Iwe ni mara yako ya kwanza,
au umezoea kutoka na mtu wa jinsia tofauti lazima kuna vitu uzingatie ili usiharibu ladha na maudhui ya mtoko wako.
Kwani ni ukweli ulio wazi kuwa mpaka umekubali kupata mtoko na mtu wa jinsia tofauti maana yake unafurahia uwepo
 wake karibu yako.
Na pengine ushaanza fikiria mipango ya baadaye ukiwa naye.
Lakini kuna makosa ambayo tunayafanya wengi wetu siku ya kwanza unapotoka na mtu wa jinsia tofauti.

Pitia vipengele vifuatavyo ugundue unafanya wapi makosa na uyaepuke.

1.USIMZUNGUMZIE MTU WAKO ALIYEPITA

Hili ndio kosa kubwa la kwanza ambalo wengi wanalifanya wanapokuwa katika mtoko na mtu mwengine wa jinsia tofauti.
Tambua wazi si kwamba utamuonyesha kuwa una hisia na watu unaowahi kuwa nao,
 lakini ujue unamuudhi mtu uliyetoka naye.
Kuleta suala la mtu mwengine aliyepita wakati uko na mwengine halina maana yoyote kama umekosa la kuongea heri unyamaze hadi uulizwe.

2.USIZUNGUMZIE NGONO

Kabla hujajua kama unayetoka naye anapendelea mazungumzo ya aina gani,
usikurupuke kuzungumzia habari hizo kana kwamba wewe ni mtaalamu sana ukidhani utamvutie uliyetoka naye.
Kama uliyetoka naye ana malengo ya mbali utamfanya afikirie mara mbili kama utamfaa siku za mbele.

3.USIJIZUNGUMZIE WEWE KILA WAKATI

Kujizungumzia wewe kila wakati itamuonyesha uliyetoka naye kuwa una ubinafsi ndani yako.
Kila mtu angependa kupata nafasi ya kujielezea mbele ya mwenzake lakini kama wewe unamkatisha na kujizungumzia wewe tu utamtisha.
Ukionyesha unampa nafasi ya kumsikiliza anachoongea yeye utamfanya aone wewe ni msikivu.
Na ukiwa msikivu kwa mwenzako utapata nafasi ya kumtambua uliyetoka naye anapendelea mazungumzo ya aina gani.

4.IJUE HISTORIA YAKE

Tafuta taarifa za mtu unayetaka kutoka naye kabla haujafanya hivyo,
kwasababu wengine wana tabia ya kurudia matukio mabaya waliyoyafanya siku za nyuma.
Ukijichanganya kutoka na mtu bila kujua ana tabia gani anapofanya mtoko na mtu wa jinsia tofauti usije ukakumbana na balaa.
Wengi walipatwa na mabaya kwa kutojua historia ya wanaotoka nao na baadaye kujutia.

5.USITUMIE LUGHA CHAFU

Hata kama ni kawaida yako kuzungumza kwa 
lugha chafu,
unapotoka na mtu kwa mara ya kwanza jitahidi kuficha mizuka yako.
Kutumia lugha chafu kwa kudhani utamuonyesha uliyetoka naye kuwa unajiamini na umuogopi ni kujiongopea.

6.KUVAA HOVYO

Tabia ya kumchukulia poa unayetoka naye na kuvaa hovyo ili ujionyeshe kuwa unaamua unalotaka,
unaharibu taswira yako kwake.
Kwani wengi huona kama umeshindwa kumuonyesha kumuheshimu siku ya kwanza au kabla hamjawa pamoja inawezekana ukamuonyesha dharau zaidi utakapokuwa naye.

7.USIBEBE ZAWADI ZA GHARAMA

Kumbuka huo ni mtoko tu na sio sherehe.
Unapobeba zawadi za gharama kubwa kwa mwenzako si kwamba utamfurahisha lakini ndani yake utamfanya akuone kuwa upendo wako pia unajengwa zaidi na vitu vya gharama.

8.USISHAMBULIE WENGINE

Ukiwa umetoka na mtu usianze kumzungumzia vibaya mtu au watu wengine,
kwani utamuonyesha wazi kuwa ipo siku na yeye itakuwa zamu yake.

9.USINYWE MPAKA UKALEWA

Hata kama ulikuwa na kiu kubwa  ya kunywa pombe angalia usivuke kiwango mpaka ukalewa na usijielewe.
Tabia hii itamuonyesha ishara mbaya juu yako.

UFANYE MTOKO WAKO KUWA WA KAWAIDA, 
MSAFI, KUFURAHISHA,
NA WAKUKUMBUKWA.

ANZA SASA KUWA MAKINI UNAPOKUWA UMETOKA NA MTU WA JINSIA TOFAUTI ILI USIHARIBU SIKU YAKO YA KWANZA YA MTOKO NA KUMPOTEZA MTU AMBAYE UNGETAMANI AWE KARIBU YAKO.

Share this post:

Digg it StumbleUpon del.icio.us Google Yahoo! reddit

0 comments:

Post a Comment

 
Copyright 2013-2017 Lisha Ubongo
| Branded by www.pixelbase.co.tz