Si kila mwenye mafaniko leo hii,
 aliyapata kwa mara ya kwanza
 alipojaribu.
Mara nyingi ni watu ambao walijaribu mara nyingi bila mafanikio,
 kabla hawajapatia na 
kufanikiwa.

Na wengi wao ni wale,
 waliokuwa wamejitolea kupambana 
na vikwazo 
kutoka kwa watu
 mbali mbali na mifumo.

Wanapovuka hatua hii ya vikwazo,
 wengi wao 
wanakosa majibu ya moja kwa moja wamefikaje hatua hiyo
 ya mfanikio pamoja na vikwazo vyote walivyokutana navyo.

Kuna siri imejificha hapa?
Ndio, 
kushindwa mara nyingi na bado kuendelea kunga'ang'ania mpaka unashinda,
 inaonyesha kuna kitu
 alikiona hapo.

Ni kipi hicho?
Nadhani,
 tunahitaji makala itakayojitegemea, 
kuelezea siri iliyopo 
hapa kwa watu wengi
 waliofanikiwa.

Unapopatwa na wakati mgumu,
 iwe katika masomo au kazini 
hupaswi kukata tamaa mapema 
bali 
tumia historia fupi za watu hawa kujitia 
nguvu ya kusonga 
mbele.

Watu hawa waliofanikiwa wapo katika makundi makuu 8.
Leo tunaanza na kundi la kwanza la 
wafanya biashara.

1.Henry Ford:

Huyu ni mfanyabiashara raia wa Marekani,
alizaliwa 
30 julai 1863 katika familia ya wakulima wadogo,
 na kufa 7 Aprili 1947.
Ndiye aliyeanzisha
 kampuni kubwa ya magari aina ya Ford.
 Aliondoka kwao,
 akiwa na miaka 16 tu
 na kwenda kutafuta 
ajira ya umakenika.
Kabla hajafanikiwa,
 alifilisika kibiashara mara tano.
 Alianza kuonja mafanikio baada ya kubuni 
gari la kwanza kutengenezwa 
Marekani aina ya 
Ford Model T.


2.R. H. Macy:

Ni raia wa Marekani
 ambaye alikuja kuanzisha 
biashara ya idara ya stoo kubwa za biashara
 katika jiji la
NewYork.
Alizaliwa 30 Agosti 1822 na 
kufariki 29 machi 1877.
Kabla hajafanikiwa katika wazo hili alifeli mara saba.

3.F.W. Woolworth:
Huyu ni raia wa Marekani ambaye alifanya kazi katika stoo ya bidhaa ya 
mfanyabishara mwengine,
ambako alipokea manyanyaso 
mengi hadi yakamfanya 
aamue kukaa chini na 
kupata wazo la yeye kufungua stoo zake mwenyewe za biashara.
Alizaliwa 13 Aprili 1852 na
kufa 8 Aprili 1919. 
Hata huku Tanzania kuna maduka yenye hili 
jina lake moja 
maeneo ya Posta PPF Tower.

4.Soichiro Honda:
Ni raia wa Japan,
na muanzilishi wa kampuni ya Honda.
Aliwahi mara kadhaa kuomba 
kazi katika kampuni ya
 Toyota kama injinia,
lakini alikosa baada ya 
kufanyiwa usaili na 
kuonekana hana vigezo.
Alikaa muda mrefu sana bila kuwa na 
kazi,
 kitu kilichomfanya 
akae chini kufikiria na kuibuka na 
wazo la 
kampuni ya Honda.
Alizaliwa 17 Novemba 1906 na
 kufa 5 Agosti 1991.
 Ambayo imekuja kuwa mpinzani wa kampuni iliyomkataa.

5.Akio Morita:
Ni raia wa Japan,
na muanzilishi wa
 kampuni ya Sony.
Bidhaa yake ya kwanza,
 kuanzisha ilikuwa ni 
jiko la kupikia mchele(Rice cooker) 
ambayo ilikuwa inaunguza sana wali hivyo watu waliacha kununua bidhaa hiyo.
Lakini,
 hakukata tamaa mpaka 
alipokuja kuboresha na 
kuja kukubalika tena na bidhaa 
nyingi tofauti tofauti
 za vifaa vinavyotumia umeme.
Alizaliwa 26 Januari 1921
na kufa 3 Oktoba 1999.

6.Bill Gates:

Ni raia wa Marekani,
alizaliwa 28 Oktoba 1955 mpaka leo bado anadunda.
Alianza na mkosi wa kufukuzwa
 chuo cha Harvard
ambapo aliamua kuanzisha biashara 
na mwenzake kwa jina la kampuni 
iliyoitwa Traf-O-Data 
ambayo 
haikufanikiwa kabisa.
Alipopata wazo la kutengeneza kompyuta alilipeleka katika kampuni moja ambapo lilikataliwa.
Hakukata tamaa na mwisho wa uvumilivu wote akaja na kampuni ya 
Microsoft ambayo imempa utajiri 
usioelezeka.

7.Harland David Sanders:
Ni raia wa Marekani,
na muanzilishi wa kampuni ya kukaanga kuku ya Kentucky Fried Chicken(KFC).
Alipoanza hii biashara alikataliwa mara 1,009 na migahawa ya Marekani kumpa 
oda ya kuku anaouza.
Lakini uvumilivu wake ukaja kumpa mafanikio makubwa katika biashara hiyo hiyo.
Alizaliwa 9 Septemba 1890 na 
kufa 16 Desemba 1980.

8.Walt Disney:
Kwa wale wapenzi wa 
filamu na katuni,
huyu ndio mtu aliyewaingizia 
hiyo burudani kwa mafanikio sana.
Alianza kwa kufanya kazi ya 
uhariri wa gazeti 
ambapo alifukuzwa kwa 
kuonekana hana ubunifu.
Na alikuja kuanzisha miradi 
 mbali mbali ambayo haikuweza kudumu muda mrefu na kumfilisi kabisa.
Lakini mwisho wa uvumilivu wake akaja kufanikiwa katika 
kampuni yake ya Disney ambayo 
inajihusisha na filamu na katuni.
Alizaliwa 5 Desemba 1901 na 
kufa 15 Desemba 1966.

USIOGOPE KUSHINDWA,
KILA KITU USIPOJARIBU
 HAUTAWEZA KUKIJUA KAMWE.

KAMA WEWE UNATAKA KUFANYA BIASHARA 
AU 
ULISHAANZA,
 UKISHIDWA USIKATE TAMAA.
 ENDELEA KUNG'ANG'ANIA KAMA 
UNAJUA NDICHO KITU PEKEE UNACHOWEZA KUFANYA 
KATIKA MAISHA YAKO.

USIKATISHWE TAMAA NA WAFANYABIASHARA AMBAO WANADHANI WANAFAHAMU KILA KITU ,
KWA KUKOSOA WAZO LAKO.
 NAO PIA KUNA VITU HAWAJUI HATA KAMA WAMESHAFANIKIWA KWA HIYO PIGANIA ULICHONACHO.

Share this post:

Digg it StumbleUpon del.icio.us Google Yahoo! reddit

0 comments:

Post a Comment

 
Copyright 2013-2017 Lisha Ubongo
| Branded by www.pixelbase.co.tz