"Kuvaa na kupendeza, ni kipaji jamani!!"
Linapokuja,
 suala la uvae nini ili upendeze 
mara nyingi 
linaumiza kichwa.

Na unapoangalia uvaaji wa kila mtu na anaonekanaje,
 ndio unagundua kuvaa ni kipaji.

Kuna watu wao kila nguo wanayonunua inawapendeza.
Kwa wengine wakina sisi inakuwa ni kitendawili,
 cha tuvae nini ili tupendeze.

Na kuna makosa makubwa ambayo tunayafanya wakati tunapoenda kuchagua nguo za kuvaa ni haya hapa:

1.KUNUNUA NGUO ISIYOTOSHA

Hapa unakuta unanunua nguo kubwa 
au ndogo sana 
kuliko mwili wako.
Nguo inapokuwa kubwa inakufanya uonekane imekuvaa,
na 
inapokuwa ndogo sana 
itaonekana imekuchora mwili wako na 
kupendeza katika hali hiyo ni 
nadra sana.
Ukiona unashindwa kabisa katika kuchagua, jenga urafiki na 
fundi nguo tu.

2.KUVAA SHATI MIKONO MIFUPI NA TAI

Labda,
 kama uwe unafanya kazi mgahawani,
kwahiyo 
unaogopa mikono ya shati kuchafuka na vyakula vinavyomwagika mezani,
 ndio uvae hivyo.
Ukiwa umevaa hivi katika mazingira mengine,
hakuna 
atakayekuona umependeza.

3.KUVAA VIATU VICHAFU

Inawezekana kabisa,
 ukavaa nguo zikakupendeza sana,
 lakini 
ukiharibu katika viatu utaonekana haujapendeza kabisa.

4.KUVAA MKANDA WA RANGI TOFAUTI

Ukikosea kuvaa mkanda,
 ambao rangi yake haiendani na rangi ya nguo au viatu ulivyovaa
 utachosha machoni pa watu.

5.KUFUNGA TAI NDEFU AU FUPI SANA

Ikiwa utavaa tai ambayo ni ndefu sana,
 au fupi sana 
utaharibu ladha ya muonekano wako.
We utakuta mtu amevaa tai kubwa 
inapita hadi mkanda wa suruali au fupi sana inaishia kifuani tu,
kupendeza utaota milele.

6.KUVAA SOKSI NA VIATU VYA WAZI

Hapa bwana,
 hata kama umevaa vipi huko juu
 lakini 
utaonekana kituko tu 
katika hili.

7.KUVAA NGUO ZA RANGI ZINAZOPINGANA

Ni vizuri,
 ukawa makini wakati wa
 kuchagua nguo ya rangi gani 
inaendana na rangi gani 
sio ilimradi umevaa tu.
Na kuna muda mwengine hata ujaribu kujua rangi yako ya mwili pia 
kama inaendana na rangi ya 
nguo utakayovaa.

8.KUVAA NGUO ZILIZOJIKUNJA

Ni vyema,
 ukazinyoosha nguo zako 
kuliko 
kuzivaa bila kuzinyoosha ni kujishusha muonekano wako.
Ni heri kama unajua hupendi kunyoosha basi usizitupe nguo hovyo,
tafuta kitu cha kutundikia ili isijikunje kama unajua utairudia.

9.KUVAA NGUO ZENYE RANGI NYINGI NYINGI

Wewe utakuta mtu unavaa nguo ina rangi nane tofauti tofauti 
halafu eti unategemea kupendeza.
Lazima ujaribu 
kuchagua nguo zenye 
mchanganyiko mdogo wa rangi na 
sio rangi nyingi nyingi.

10.KUVAA WIGI LA RANGI AU MTINDO USIOENDANA NA WEWE

Si kila wigi la nywele linafaa kuvaliwa na kila mtu,
kuna mawigi mengine rangi yake haiendani na wewe.
Hata kama ndio liko katika fasheni lakini usiharibu muonekano wako 
kwa kuingia kichwa kichwa matika mtindo 
usiokupendeza.

KILA MMOJA WETU ANAPENDA AONEKANE AMEPENDEZA,
HILO HALIPINGIKI.

NA INAWEZEKANA KABISA MAKOSA HAYA YA UVAAJI TUNAYAFANYA.

BASI TUJARIBU KUWA MAKINI TUNAPOCHAGUA NGUO ZA KUVAA.

ITAENDELEA....



Share this post:

Digg it StumbleUpon del.icio.us Google Yahoo! reddit

0 comments:

Post a Comment

 
Copyright 2013-2017 Lisha Ubongo
| Branded by www.pixelbase.co.tz