Si kila
 anayefanya shughuli fulani
 huwa na 
utaalamu nayo,
wengine wanaifanya kwa kuwa tu nafasi ilitokea  ya kuifanya.
Na hautachukua muda
 kumgundua mtu anayefanya kazi zake kwa utaalamu,
 na yule anayebangaiza njaa tu,
kwa jinsi wanavyoenenda na tabia zao.

Mara nyingi
 waajiri na wateja 
hulalamika kuwa anayewafanyia kazi 
 hana utaalamu.
Yawezekana humalizi kazi vizuri, umemcheleweshea au hata kumzungusha kwa muda mrefu bila taarifa sahihi.

Si mara moja tunasikia 
ni jinsi gani tunatakiwa kuwa wataalamu katika 
shughuli tunazofanya.

Kama unataka kupata mafanikio,
 kuchukuliwa kama mtu makini, 
kuonekana una mchango kwa unaofanya nao shuguli zako,
 kuzifanya kitaalamu ndio njia pekee ya kukufikisha huko.

Lakini tujiulize waajiri/wateja wanatafsiri gani juu ya utaalamu?
Wengi wao watakuona mtaalamu ikiwa wewe:

*Unafika eneo la kazi katika muda unaotakiwa;

*Unaifanya kazi uliyopewa vizuri;

*Unamaliza kazi kwa wakati.

Unadhani kuna matukio mengine ambayo unahisi ukiyafanya yatakuonyesha wewe si mtaalamu?

Kuna matukio ukiwa unayafanya yanakutafsiri moja kwa moja kuwa wewe si mtaalamu wa shaghuli unayofanya.
kwa mfano ukiwa:

*Unachelewesha kazi za watu;

*Unahudhuria vikao ukiwa haujajiandaa;

*Unatumia muda mwingi kuongea umbea muda wa kazi;

*Wavunjia heshima wenzako;

*Wasubirisha wateja muda mrefu bila sababu za msingi;

*Unaiba mawazo ya watu wengine kufanyia shughuli zako bila kuwahusisha;

*Vunja ahadi zako mara kwa mara.

Hebu leo tuangalie njia kumi utakazoweza kutumia kuwa mtaalamu katika shughuli yoyote unayofanya:

Jitahidi kufanya shughuli zako kitaalamu na watu waweze kukuamini, 
kukuheshimu, 
na kukuona una uwezo wa kipekee.
Japo
 mazingira ya kila kazi 
yanatofautiana lakini 
linapokuja suala la utaalamu huwa
 na tafsiri moja dunia nzima.

Hebu tuangalie sifa za kuwa mtaalamu ni zipi:

1.UMAHIRI:

Lazima
 uwe mahiri katika kile unachofanya,
ukitumia ujuzi na maarifa 
ya kutosha katika kazi yako 
lazima utaonekana mtaalamu na watu.

2.ZINGATIA MUDA:

Watu watakuwa wanakutegemea wewe 
ufike katika muda unaotakiwa 
ili shughuli ziende na 
umalize kwa wakati.
Sio kuendelea kufanya shughuli zako kwa mazoea tu bila kujali muda,
kwani hakuna anayependa kumuamini na kumpa kazi mtu asiyemaliza kwa wakati.

3.UAMINIFU:

Unatakiwa kuwa 
muwazi wa shughuli zako,
 na wale unaofanya/unaowafanyia kazi nao wajue nini kinachoendelea.
Ukianza kujifanya mjanja mjanja, 
katika shughuli unayofanya 
huku 
huwaweki wazi watu wengine 
hakuna atakayekuona mtaalamu hata kidogo.

4.UADILIFU:

Utaonekana mtaalamu 
ikiwa utakuwa unasimamia kanuni za 
shughuli yako.
Hakuna anayependa kumpa kazi mtu asiyejua kufuata kanuni za kazi yake.

5.HESHIMA:

Kama huna heshima kwa watu wengine 
unaofanya nao 
au unaowafanyia shughuli
 basi hautaonekana 
mtaalamu hata kidogo.

6.ONGEZA UJUZI:
Tafuta ujuzi wa ziada,
usiendelee kung'ang'ania ujuzi ule ule 
kila siku. 
        Toka nje ya yale unayoyafahamu
           ili kupata mengine mapya 
     kuongezea katika yale unayayafahamu 
            ili kuboresha zaidi utendaji.


7.MTAZAMO CHANYA:

Kama wewe
 kila siku unaangalia makosa tu bila 
kuwa na mtazamo chanya juu ya shughuli unayofanya
 kuwa mtaalamu itakuwa ndoto kwako.

8.TOA MSAADA:

Wasaidie wenzako unaofanya nao shughuli
 sio kwa kuwa wewe unafahamu kitu 
fulani basi hutaki 
wenzako wafahamu.
Waonyeshe jinsi ya kufanya kazi vizuri pale unapoweza 
na wasikilize pale wanapokuuliza
 maswali.

9.TENGANISHA MATUKIO:

Usihusishe matukio ya nyumbani au
 mtaani na kazi,
ukiwa katika shughuli zako weka mawazo
 yako yote hapo.
Utakuwa mtu wa ajabu
 kufika eneo la kazi na kuanza kushughulikia masuala ya nyumbani 
huku ukiacha kazi haziendi.

10.KUWA MSIKIVU:

Kila mtu
 ana hitaji la kusikilizwa pale 
anapokuwa na 
jambo la kusema,
Kwa hiyo wape watu nafasi ya kukuelezea 
yale wanayodhani yatasaidia 
katika utendaji wa kazi.

KILA MMOJA WETU ANAPENDA KUPATA MAFANIKIO KATIKA SHUGUHULI ILE ANAYOFANYA,
BASI TUANZE SASA 
KUFANYA KAZI KITAALAMU ILI TUWEZE KUFIKIA YALE TUNAYOYATAKA.

Share this post:

Digg it StumbleUpon del.icio.us Google Yahoo! reddit

0 comments:

Post a Comment

 
Copyright 2013-2017 Lisha Ubongo
| Branded by www.pixelbase.co.tz