Ulimwengu jinsi ulivyo,
 hupati picha kama 
binadamu angekuwa mmoja angeishi vipi
 peke yake.
Kwani 
ukiangalia mfumo ulivyo,
 unamfanya na kumtaka 
binadamu awategemee wenzake katika kutimiza mahitaji yake,
 kuanzia kimwili hadi kihisia.
Hali hiyo humfanya kila binadamu awe tegemezi kwa binadamu wengine,
 katika kukamilisha furaha
 yake ya kila siku.

Lakini
 kwa kuwa watu unaokutana nao 
hamfanani tabia kuna kipindi 
lazima
 kutatokea utengano na hao marafiki.
Ama 
uwe wewe umechoka na mwenendo wao au wao wachoke na mwenendo wako.

Lakini 
mpaka utengano kukamilika,
 kuna dalili huwa zinajionyesha mwanzoni ambazo
 ukizisoma utagundua mapema sana kwamba kuna kitu unatakiwa ufanye ama kuuokoa au kuumaliza kabisa na wewe.

Hebu tuangalie dalili 5 unazoweza kuziangalia katuika urafiki wako:

1.MUONEKANO WA USONI

Kama
 wana nyuso za furaha 
wanapokuona,
 hapo jua wanafurahia uwepo wako.
Lakini 
ukiona umetokea tu nyuso 
za watu zimebadilika ujue hizo ni
 dalili za 
kuwa uwepo wako 
hauna umuhimu kwao.

2.MATEMBEZINI

Kama
 wanakuita katika safari zao 
za matembezi 
ya kawaida ujue wanapenda 
uwepo wako lakini kama 
kila siku unashtukia tu wanahadithiana waliyoyafanya jana ambapo wewe hukuwepo hiyo ni dalili mbaya.

3.KUKUPIGIA SIMU AU KUKUTUMIA MESEJI

Kama 
ukiona wewe haupigiwi wala 
kutumiwa meseji 
kama 
kipindi cha nyuma huku wao 
wanawasiliana
ujue dalili sio nzuri.

4.MANENO KUTOKA KWA MARAFIKI ZAO

Hata 
marafiki zako pia 
nao wana marafiki,
 kwahiyo 
endapo hawafurahii uwepo wako
 wao ndio wa kwanza kuwasimulia habari zako wasizozipenda.

5.KUKUPINGA KILA UNACHOONGEA

Yaani
mkiwa mna jadili jambo,
 wao ndio huwa wa kwanza kukucheka unachoongea.
Wanakuonyesha wazi kuwa,
 hawakubaliani na unayoongea hata kama kuna ukweli ndani yake.

KUPOTEZA MARAFIKI KATIKA MAISHA YETU
 SI KITU KIZURI.

USIPOTAFUTA TATIZO LIKO KWAKO 
AU KWAO
 UTAJIKUTA HAUDUMU NA
 MARAFIKI KAMWE. 

KAMA UKIONA URAFIKI HAUNA FAIDA 
UMALIZE 
LAKINI 
UKIONA UNAFAIDA 
PIGANIA KUUDUMISHA KWA 
KUREKEBISHA KASORO ZILIZOPO.

Share this post:

Digg it StumbleUpon del.icio.us Google Yahoo! reddit

0 comments:

Post a Comment

 
Copyright 2013-2017 Lisha Ubongo
| Branded by www.pixelbase.co.tz