Tangu demokrasia 
imeingia bara la Africa,
wanasiasa wengi wenye kariba mbali mbali wamekuja na kuondoka.
Kuna wengine 
wanafahamika sana na wengine hawajawahi kufahamika kabisa.

Wasomi wa kufanya maamuzi
 ya nchi kwa teknolojia,  
wamekuwa wengi kiasi kwamba 
inasemekana ukirusha jiwe nchini
 Nigeria uwezekano wa kumpiga msomi 
wa chuo ni asilimia 99.

Pamoja na mahesabu yote 
magumu ambayo tumekuwa tunatumia 
kufanya maamuzi,
mimi nadhani tunachohitaji katika dunia ya sasa ni hesabu rahisi za 
MAGAZIJUTO
(Mabano Gawanya Zidisha Jumlisha Toa) 
juu ya hapo huitaji kitu kingine zaidi ya utashi na maono.

Kwa upande mwingine wakoloni 
walikuja Afrika 
na wakaingiwa na tamaa ya maliasili 
ambazo Afrika inazo.
Wakafanya nini?
  Katika ardhi yenye maliasili 
za thamani
 ni lazima walishawishika 
kuitamani sana.
Na walianza kuwa na maono na maliasili zetu huku sisi hatujui kinachoendelea.

Lakini ngoja niseme ,
Afrika inahitaji kusonga kwa kasi ya 
ajabu,
 ila tu 
kwa kukipata kiunganishi sahihi kilichokosekana.
Je, hicho kilichokosekana ni kipi?

Kitu tulichokosa mpaka sasa 
Afrika ni 
watu wenye maono.
Nchi nyingi zilizoendelea 
zilifanikiwa kwa kuwa walikuwa na 
watu wenye maono na 
sio watu wataalamu na wasomi tu.
Na hii inatokana na kuwa maono huwa yana mantiki ndani yake na pia hudumu muda mrefu.

Mwaka 1901,
ulifanyika mkutano wa wasomi na wataalamu katika jiji la London.
Na walikuja na maadhimio yafuatayo:
1.Haiwezekani kitu kilichotengenezwa kwa chuma kuruka angani;
2.Haiwezekani kwa gari kutembea maili 36 kwa saa bila kumletea madhara mtu aliye kwenye hilo gari.
Na huu ndio ufahamu waliokuwa nao kipindi hicho.

Mwaka 1904,
ndugu wa familia ya Wright walikuwa na ujauzito wa maono ndani yao,
na wakafanikiwa kurusha ndege ya 
kwanza angani.
Hakuna kingine,
 unaweza ukasema kilichangia 
ndugu hawa kung'ang'ania majaribio mengi 
mpaka kufanikiwa 
kuirusha ndege
 zaidi ya kuyaamini maono na kujiamini.
Yawezekana,
 ndugu hawa walijiambia 
kuwa katika dunia hii 
hakuna mwenye hakimiliki ya hekima ya kuamua kipi kinawezekana na kipi hakiwezekani.

Kuna maono ya aina mbili,
ya kwanza ni maono kutoka kwa Mungu na 
ya pili ni maono ya kisomi.
Maono ya Mungu 
humjia mtu pale anapokuwa amelala na
 ni ya kiroho zaidi
lakini maono ya kisomi huwa yanatolewa
 na akili ya mtu.
Maono ya Mungu,
 mara nyingi huwa ni makubwa 
na yanamfanya anayeonyeshwa 
ashindwe kuyaelewa sawa sawa,
ukubwa wake ndio 
unachangia mara nyingi yasitekelezwe na aliyeonyeshwa.

Hii inatokana na aliyeonyeshwa kushindwa kuyaamini maono hayo,
kwa kuwa kiwango cha akili 
kinakuwa kimeishia hapo na kinaendelea kumwambia haiwezekani.

Kuna vitu vingi Afrika 
tunaona haviwezekani 
lakini 
wakiwepo watu wa maono 
vyote vitawezekana,
 na si tu kuwezekana bali tutaviona kuwa rahisi.
Kwasababu tunaendelea kutumia 
kiwango cha akili ile ile ya kibinadamu 
maono mengi tunayaacha yakipita tu bila kufanyiwa kazi,
ambapo yangeweza kuibadilisha sura ya 
Afrika kwa ujumla.

Tunapoendelea 
kutumia maono ya kisomi,
mara nyingi huwa ni ya vitabuni na 
ambayo yana uwezo sana wa kumbadilisha mtu mmoja na si dunia uliyopo.

