Laurie Notaro aliwahi kusema;

“If you really believe in what you're doing, work hard, take nothing personally and if something blocks one route, find another. Never give up”.

Kauli hii ikimaanisha;

 “Kama unaamini katika kile unachofanya, fanya kwa bidii, usifanye ubinafsi na kama kuna jambo litajitokeza kufunga njia moja, tafuta njia mbadala. Usikate tamaa”.

Kukata tamaa ni kitendo cha kuishiwa mbinu mbadala za kukamilisha jambo Fulani ulilokuwa unalifanya kwakuwa tu umekumbana na ugumu. Katika kila jambo tunalofanya huwa tuna matarajio ya kufanikiwa ila pia changamoto haziwezi kuepukika.


Maneno “Kata” na “Tamaa” hayatakiwi kuwa pamoja. Hata neno hapana halipaswi kuwa sehemu ya neno katika kamusi yako. Kuwa sehemu ya jamii ya watu Fulani katika dunia unakuwa ni kiumbe wa pekee kuwahi kutembea juu ya ardhi hii.

SABABU 8 ZA KWANINI HUTAKIWI KUKATA TAMAA

      1.UPO HAI,NA UNAWEZA



Yaani ilimradi una pumua pumzi ya uhai, hakuna uhalali wa wewe kusema kuna jambo limekushinda na unalikatia tamaa. Kama ukiweka akili na mawazo yako katika hilo jambo lazima utaweza kufanya japo kufanikisha sehemu yake. Hakuna lisilowezekana chini ya jua.

Christopher Reeve aliwahi kusema;
So many of our dreams at first seem impossible, then they seem improbable, and then, when we summon the will, they soon become inevitable.

Ikimaanisha; “Ndoto zetu nyingi kwa mara ya kwanza huonekana haziwezi kuwa kweli, baadae huonekana haziwezekani kabisa, ila, tunaipoita utayari wa kufanya ndani yetu, punde zinakuwa haziwezi kuepukika”

Udhuru pekee unaoweza kuutoa kwa kutoweza kutimiza ndoto zako ni ikiwa umekufa ila kama unaweza kusoma hapa, hakuna cha kukuzuia.

       2. AMINI KATIKA NDOTO ZAKO


Ukikata tamaa, unajikatia tamaa mwenyewe na si mtu mwengine yeyote. Usijiuze mwenyewe wala kuruhusu mtu mwengine akurudishe nyuma. Kama unaweza kuwa na ndoto zako mwenyewe basi hata uwezo wa kutimiza unao.

Kuna mamilioni ya watu wa kale waliokuwana na ndoto zao katika ulimwengu huu, kama na wao wangekata tamaa hapo mwanzo hii dunia isingekuwa hivi unavyoiona leo.

Chukulia mfano ndugu wawili kutoka katika familia ya Wright waliokuwa wana ndoto za kutengeneza ndege jinsi walivyokumbana  na vikwazo vya kuifanya ndogo yao kuwa kweli huku hakuna aliyedhani kama ndoto inawezekana kwa kuwacheka na kejeli. Hawakukatishwa tamaa ila walipambana kuifanya ndoto yao kuwa kweli na walifanikiwa, je usafiri wa ndege si kiunganishi muhimu katika dunia ya leo?

Langston Hughes aliwahi kusema;
“Hold fast to your dreams, for without them life is a broken winged bird that cannot fly.

Ikimaanisha;
“Shikamana na ndoto zako, kwakuwa bila ya hizo maisha ni sawa na ndege aliyevunjika mabawa asiyeweza kuruka”

      3.UNA KILA KITU UNACHOTAKA

Kila unahohitaji ili kufikia malengo yako, kimewekwa tayari ndani yako. Usiwe mtu wa kutoa udhuru, kama inawezekana kuwa na wanamichezo walemavu wenye uwezo wa kushiriki michezo katika kiwango cha olimpiki,mapungufu yako hayawezi kukuzuia kutimiza ndoto yako. Mshukuru Mungu na tumia uwezo aliokupa kufanikisha ndoto zako.

      4. HAUHITAJI KUJA KUJUTA

Majuto ni hisia mbaya sana mtu kuwa nayo. Usiruhusu nafsi yako ijiweke katika mazingira ya kuja kujuta ila unapaswa ufanye unachotakiwa kufanya sasa.

Rory Cochrane alisema;
“I do not regret the things I've done, but those I did not do

Ikimaanisha;
“Sijutii kwa vitu nilivyofanya, ila kwa yale yote ambayo sikuyafanya”

      5.UNATAKIWA UJITHIBITISHIE MWENYEWE


Unatakiwa uje ujithibitishie mwenyewe na ulimwengu mzima kwamba unaweza kufanya jambo. Usiruhusu jambo au kitu chochote kikuzuie kutimiza ndoto zako.

Kushindwa kwa kweli si kule kujaribu na kukosa, bali ni kule kutojaribu kabisa.
Wewe unaweza kutimiza ndoto zako, sababu wanaoshindwa ni watu wasiofanikiwa daima.

      6.UTAPATA MABADILIKO MAZURI


Inawezekana kabisa unapitia wakati mgumu sasa, lakini ukishikilia kwa muda utapata mabadiliko ya haraka na mazuri. Kama utaendelea kupambana hutakiwi kukata tamaa sababu huwezi jua lini ndio siku yako ya kutoboa.

Usiwe kama mtu anayechimba kisima ambaye hadi anafika mita 50 hajapata maji, anakata tamaa na kuacha lakini anakuja mwengine anachimba mita 1 tu toka pale alipoishia yeye anakutana na maji. Kama umeamua fanya kweli mpaka upate matokeo.

      7.UNAPASWA KUTIMIZA

Si kila mtu anaweza kusikia sauti ya ndani inayomwambia afanye jambo Fulani, ila kama wewe umeweza kuisikia ikikwambia timiza jambo Fulani, nakwambia usiachie bila kutimiza sababu umeumbwa ili kufanikisha hilo.

      8.HAMASISHA WENGINE

Katika maisha yetu lazima kuna watu uliowazidi watakuwa wanakuangalia kama mtu wao wa mfano, mathalani wadogo zako au hata watu wa karibu na majirani. Sasa wanapokuona wewe umekata tamaa inawakatisha tama hata wao. 

Ndio maana hutakiwi kukata tamaa sababu hujui wangapi wanakuangalia, ushindi wako utawapa hata wao nguvu ya kupambana katika safari yao kwa kuwa walishawahi kuona Fulani aliweza.



Kuna idadi ya kutosha ya mitazamo chanya ndani yako ambayo pengine haujaweza kuitambua na inasubiri kuamshwa. Na kila wakati unapopoteza motisha unapaswa kujikumbusha kwa haraka uwezo wako. 

Daima kumbuka kwamba ladha ya mafanikio daima inakabiliwa na kushindwa kwa muda. Kama wewe utakata tamaa kutokana na magumu ya muda utakuwa unajiandaa kushindwa, lakini kama wewe utaendelea kupambana utakuwa na mafanikio.

Share this post:

Digg it StumbleUpon del.icio.us Google Yahoo! reddit

0 comments:

Post a Comment

 
Copyright 2013-2017 Lisha Ubongo
| Branded by www.pixelbase.co.tz