VIZA 
             Viza ni cheti au muhuri maalumu unaowekwa 
(katika hati ya kusafiria ya mwombaji) na mamlaka ya uhamiaji ya            nchi husika ambayo mwombaji anataka kutembelea,
alama hii ina maanisha mwombaji amepewa ruhusa ya kuingia nchi                           husika kwa muda maalumu.
Kuna viza ambazo zinaweza kukuruhusu uingie mara moja na kutoka                         (Single entry visa) na 
kuna viza nyingine zinakuruhusu kuingia na kurudi zaidi ya mara             mpaka pale muda uliopangwa kuisha matumizi ufike 
                     (multiple entry visa).


                             Viza za muda
Kuna aina mbali mbali za viza za muda zinazotolewa na ubalozi wa Marekani. Aina hizi za viza zinatambulika na sheria ya Uhamiaji ya Marekani(Immigration Law)na inaenda sambamba na dhumuni la kusafiri mwombaji.

Viza hizi zimewekwa kwa ajiri ya wasafiri ambao wana nia ya kukaa Marekani kwa muda na kurudi nchini kwao.
             Aina za Viza za muda ni pamoja na:
               .       Biashara na Utalii (Mapumziko)
2              .       Matibabu
               .       Wanafunzi
     .       Mwanadiplomasia, Maofisa wa serikali, na Wafanyakazi wa mashirika ya kimataifa 
               .       Wageni wa kubadilishana.
               .       Wafanyakazi wa muda
7              .       Waandishi wa habari
8              .       Wafanyakazi wa mashirika ya dini

         A.      Biashara na Utalii (Mapumziko)

Kutokana na dhumuni lako hili la kwenda Marekani, Unahitaji aina hizi za Visa B1, B2 au B1/B2 viza.

                  B1-Waingiaji wa muda Kibiashara
Umewahi kujiuliza unahitaji viza ya aina gani ili uweze kufanya biashara Marekani?
Kama unataka kuingia Marekani kwa dhumuni la biashara unahitaji aina hii ya viza. Viza hii haitakuruhusu ukubali ajira Marekani,lakini unaweza kukubaliana mkataba, mashauriano na washirika wa kibiashara,kukutana na wateja,kushiriki makongamano na semina na kuchukua oda za wateja.
                           
       
              B2-Waingiaji wa muda Utalii (Mapumziko)
 Umewahi kujiuliza unahitaji viza ya aina gani ili uweze kufanya utalii au kutembelea marafiki Marekani? 
Unahitaji viza hii kama una dhumuni la kuingia marekani kwa ajiri ya mapumziko, au kuitembelea familia na marafiki.

     B1/B2- Waingiaji wa muda wa biashara au utalii (Mapumziko)

Umewahi kujiuliza kama unataka kutembelea maonyesho ya biashara halafu ukitoka hapo ukashangae shangae kidogo mambo mengine?
Unahitaji viza aina ya B1/B2 kama unataka kwenda Marekani kwa dhumuni la ama biashara au mapumziko au kwa shughuli maalumu,elimu, dini, makongamano ya kitaaluma,kozi za muda mfupi, kushauriana na washirika wa kibiashara au wataalamu,kutibiwa, kushiriki katika shughuli za kujitolea katika mashirika ya misaada au kushiriki katika michezo.


                      B.      Matibabu

Ili hali yako ya ugonjwa ipewe kipaumbele unapoomba viza unatakiwa                        uwe na taarifa zifuatavyo:                       
   a) Barua iliyoandikwa kwa lugha ya Kiingereza kutoka kwa daktari wako wa hapa Tanzania:
-          Ikielezea hali yako ya ugonjwa;
-          Inayofafanua chanzo cha ugonjwa na sababu za kuhitaji matibabu Marekani.

