ikiendelea inamuumiza sana
 na inamjengea hali ya kumuogoga
 sana mtu anayemfanyia 
kitendo hicho,
na huingia kuathiri hadi maendeleo 
yake ya shule,
 afya au kazi.

Uchunguzi unaonyesha,
 watu wanaofanyiwa uonevu 
na wenzao 
wana hatari ya kupata 
matatizo ya afya ya akili, 
kama kutojiamini, 
msongo wa mawazo, 
unyogovu, hofu, 
au wengine huishia kujiua wenyewe.

 Wanao waonea wengine
 pia wako katika hatari,
kwani 
anapoanza tabia hiyo
 tangu akiwa mdogo
 anapokua mkubwa huwa katika 
kiwango kibaya zaidi
 cha uhalifu.
Utafiti unaonyesha kuwa 
katika kila watoto 4
 waliowahi kujihusisha 
na uonevu walikuja kuwa wahalifu wakubwa katika jamii zao wanapokuwa 
na umri mkubwa.

Wengine huishia kukataliwa na wenzao
 na kupoteza marafiki wengi 
wanavyoendelea kukua,
na wanakuwa katika hatari ya 
kukosa maendeleo mazuri
 shuleni na kazini.

Waonevu wengi huwa na sifa zinazofanana:

1.Wanapenda kuwatawala wengine;

2.Wanapenda kujizungumzia wao tu;

3.Sio wazuri katika kuwasiliana na wengine;

4.Wanatawaliwa na mawazo mabaya kuhusu wengine;

5.Hawajali hisia za wengine;

Hii inatokana na wao
 kujiona bora sana 
kushinda watu wengine, 
na wanajiona wana haki ya kuwafanyia wengine 
wanavyotaka wao. 
 muda mwingine wanawafanyia wenzao hivi 
kwa kuwa 
wanajiona hawako salama.

Kwahiyo 
wanatumia njia hiyo 
kuwashusha wengine chini 
ili wao waonekane juu na 
wana nguvu zaidi.
Na wengine wanawafanyia hivyo wenzao 
kwa kuwa tu 
wao waliwahi kufanyiwa kwa hiyo 
wanalipiza kisasi.

Na wengine huwa wana matatizo ya akili na kushindwa kuwa hisia za hatia,
 huruma, 
uelewa au majuto. 
Na njia pekee ya kuwasaidia
 ni kuwapeleka kwa daktari wa saikolojia, mshauri, 
daktari wa magonjwa ya akili au
 mwana ustawi wa jamii.

Ufanye nini kama unakutwa na hili tatizo:

*Kwa watoto wadogo,
 na vijana wanaweza kulitatua kwa 
kuwaeleza watu wakubwa 
wanaowaamini.
Ni heri,
 ukatoa taarifa mapema
 kabla uonevu haujafikia kiwango 
cha kuumizwa mwili.

Na mara nyingine,
 anayefanyiwa uonevu anaweza akapata 
wazo la kulipa kisasi 
na hivyo njia atakayotumia 
siku zote huwa ni mbaya na 
inaweza ikaleta madhara makubwa 
eneo husika.

Hebu tuangalie njia mabazo unaweza kuzitumia kupambana na uonevu wa kisaikolojia na maneno:

1.WAEPUKE WAONEVU;
Ni heri,
 uonekane mjinga 
kuliko kuruhusu maneno yao 
yakufanye upoteze utu wako.
Nia yao ni kukuona wewe ukiumizwa 
na ujumbe wanaokutumia 
na ukiondoka watajiona hawajafanya kitu
 na wewe hukuwajali.
Ukiendelea hivyo watajiona wajinga na watachoka kukuchokoza.
Tena ukiweza ondoka kwa mbwe mbwe za kutabasamu na mwendo wa kishujaa kumuonyesha kwamba huumizwi
 na maneno yake.

2.SHINDA HASIRA ZAKO:
Yawezekana kabisa,
 wakawa wanakupa maneno makali
 na yakakuumiza sana,
 na kuondoka hilo eneo haiwezekani basi jitahidi usionyeshe hasira mbele yao.
 Kwani utawapa ushindi kuwa wamefanikiwa kukuumiza.
Wanachotaka ni kuzitawala hisia zako 
na kwamba 
wao ndio waamue muda huu ucheke 
au muda huu unune.

3.USIANZE KUPIGANA:
Yawezekana kabisa,
 hasira zimevuka kiwango na unaona huyo mtu unamudu kuzipiga naye 
lakini hujui aliyekuchokoza kajipanga 
vipi na yeye.
Kwani mara nyingi
 wenye tabia hizi huwa hawana cha kupoteza washajikatia tamaa na hivyo 
wanatumia muda wao kuharibu 
maisha ya wengine.

4.ONYESHA KUJIAMINI:
Muonyeshe anayekuonea,
 kuwa anachotaka ujisikie hakitawezekana 
kwani unajitambua na 
unaelewa unafanya nini 
katika maisha yako.
Hata kama anazungumzia kasoro ya kimwili onyesha wewe kuwa unajikubali
 vile ulivyo na kuwa maneno 
yake ni kazi bure.

5.JISAHAULISHE MANENO YAO:
Huwezi kuzuia watu
 kuongea maneno usiyapenda dhidi yako,
 lakini 
unaweza kuzuia yasikae 
kichwani mwako.
Kama unajijua unapenda sana kitu fulani elekeza mawazo yako 
huko muda mwingi.

6.ZUNGUMZA NA WAKUBWA:
Unaweza ukatumia muda wako
 kuzungumza suala hilo na watu kama 
washauri, walimu,
 marafiki, 
au yeyote unayedhani atakupa msaada unaohitaji.
Itakusaidia kupunguza hisia ulizonazo juu ya tukio hilo ukimuelezea.

7.USIOGOPE KUBADILISHA MARAFIKI:
Ukiona marafiki ulionao
 ni kawaida yao kukuzungumzia vibaya 
kwa umbea 
fanya uamuzi wa kuwaacha na
 kutafuta marafiki wengine ambao unaona hawana tabia kama hizo.

IKIWA WEWE UNAYESOMA MAKALA HII,
 UKO KATIKA MAZINGIRA HAYO YA UONEVU,
CHUKUA HATUA SASA KUPAMBANA NA HALI HIYO 
KABLA HAIJAKULETEA 
MADHARA SIKU ZIJAZO.

WAONE WANAOKUFANYIA UONEVU KUWA NI WAOGA NA WADHAIFU KWA HIYO WANAKUTUMIA WEWE KUJIONESHA NI MASHUJAA KUMBE SIO KWELI.

NA KWA SISI WENGINE 
TUNAOSHUHUDIA MATUKIO HAYO,
TUWE TAYARI KUWASAIDIA WALE WANAOONEWA,
 ILI NAO WAONE UTAMU WA KUWA KARIBU NA 
WATU WENGINE.

Share this post:

Digg it StumbleUpon del.icio.us Google Yahoo! reddit

0 comments:

Post a Comment

 
Copyright 2013-2017 Lisha Ubongo
| Branded by www.pixelbase.co.tz