Ukiwa mzazi, au mlezi
 lazima 
kuna kipindi unapata hofu
 na mtoto wako.
 Ambaye unaona anaelekea katika rika la
 ujana na kepuvuka.

Unafikiria mambo mengi ambayo wewe unayafahamu kama changamoto katika maisha ya ujana ambayo  uliyapitia,
na unaona kabisa na yeye sasa anaenda kukumbana nayo.
Hofu yako kubwa ni,
 hujui atatumia njia gani kukwepa mitego ya jamii
 na kama ataingia kwenye mtego na 
kunaswa atatokaje?

Kwani kiuhalisia kijana wako,
 anapoanza kuchangamana na vijana wengine wenye historia 
mbali mbali huwa katika uwezekano 
wa kuchota tabia zao 
kwa kuwa anatumia muda mwingi 
kuwa nao kuliko wewe.

Ushahidi unaonyesha
 kuwa vijana wengi ambao walikuwa wanapewa usia wa mambo ya maisha 
na wazazi wao,
walifanikiwa kukwepa mitego hiyo kwa kukumbuka maneno ya mzazi, na 
hofu kutotaka kwenda kinyume 
na maelekezo yao.

Kuna kipindi,
 wewe mzazi, mlezi, 
Kaka au dada unaona 
kabisa kijana wako anaonyesha mabadiliko 
ya tabia,
lakini unajisikia aibu kukaa naye chini na kumpa ukweli wa mambo ulivyo.

Kwani waswahili wanasema;
"Samaki mkunje angali mbichi"
Ukishamkosea katika rika hili,
basi uombe,
 awe na uzoefu binafsi wa kutambua  vita iliyo mbele yake ni ya namna gani na vipi ataishinda.

Hapa tuangalie mambo 7 ambayo mzazi unapaswa uanze kuzungumza na kijana wako:

1.NGONO NA JINSIA

Kijana wako,
 ambaye anakua atakutana 
na taarifa nyingi sana
 kuhusu ngono na jinsia.
 Ambazo nyingi sana huko mtaani huwa 
si sahihi.
Iwe kupitia vyombo vya habari au uzoefu atakaokutana nao
 yeye mwenyewe.
Anza kuzungumza naye kuhusu masuala ya uzazi, mimba za utotoni, na utoaji wa mimba
huku ukijikita katika madhara na namna ya kujikinga navyo.

2.DAWA ZA KULEVYA,NA POMBE

Vijana wanapenda sana kuhudhuria 
burudani kipindi
wakiwa mtaani,
 shule au hata vyuoni miaka ya mwanzoni.
Huko
 wanakuwa katika hatari ya 
kutumia vilevi
 kwa kuwa wanakutana na vijana wenzao wenye historia tofauti tofauti.
Kama usipomnyoosha mapema wewe mwenyewe vijana wenzake
 watamnyoosha katika njia zao.
Kwani wengi wao 
wanaingia katika mkumbo kwa kuwa,
 hawakupata taarifa sahihi kutoka kwa wenzao juu ya madhara ya tabia hizo,
na pia kukwepa kuonekana mshamba.

3.MATUMIZI YA PESA

Kipindi cha ukuaji mahitaji na
 matumizi ya kijana yanaongezeka kwa 
kasi kubwa sana,
hata kutunza kidogo anachopata kwake 
huwa ni tatizo.
Kaa na kijana wako umuonyeshe namna ya kutunza kidogo anachopata.
Mueleze faida za kutunza pesa zilivyo na zitamsaidiaje katika maisha yake ya kujitegemea.

4.UMUHIMU WA FAMILIA

Mara nyingi,
 vijana wanapopata nafasi ya kufanya 
shughuli zao wenyewe,
kukaa karibu na familia huwa ni
 kitu kigumu.
Hata muda anaotumia kukaa na wanafamilia wenzake huwa ni mdogo kuliko anaotumia kukaa na marafiki.
Tumia busara zako kumuungabnisha na wanafamilia wengine ili washirikiane kwa pamoja.

5.MAHUSIANO NA MITOKO

Vijana hawaoni tabu 
kubadilisha marafiki hata kwa mwezi mara nne na bado akajiona yuko juu kwa 
kuwa anawabadilisha anavyotaka.
Usiruhusu kijana wako akue na misingi isiyostahili,
 kwani itakuja kumuumiza siku zijazo.
 Nawe hautajivunia utakayokuwa unayasikia na kuona kumhusu yeye.
Kaa naye kabla hajaingia huko,
na ujaribu kumuongoza 
njia sahihi.

6.MATUMIZI YA MITANDAO

Katika zama hizi ambazo teknolojia ya mtandao wa intaneti imeenea kila mahali.
Vijana siku hizi 
kama wamewekewa gundi hapo,
kinachopaswa ni wewe mzazi kumfundisha
 mambo yapi yana umuhimu na yapi hayana umuhimu kwake katika 
mtandao wa intaneti mapema sio mpaka ulimwengu wa nje uje umfundishe akiwa ameshaumia.

7.TAFSIRI YA KUFANIKIWA

Vijana wengi,
 tuna tafsiri tofauti tofauti 
juu ya maana halisi ya kufanikiwa 
katika maisha.
Hapa ndipo tunapoanzia kupoteza dira kwasababu 
tunayoyahangaikia kwa kudhani 
ndio yatakuwa mafanikio 
yanakuja kuwa sio.
Iwe katika michezo, elimu, au jambo lolote ambalo litakuwa 
linahusisha nguvu na akili zake lazima umpe tafsiri sahihi ya kufanikiwa 
ni kuwa na nini.

Yafuatayo unaweza ukaanza kuyafanya leo:

*Mpe usalama;

*Muonyesha upendo na kumjali;

*Weka misingi yako ambayo yeye ataifuata kipindi yupo chini yako;

*Muadhibu pale inapobidi;

*Kuwa na muda wa kutosha kukaa naye na kuzungumza naye;

*Fuatilia uhusiano wake na wengine;

*Muonyeshe mfano.

KILA MZAZI ANAPENDA KUONA MTOTO WAKE AKIWA ANAJIHUSISHA NA
 MAMBO YA MSINGI KATIKA MAISHA YAKE.

UKIANZA KUMTEGENEZEA MAZINGIRA HAYO TANGU MAPEMA UTAWEZA KUJIVUNIA 
TABIA YAKE YA KESHO.

ISIJE BAADAYE KIJANA WAKO AKAKULAUMU KWAMBA HUKUMUELEZA NA KWAMBA 
UMECHANGIA KUHARIBU 
MAISHA YAKE KWA KUKAA KIMYA. 

Share this post:

Digg it StumbleUpon del.icio.us Google Yahoo! reddit

0 comments:

Post a Comment

 
Copyright 2013-2017 Lisha Ubongo
| Branded by www.pixelbase.co.tz