   b)      Ushahidi wa fedha ya kutosha kwa matibabu:
-          Ushahidi wa ufadhili wa kifedha au hati ya kiapo cha ufadhili (Fomu 1-134) kutoka kwa mfadhili. Zinatakiwa hati halisi tu-faksi na nukushi hazikubaliwi.
-          Uhakika kutoka kwa mfadhili kwamba mgonjwa atakuwa na tiketi ya kurudi.
-          Barua kutoka kwa mwajiri wa mfadhili  ikiwa na anuani ya kampuni ikieleza cheo chake kazini, mshahara, na mwisho wa ajira yake.
-          Barua kutoka benki ya mfadhili ikiwa na anuani ya benki  na ikiwa imesainiwa na ofisa wa benki.
-          Ripoti ya ulipaji kodi wa mfadhili kwa mwaka uliopita.


    c)       Barua binafsi ya mfadhili kwenda ubalozi wa Marekani
-          Ikieleza wapi hasa mgonjwa atafikia wakati wote ambao atakuwa anahudhuria matibabu.
-          Ikielezea kwa nini ameamua kumfadhili mgonjwa (mwombaji wa viza), Historia kamili ya uhusiano wao, ni wa vipi na ulianza linin a anatarajia kupata nini kutokana na ufadhili wake.

    d)      Barua kutoka kwa daktari wa Marekani:
-          Ikieleza hali ya mgonjwa na utayari wa kumtibu.
-          Makadirio ya juu na ya chini ya kipindi atakachokuwa         anamtibu mgonjwa
-          Makadirio ya juu na ya chini ya gharama za matibabu (Ada       ya daktari, ada ya hospitali, gharama za vipimo,        gharama za dawa na gharama zote zitakazohusiana matibabu)
-          Uhakika kwamba gharama za matibabu zitalipwa na fungu       lipo tayari kwa ajili ya kugharamia.
-          Tarehe maalumu ya ahadi.

Sheria ya uhamiaji ya taifa la Marekani imeweka dhahania kuwa       waombaji wote wa viza za muda wana nia ya kukaa Marekani moja kwa moja. 
Kwahiyo kuwa na vigezo vya kupata aina hizi za viza za muda unahitaji kuwathibitishia kuwa dhahania yao si sawa kwako na hauna   nia ya kukaa moja kwa moja.

Unaweza kuishinda hii dhahania yao kwa kuwapa ushahidi kuwa wewe una mambo ya msingi yatakayo kurudisha nyumbani na wala huna nia ya     kuikimbia nchi yako.

Itaendelea.....

Share this post:

Digg it StumbleUpon del.icio.us Google Yahoo! reddit

8 comments:

Unknown

Asante kwa elimu uliotupa, ila nina maswali mawili,
1:Malipo ya visa ni Tsh ngapi au $?
2:na vigezo au sababu za muhimu kuachia utalii mf nataka kwenda kuishi huko bt najua hawatakubali nitumie njia gani kwa.convince wanipe visa...? Asanteni

Unknown

Asante kwa elimu uliotupa, ila nina maswali mawili,
1:Malipo ya visa ni Tsh ngapi au $?
2:na vigezo au sababu za muhimu kuachia utalii mf nataka kwenda kuishi huko bt najua hawatakubali nitumie njia gani kwa.convince wanipe visa...? Asanteni

Unknown

Kwakweli nahitaji visa niende america kwa shughuli za kimuziki na kujifunza mambo machache huko nifanyaje??????

Unknown

Naitwa john benoit naishi south Africa nikuwa napenda kujuwa bei ya visa ya marekani iko ku dollar ngapi ...pia na visa ya Australia pia iko ku dollars ngapi?

Unknown

Naitwa Richard Frank niko dar nataka kujua njia gani za kufata ili kupata visa ya American maana nimejarbu kusoma hapo sipati majibu sahihi ya kufata

Unknown

Nataka viza ya kwenda marecani kutembeaa je niende na vigezo au vitu gani wanavyo itaji ubalozi

Unknown

Thanks for being given an education

Post a Comment

 
Copyright 2013-2017 Lisha Ubongo
| Branded by www.pixelbase.co.tz