Kama umeshindwa jambo
 na unafikiria 
kuwa upo mwisho wa safari yako 
na huna sehemu nyingine ya kwenda,
tambua 
unajidanganya nafsi yako.

Umejifunga jela mwenyewe 
na mawazo yako ya 
kujikatisha tamaa.

Kwa kufikiria hivyo 
ni kujitengenezea nafasi ndogo ya kufanikiwa katika unalofanya,
 na nafsi yako itaanza kuamini wewe ni 
mtu wa kushindwa.

Tunaishi katika ulimwengu wenye njia nyingi za kufanikiwa katika 
yale tunayojihusisha nayo.

Haya ndiyo unapaswa uyafikirie kabla ya kukata tamaa:

1.UMERIDHIKA NA KUSHINDWA?

Kushindwa si kuanguka chini;
ila ni kushindwa kunyanyuka wakati una nafasi ya kunyanyuka.
Mara nyingi ni lazima kushindwa mara nyingi ili ufanikiwe.
Na ndio maana unaposhindwa mara moja sio mwisho wa kila kitu.
Wazo lako lolote ambalo limeshindwa 
kufanya kazi,
linafungua njia ya wazo litakaloshinda.
Ukishindwa na ukaanza kukubaliana na 
hilo maana yake ni 
kuridhika na kushindwa.

2.UMEJIFUNZA NINI LA MUHIMU?

Maisha siku zote yanatoa nafasi ya pili,
ili usahihishe makosa.
Lakini
 nafasi hii ya pili haitakuwa na 
maana yoyote kama hakuna ulilojifunza 
katika kosa lililopita.
Unatakiwa ukubali udhaifu wako 
lakini
 kusanya nguvu kupitia hayo na ujifunze kitu ndani yake.
Unapofanya kosa 
chukua nafasi ya kutafuta nafasi ya pili kusahihisha kosa hilo
 na ukusanye uzoefu mpya.

3.WEWE NDIO WA KWANZA KUKUTANA NA MAGUMU?

Maisha huanza na maisha huisha,
kuna muda maisha yanacheka na maisha yanalia,
maisha yanakata tamaa na 
maisha yanajaribu.
Maisha yana picha tofauti katika macho ya kila binadamu aliye juu ya ardhi.
Ukweli ni kuwa vile ulivyokuwa zamani,
ulivyo sasa na 
yule utakayekuja kuwa ni 
watu watatu tofauti.

4.MAUMIVU YAMEKUSAIDIA NINI?

Kuna muda lazima mambo yabadilike ili na
 wewe ubadilike.
Lazima kuna muda upate maumivu ili ukue kiuzoefu.
Kuumia ni lazima ili upate hekima ambayo haukuwahi kuiwaza kama utaipata.
Lazima uumie moyo 
ili uanze kuufuata moyo wako katika 
maamuzi sahihi.

5.KUFANIKIWA NI KUWA NA NINI?

Usiruhusu mahangaiko yako ndio yakutambulishe kwa watu wewe ni nani.
Sio kila kitu unavyokitarajia kiwe kitakuwa hivyo hivyo ulivyodhani wewe.
Na ndio maana unapaswa kuacha kuishi matarajio,
ishi wakati ulionao na fuata mkondo na si kwenda kinyume na njia ya mkondo.
Jikumbushe kuwa ni ukamilifu kutokuwa mkamilifu.
Mafanikio si kitu unachopata,
ila ni uwezo wako wa kufanyia kazi uliyojifunza na kuyatumia kwa ufanisi katika uhalisia wa maisha yako.

6.KUNA NJIA NYINGINE YOYOTE?

Tofauti ya njia nyembamba na ndogo inajengwa na mtazamo wako.
Na hapo ndio unapaswa ujue kuwa ili kubadilisha kitu ni lazima ubadilishe 
mtazamo wako.
Kutoweza kuona njia mbadala 
katika maisha yako inatokana na
 mtazamo wako 
kujifungia eneo moja la maisha.

7.KUNA JAMBO LINAWEZA KUFANIKIWA BILA KIKWAZO?

Hata kama haupo
 sehemu ambayo ulitamani kuwa haimaanishi kuwa hautakuwa siku moja.
Kufanikiwa kunaambatana na kujitambua ambapo kutakusaidia kupambana 
mpaka mwisho.
Mafanikio bila ya vikwazo vitakufanya usione thamani yake
 na unaweza kuyatumia vibaya.
Ukuta uliokutenga na ndoto yako unakusaidia kufahamu ni jinsi gani utajitoa kufikia unalotamani kwa kuuvunja.

8.ZURI NI HILO TU?

Unaweza ukawa umekutana na mabaya wakati unatafuta mazuri fulani,
lakini
haimaanishi hayo mazuri uliyoyakosa ndio pekee yaliyopo duniani.
Maisha yana mambo mengi mazuri na 
si yale tunayodhani sisi 
kuwa ni mazuri na kuyaona mengine kuwa mabaya kwa kuwa ndivyo tunavyodhani.

KUKATA TAMAA KATIKA MAISHA, 
SI KITU 
CHA KUKIFIKIRIA KWANZA PALE UNAPOKUMBANA 
NA MAGUMU.

HAKUNA UTAKALOPANGA KULIPATA,
 UKALIPATA KIRAHISI RAHISI KAMA WENGI WETU TUNAVYOTAMANI IWE.

TUMIA MASWALI HAYO HAPO JUU,
 KUJIULIZA PALE UNAPOKUMBANA 
NA WAKATI MGUMU ILI USIKATE TAMAA.

Share this post:

Digg it StumbleUpon del.icio.us Google Yahoo! reddit

0 comments:

Post a Comment

 
Copyright 2013-2017 Lisha Ubongo
| Branded by www.pixelbase.co.tz