Katika maisha kuna mambo mengi sana ambayo unayatamani,
na kila siku unaomba 
yawe mikononi mwako.
Tangu ulipoanza kuyatamani ulikuwa na mipango, 
mawazo na mikakati mingi 
sana kichwani,
lakini mpaka leo haujafanikiwa 
kuwa nacho.
Na yawezekana unajiuliza kila siku na jibu mpaka leo haujapata. 

Sasa hebu leo chukua hizi hatua nane halafu anza kuzifanyia kazi:

1.ANZA KUKAA NA WATU SAHIHI

Hawa ni watu ambao wewe unapokuwa nao unafurahia, 
wanaokupenda, kukuthamini, na 
wanaokutia moyo wa kutokata tamaa katika mambo yako.
Hawa ni wale watu ambao ukikaa nao wanakufanya ujihisi uko hai, 
ambao wanaokukumbatia wewe wa sasa hivi na wanaotamani kumkumbatia yule unayetamani kuwa, 
bila masharti yoyote.

2.ANZA KUWA MUAMINIFU KWA NAFSI YAKO

Kuwa muaminifu kwa jambo lipi ni sahihi kwako,
 na lipi linahitaji
 kubadilishwa.
Kuwa muaminifu kwa lipi unataka
 kufanikisha na nani 
unataka kuwa.
Ukianza kujidanganya nafsi yako mwenyewe utakuwa unakosa fursa 
za kujitambua 
kama unachotamani ni sahihi kwako.


3.ANZA KUTENGENEZA VIPAUMBELE VYA FURAHA YAKO

Mahitaji yako yana umuhimu sana. 
Kama usipoanza kuweka vipaumbele vya vitu gani hasa vinakupa furaha,
hautaweza kujitambua 
wewe ni nani.
Kama utaweza kutambua wewe 
unafurahia nini itakuwa 
rahisi kuwafurahisha na watu
 wako wa karibu.

4.ANZA KUWEKA WAZI WAZO NA NDOTO ZAKO

Katika maisha,
 kama unasubiri fursa zikufuate utangoja milele, 
lakini kama ukiziuata fursa huko ziliko zitakupokea kwa 
mikono miwili.
Haina maana kukaa chini na kujisifu kuwa una mawazo na ndoto nzuri,
 kama haujaanza kuzitoa zionekane.

5.ANZA KUJIVUNIA ULIVYO

Kama haujaanza kujivunia vile ulivyo leo, itakuwa
 ngumu kupiga hatua zako mwenyewe kuelekea mafanikio.
Ukianza kujivunia vile ulivyo
 utafanya uyaone mawazo yako yana thamani, nguvu na uzuri ambao hakuna 
mwengine yeyote anao.

6.ANZA KUJIFUNZA KUTOKANA NA MAKOSA

Kama uliwahi kukosea na ukapata funzo fulani anza kulithamini hilo funzo
 kwa kuchukua mafundisho yake na 
kuyafanyia kazi.
Na ukiweza kufanya hilo,
 utaona kumbe kukosea ni hatua moja wapo katika kupata mafanikio.
Kwani kuna uwezekano mkubwa kabisa kama usipotaka kujifunza 
kutokana na hilo basi 
utakuwa unalikwepa daraja ambalo lingekuunganisha na mafanikio.

7.ANZA KUWA MKARIMU KWA NAFSI YAKO

Kama utaendelea kutumia muda mrefu katika kuilaumu nafsi yako,
 na kutaka kujiadhibu utakuwa unaendelea kujirudisha nyuma.
Ukiwa mkarimu kwa nafsi yako utaona nafasi ya wewe kunyanyuka kila 
unapokuwa umedondoka
 bila kujikatisha tamaa.

8.ANZA KUSHUGHULIKIA MATATIZO YAKO

Matatizo yanayokukabili hayatoi tafsiri
 ya wewe ni nani, 
bali jinsi unavyoyakabili 
na kuyamaliza ndiyo 
tafsiri yako ilipo.
Matatizo hayawezi kuondoka mpaka wewe mwenyewe uyakabili.
Fanya jitihada zako zote pale unapoweza halafu jipongeze kwa 
hatua uliyopiga.
TUANZE LEO KUCHUKUA HATUA HIZI NA YALE YOTE TUNAYOOTA YAWE YETU YATAKUWA 
KWETU BILA UTATA.


Share this post:

Digg it StumbleUpon del.icio.us Google Yahoo! reddit

0 comments:

Post a Comment

 
Copyright 2013-2017 Lisha Ubongo
| Branded by www.pixelbase.co.tz