Acha ukweli usemwe, furaha ya kweli si kutokuwa na matatizo, lakini ni uwezo wa kukabiliana nayo kwa ujasiri. Mara zote angalia kile ulicho nacho mkononi, badala ya kufikiria ulichopoteza. Sababu haijalishi dunia imechukua nini kutoka kwako, bali utafanya nini na kile ulichobaki nacho mkononi.



Yafuatayo ni mambo sita unayopaswa kujikumbusha kila unapopatwa na jambo gumu linalotaka kukukatisha tamaa ili usisonge mbele.  
    
      1.       MAUMIVU NI SEHEMU KATIKA UKUAJI



Kuna kipindi maisha yanafunga mlango sababu ni muda muafaka kusonga mbele. Na hiki ni kipindi kizuri sababu mara nyingi hatuwezi kusonga mbele wenyewe mpaka matukio Fulani yatokee kutusukuma ndo tunasonga.
Mambo yanapokuwa magumu jikumbushe kuwa hakuna maumivu yanayokuja bila dhumuni maalumu. Songa mbele baada ya maumivu lakini usisahau ulichojifunza kipindi cha maumivu.

Eti kwasababu una pata mahangaiko ndo imaanishe kuwa unafeli maisha. Kila jambo lolote kubwa la mafanikio huwa haliji kirahisi mpaka liambatane na mahangaiko ya hapa na pale. Mambo mazuri huchukua kipindi kirefu kukamilika. Kuwa mvumilivu na kuwa na mtazamo chanya. Kila kitu kitaenda kuwa sawa, labda sio kwa kasi unayoitaka wewe lakini mambo yatakuwa sawa tu.

Kumbuka kuna maumivu ya aina mbili, kuna yale yanayokuumuiza na yale yanayokubadilisha. Ukiwa unaenda na mtiririko wa jinsi maisha yanavyokwenda, badala ya kupingana na mabadiliko, itakusaidia kukua.

      2.       KILA KITU KIPO KWA MUDA TU



Kila wakati mvua inaponyesha, huwa kuna muda itaacha. Kila wakati wewe unapopata madhara, kuna wakati wa wewe kupona. Baada ya giza daima kuna mwanga - wewe hili unakumbushwa kila asubuhi, lakini bado mara nyingi unasahau, na badala yake unachagua kuamini kwamba usiku utadumu milele. Haitakuwa hivyo. Hakuna kinacho dumu milele.

Hivyo kama mambo ni nzuri sasa hivi, furahia. Sababu haitadumu milele. Kama mambo ni mabaya, msiwe na wasiwasi kwa sababu haitakuwa milele. Kwa sababu tu maisha si rahisi wakati huu, haina maana huwezi kucheka. Kwa sababu tu kitu  kinakusumbua wewe, haina maana huwezi tabasamu. Kila wakati unakupa mwanzo mpya na mwisho mpya. Unapata nafasi ya pili, kila wakati . Wewe unapaswa kuchukua nafasi na kuufanya kuwa ni wakati bora zaidi.

     3.       KUWA NA HOFU NA KULALAMIKA HAKUBADILISHI KITU


Wale ambao wanalalamika zaidi, kukamilisha mambo inakuwa ni ngumu. Ni vyema kujaribu kufanya jambo kubwa na kushindwa kuliko usijaribu kufanya chochote na utarajie kufanikiwa. Sio mwisho kama umefanya jambo na ukashindwa; na sio mwisho pia kama haujafanya jambo lolote lakini ukaishia kulalamika kuhusu hilo jambo.

Kama unaamini katika kitu, usiache kuendelea kujaribu. Usikubali vivuli vya zamani vikazima hatua zako za maisha yako ya baadaye. Ukiwa unaitumia leo kulalamika kuhusu jana hautaifanya kesho kuwa nzuri. 

Badala yake chukua hatua. Hebu tumia ulichoweza kujifunza kuboresha jinsi ya kuishi. Endelea kufanya mabadiliko na kamwe usiangalie nyuma.

Furaha ya kweli utaipata pale tu utakapoacha kulalamika kuhusu matatizo yanayokukuta bali unatakiwa uanze kushukuru kwa matatizo ambayo hauna.

