Siku hizi,
 suala la mtu kupokwa akaunti yake ya facebook,
 na ikawa inatumiwa 
na mtu mwengine 
ni jambo limekithiri sana.
Anayepoka akaunti na 
kubadilisha alama za siri 
na email yako anakufanya usiweze kuitumia tena akaunti yako.

Na mbaya zaidi
 anaweza kuanza kuitumia kukuharibia 
uhusiano wako 
na watu wengine.
Anaweza akawa
 anaweka lugha za matusi juu ya 
ukurasa au
 hata kuwatukana watu 
unaofahamiana nao.

Watu hawa 
 hutumia njia mbali mbali katika kupata nafasi ya kukupoka
 akaunti yako:
1.Kuzifahamu alama zako za siri;
2.Kuifahamu email yako;
3.Kufahamu majibu ya maswali yako ya siri.

Na unapojaribu kuingia hili ndio unakutana nalo.
Ukishapokwa ukitaka kuingia 
utaambiwa umekosea email
 au alama za siri.

Kama ushapokwa tayari leo nitakuonyesha 
jinsi ya kuirudisha akaunti yako:

Itakuletea ukurasa 
ambao wewe kwa juu kuna nafasi ya wewe kuingiza hitaji lako.
Andika neno: "My Account Compromised"
au "My Account hacked"


2.HATUA YA PILI:
Katika ukurasa ufuatao bonyeza sehemu iliyoandikwa 
"I can't identify my account"


3.HATUA YA TATU:
Jaza majibu katika maswali yaliyoweka katika ukurasa ufuatao.

Jinsi ya kujibu maswali ya hapo juu:

*Ingiza Email address uliyotumia kufungulia akaunti yako sehemu zote mbili.

*Katika kipengele cha tatu
 Kubali kuwa unaifikia hiyo
 email address kwa kuchagua 
"Yes" 
itasaidia facebook wakupe 
nafasi ya kubadilisha alama za
 siri za email yako.

*Ingiza jina lako lote unalotumia 
uliokuwa unatumia katika 
akaunti yako.

*Ingiza tarehe yako ya kuzaliwa, 
njia mbadala ya kuitambulisha 
akaunti yako, 
na namba yako ya simu,
kwa ajili ya sababu za kiusalama.

*Ingia akaunti nyingine halafu 
ingiza jina lako 
la akaunti uliyopokwa halafu 
kopi ile anwani ya pale juu.
Njoo uipesti hapa 'Facebook profile URL'

*Kama uliwahi kuipa jina picha yako iliyo juu andika hilo jina hapo.

*Kipengele hiki cha mwisho elezea jinsi akaunti yako ilivyopokwa,
jitahidi kuorodhesha njia mbali mbali
 ambazo unahisi alaiyekupoka
 alitumia kuingia katika akaunti yako.

*Mwisho 'Submit' na facebook watakutumia meseji katika email yako.

HATUA ITAWAFANYA FACEBOOK WAKURUDISHIE UTAWALA WA AKAUNTI YAKO IKIWA NA KILA KITU ULICHOKUWA NACHO MWANZO.

JITAHIDI MTU MWENGINE ASIJUE TAARIFA ZAKO ZA SIRI KATIKA AKAUNTI YAKO.

 Eid Mubarak!

Share this post:

Digg it StumbleUpon del.icio.us Google Yahoo! reddit

0 comments:

Post a Comment

 
Copyright 2013-2017 Lisha Ubongo
| Branded by www.pixelbase.co.tz