UELEWE KWA UFUPI MPANGO WA MAENDELEO WA MILENIA (MDGs)

Mwaka 2000 mwezi wa tisa nchi wanachama wa umoja wa mataifa zipatazo 189 zilikutana na kuasisi mpango wa maendeleo wa milenia ulioitwa Millenium Development Goals(MDGs) kwa lugha ya kiingereza.
Nchi hizi wanachama ulizitaka nchi zilizoendelea na zinazoendelea kushirikiana kwa pamoja ili kupunguza Umasikini, Njaa, Magonjwa, Vifo kwa akina mama na watoto, Fursa sawa kwa wanawake na Afya bora ya mazingira.
Nchi wanachama zilianza kuchukua takwimu za mwaka 1990 mpaka 2015 ambapo ndio lengo linapaswa kuwa limeshafikiwa na nchi wanachama.
Moja ya nchi wanachama ni Jamhuri ya muungano wa Tanzania ambapo ili kufikia lengo hilo iliandaa mikakati pande zote mbili za muungano(Tanzania bara na Zanzibar).
Tanzania bara ilianzisha MKUKUTA(Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini Tanzania) na Zanzibar ukaanzishwa MKUZA(Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kuondoa Umasikini Zanzibar).

Share this post:

Digg it StumbleUpon del.icio.us Google Yahoo! reddit

1 comments:

Post a Comment

 
Copyright 2013-2017 Lisha Ubongo
| Branded by www.pixelbase.co.tz