Siri moja iliyojificha
 ambayo wengi tunashindwa kuigundua, 
ni kuwa 
vitu vya kiroho ndio halisi na vile vya kimwili vimetokana na matokeo 
ya vitu vya kiroho.
Kwa mfano,
 mtu anapokufa kitu tunachoendelea kukiona mpaka muda wa kuzika
 ni maiti ambayo haina roho,
kwahiyo kukosekana kwa roho ni kukosekana
 kwa maisha.
Kwa hiyo maono ya kiroho ndio yenye 
uwezo wa kuibadilisha dunia.

Kuna sababu nyingi,
 sana zinazofanya maono mengi 
yasifanyiwe kazi.
Lakini
 mimi nitazungumzia sababu moja 
ambayo ndio hutoa 
kiashiria cha ukubwa wa maono yako 
na si kingine ni 'upinzani'.
Mtu mwenye maono makubwa,
 ndiye mwenye upinzani 
mkubwa sana.
Unapokuwa na maono usikae nayo kimya,
 bali yaweke wazi
 kwa watu wengine.
Wengi wetu tunataka tunapoeleza maono
 kwa watu wengi tusifiwe tu,
nakuambia ukweli
 kama maono utakayotoa 
hayapati upinzani jua kabisa hayo 
sio maono bali ni hadithi 
tu ya kuvutia.

Unapokutana na upinzani mkubwa,
 ndio hukupa picha kuwa ulichobeba 
sio kitu cha kawaida.
Ikitokea msimu wa kiangazi mvua kubwa ikanyesha kwa mtu mwema,
watu wabaya watazungumzia
 sana ukubwa wa hiyo mvua/au 
muda uliyotumia kunyesha.

Lakini kuna mvua ambayo,
 wewe peke yako ndio unaijua ukubwa wake,
na unapaswa uwe ndio mwenye 
maelezo yake.

Kwa wafanyabiashara 
wenzangu jambo hili la maono yawezekana liko mbali na upeo wetu wa kufikiri.
Kwani dhumuni kuu la biashara ni kutengeneza faida ambayo huwa na mwisho wake.
lakini,
 unapokuwa na maono na kuyafanyia kazi utaingiza faida isiyokwisha kwasababu utakachoacha ni urithi kwa vizazi vilivyopo 
na vijavyo.
Urithi huishi milele. 

Kwahiyo,
 jinsi unavyoyaamini maono yako ndio itakayoamua 
yatakavyofanikiwa.
Kujiamini ndio kutafanya maono 
yaweze kutelezeka na 
kuwa vitu halisi.
Nina maono yangu yanaitwa 'Maono ya Afrika',
hakuna kitakachonizuia 
kuyafanikisha.

Maono yako hayawezi kufanana na ya mtu mwingine yeyote 
ni wewe peke yako mwenye uwezo 
wa kuwa nayo.
Bwana Alexander Bell alifanikiwa  
kutimiza maono yake ya kutengeneza simu ya kwanza,
zaidi ya hapo wanaofuatia wanabaki kuiboresha tu aliyoianzisha yeye.
Huu ndio tunaita urithi wa milele.


YAWEZEKANA KABISA TUKAWA BADO TUNAKOSA KUJIAMINI KATIKA KUYAFANYA MAONO TULIYONAYO YAWE KWELI.

HATA KAMA UNAYAONA NI MAKUBWA SANA KWAKO NA UNAONA ITAKUCHUKUA MUDA MREFU KUYATIMIZA USIACHE.

TEMBO ANABEBA MIMBA KWA MUDA WA MIEZI 24 NA KIUMBE ANACHOKUJA KUKITOA HUWA NI KIKUBWA.

NIMETUMIWA MAKALA HII NA:
Patrick Marimo
Motivational Speaker & Dreamer of The African Dream
 pmarimo@gmail.com +255 785159444

Share this post:

Digg it StumbleUpon del.icio.us Google Yahoo! reddit

1 comments:

Unknown

Speak of which, that is the wise we are missing now_days in our Africa. Binafsi nmejifunza kitu cha muhimu kupitia article hii. Nikushauri uzi_post kwenye mitandao mikubwa ya kijamii like facebook.

Sisi vijana wa sikuhizi tumekosa elimu ya kujitambua na hekima kwahiyo tunahitaji sana maarifa kama haya. Elimu ya darasani haitutoshi kabisa pamoja na wazazi kutukaririsha kuwa elimu hiyo pekee ndo ufunguo wa maisha. Tukijitambua na kutambua majukumu yetu na kuacha uvivu basi bila_shaka tutaibadili AFRICA YETU.
Jina langu ni Shalom Mgalawe, asante.

Post a Comment

 
Copyright 2013-2017 Lisha Ubongo
| Branded by www.pixelbase.co.tz