      4.       MAKOVU YAKO NDIO NGUVU YAKO


Usije kuona aibu hata siku moja kutokana na makovu ambayo maisha  yamekupa. Kovu ina maana uliwahi kuumizwa na tatizo limekwisha na jeraha limefunga. Ina maana wewe alishinda maumivu, umejifunza somo, umekuwa na nguvu, na umesonga mbele. Kovu ni alama ya ushindi ya kujivunia. 

Usije kuruhusu makovu yako yakushikilie mateka. Usije kuyaruhusu yakufanye uishi maisha yako katika hofu. Huwezi kufanya makovu katika maisha yako kutoweka, lakini unaweza kubadilisha mtazamo wa jinsi unavyoyaangalia. Unaweza kuanza kuona makovu yako kama ishara ya nguvu na si maumivu.

      5.       KILA KIKWAZO KIMOJA NI HATUA YA KUKUA


Katika maisha, uvumilivu si kuhusu kusubiri tu; ni uwezo wa kushikilia tabia nzuri wakati wa kufanyia kazi kwa bidii ndoto yako, ukijua kwamba kazi unayofanya ni ya thamani. Hivyo kama unakwenda kujaribu, jitahidi kuweka muda wako wote huko.

Vinginevyo, hakuna faida kuanzisha jambo. Hii inaweza kuwa na maana ya kupoteza utulivu na faraja kwa wakati, na labda hata akili yako juu ya tukio. Na inaweza kumaanisha kukosa kula, au kukosa kulala, kama ulivyozoea, kwa siku kadhaa.

Na inaweza kuwa na maana kutoka eneo lako la faraja na ukaruruhusu kuumizwa na baridi kwa ajili ya jambo unalojaribu. Inaweza kumaanisha kutoa sadaka mahusiano na yote yale ambayo ni yako. Inaweza kuwa na maana ya kukubali kejeli kutoka kwa wenzako.

Kila kitu kingine ni mtihani wa dhamira yako ni kiasi gani cha wewe kweli unataka kutimiza jambo uliloanzisha.
Na kama unataka kutimiza jambo, itabidi kufanya, hata kama litaambatana na matukio ya  kushindwa na kukataliwa. Na kila hatua utakayopiga utajisikia vizuri kuliko kitu kingine chochote unaweza kufikiria. 

Utagundua kuwa mapambano hayapatikani katika njia, bali ni njia. Na ni thamani yake. Hivyo kama wewe unakwenda kujaribu,nenda njia yote. Hakuna hisia bora katika dunia ... hakuna  hisia bora kuliko kujua nini maana ya kuwa hai.

      6.       MITAZAMO HASI YA WENGINE SIO TATIZO LAKO


Kuwa na mtazamo chanya wakati mazingira yametawaliwa na mitazamo hasi. Tabasamu wakati wengine wanajaribu kukurudisha chini. Si jambo rahisi kudumisha shauku yako na kuzingatia unakoelekea. Wakati watu wengine wanakutenda vibaya, endelea kuwa wewe. Milele usiruhusu tabia chungu za mtu mwingine zilete mabadiliko kwako.

Zaidi ya yote, milele usikubali kubadilika ili kumvutia mtu ambaye anasema wewe hauna uwezo. Badilika sababu itakufanya mtu bora na itaenda kubadilisha kitu katika maisha ya mbeleni. Watu wataendelea kuzungumza bila kujali nini unafanya, hata iwe unafanya vizuri kiasi gani. Hivyo kuwa na wasiwasi kuhusu mwenyewe kabla ya kuwa na wasiwasi kuhusu nini wengine wana kufikiria. Kama unaamini kwa dhati katika kitu, wala hupaswi kuwa na hofu ya kupambana kwa ajili yake. Nguvu kubwa inatokana na kushinda kitu ambacho wengine walifikiria hakiwezekani.


Utani wote weka pembeni, maisha yako yanakuja mara moja tu. Huo ndio ukweli. Hivyo kufanya kitu kinachokupa furaha ndio kinapaswa kuwa kipaumbele chako.

Share this post:

Digg it StumbleUpon del.icio.us Google Yahoo! reddit

0 comments:

Post a Comment

 
Copyright 2013-2017 Lisha Ubongo
| Branded by www.pixelbase.co.tz