Acha ukweli usemwe, furaha ya kweli si kutokuwa na matatizo, lakini ni uwezo wa kukabiliana nayo kwa ujasiri. Mara zote angalia kile ulicho nacho mkononi, badala ya kufikiria ulichopoteza. Sababu haijalishi dunia imechukua nini kutoka kwako, bali utafanya nini na kile ulichobaki nacho mkononi.



Yafuatayo ni mambo sita unayopaswa kujikumbusha kila unapopatwa na jambo gumu linalotaka kukukatisha tamaa ili usisonge mbele.  
    
      1.       MAUMIVU NI SEHEMU KATIKA UKUAJI



Kuna kipindi maisha yanafunga mlango sababu ni muda muafaka kusonga mbele. Na hiki ni kipindi kizuri sababu mara nyingi hatuwezi kusonga mbele wenyewe mpaka matukio Fulani yatokee kutusukuma ndo tunasonga.
Mambo yanapokuwa magumu jikumbushe kuwa hakuna maumivu yanayokuja bila dhumuni maalumu. Songa mbele baada ya maumivu lakini usisahau ulichojifunza kipindi cha maumivu.

Eti kwasababu una pata mahangaiko ndo imaanishe kuwa unafeli maisha. Kila jambo lolote kubwa la mafanikio huwa haliji kirahisi mpaka liambatane na mahangaiko ya hapa na pale. Mambo mazuri huchukua kipindi kirefu kukamilika. Kuwa mvumilivu na kuwa na mtazamo chanya. Kila kitu kitaenda kuwa sawa, labda sio kwa kasi unayoitaka wewe lakini mambo yatakuwa sawa tu.

Kumbuka kuna maumivu ya aina mbili, kuna yale yanayokuumuiza na yale yanayokubadilisha. Ukiwa unaenda na mtiririko wa jinsi maisha yanavyokwenda, badala ya kupingana na mabadiliko, itakusaidia kukua.

      2.       KILA KITU KIPO KWA MUDA TU



Kila wakati mvua inaponyesha, huwa kuna muda itaacha. Kila wakati wewe unapopata madhara, kuna wakati wa wewe kupona. Baada ya giza daima kuna mwanga - wewe hili unakumbushwa kila asubuhi, lakini bado mara nyingi unasahau, na badala yake unachagua kuamini kwamba usiku utadumu milele. Haitakuwa hivyo. Hakuna kinacho dumu milele.

Hivyo kama mambo ni nzuri sasa hivi, furahia. Sababu haitadumu milele. Kama mambo ni mabaya, msiwe na wasiwasi kwa sababu haitakuwa milele. Kwa sababu tu maisha si rahisi wakati huu, haina maana huwezi kucheka. Kwa sababu tu kitu  kinakusumbua wewe, haina maana huwezi tabasamu. Kila wakati unakupa mwanzo mpya na mwisho mpya. Unapata nafasi ya pili, kila wakati . Wewe unapaswa kuchukua nafasi na kuufanya kuwa ni wakati bora zaidi.

     3.       KUWA NA HOFU NA KULALAMIKA HAKUBADILISHI KITU


Wale ambao wanalalamika zaidi, kukamilisha mambo inakuwa ni ngumu. Ni vyema kujaribu kufanya jambo kubwa na kushindwa kuliko usijaribu kufanya chochote na utarajie kufanikiwa. Sio mwisho kama umefanya jambo na ukashindwa; na sio mwisho pia kama haujafanya jambo lolote lakini ukaishia kulalamika kuhusu hilo jambo.

Kama unaamini katika kitu, usiache kuendelea kujaribu. Usikubali vivuli vya zamani vikazima hatua zako za maisha yako ya baadaye. Ukiwa unaitumia leo kulalamika kuhusu jana hautaifanya kesho kuwa nzuri. 

Badala yake chukua hatua. Hebu tumia ulichoweza kujifunza kuboresha jinsi ya kuishi. Endelea kufanya mabadiliko na kamwe usiangalie nyuma.

Furaha ya kweli utaipata pale tu utakapoacha kulalamika kuhusu matatizo yanayokukuta bali unatakiwa uanze kushukuru kwa matatizo ambayo hauna.

      4.       MAKOVU YAKO NDIO NGUVU YAKO


Usije kuona aibu hata siku moja kutokana na makovu ambayo maisha  yamekupa. Kovu ina maana uliwahi kuumizwa na tatizo limekwisha na jeraha limefunga. Ina maana wewe alishinda maumivu, umejifunza somo, umekuwa na nguvu, na umesonga mbele. Kovu ni alama ya ushindi ya kujivunia. 

Usije kuruhusu makovu yako yakushikilie mateka. Usije kuyaruhusu yakufanye uishi maisha yako katika hofu. Huwezi kufanya makovu katika maisha yako kutoweka, lakini unaweza kubadilisha mtazamo wa jinsi unavyoyaangalia. Unaweza kuanza kuona makovu yako kama ishara ya nguvu na si maumivu.

      5.       KILA KIKWAZO KIMOJA NI HATUA YA KUKUA


Katika maisha, uvumilivu si kuhusu kusubiri tu; ni uwezo wa kushikilia tabia nzuri wakati wa kufanyia kazi kwa bidii ndoto yako, ukijua kwamba kazi unayofanya ni ya thamani. Hivyo kama unakwenda kujaribu, jitahidi kuweka muda wako wote huko.

Vinginevyo, hakuna faida kuanzisha jambo. Hii inaweza kuwa na maana ya kupoteza utulivu na faraja kwa wakati, na labda hata akili yako juu ya tukio. Na inaweza kumaanisha kukosa kula, au kukosa kulala, kama ulivyozoea, kwa siku kadhaa.

Na inaweza kuwa na maana kutoka eneo lako la faraja na ukaruruhusu kuumizwa na baridi kwa ajili ya jambo unalojaribu. Inaweza kumaanisha kutoa sadaka mahusiano na yote yale ambayo ni yako. Inaweza kuwa na maana ya kukubali kejeli kutoka kwa wenzako.

Kila kitu kingine ni mtihani wa dhamira yako ni kiasi gani cha wewe kweli unataka kutimiza jambo uliloanzisha.
Na kama unataka kutimiza jambo, itabidi kufanya, hata kama litaambatana na matukio ya  kushindwa na kukataliwa. Na kila hatua utakayopiga utajisikia vizuri kuliko kitu kingine chochote unaweza kufikiria. 

Utagundua kuwa mapambano hayapatikani katika njia, bali ni njia. Na ni thamani yake. Hivyo kama wewe unakwenda kujaribu,nenda njia yote. Hakuna hisia bora katika dunia ... hakuna  hisia bora kuliko kujua nini maana ya kuwa hai.

      6.       MITAZAMO HASI YA WENGINE SIO TATIZO LAKO


Kuwa na mtazamo chanya wakati mazingira yametawaliwa na mitazamo hasi. Tabasamu wakati wengine wanajaribu kukurudisha chini. Si jambo rahisi kudumisha shauku yako na kuzingatia unakoelekea. Wakati watu wengine wanakutenda vibaya, endelea kuwa wewe. Milele usiruhusu tabia chungu za mtu mwingine zilete mabadiliko kwako.

Zaidi ya yote, milele usikubali kubadilika ili kumvutia mtu ambaye anasema wewe hauna uwezo. Badilika sababu itakufanya mtu bora na itaenda kubadilisha kitu katika maisha ya mbeleni. Watu wataendelea kuzungumza bila kujali nini unafanya, hata iwe unafanya vizuri kiasi gani. Hivyo kuwa na wasiwasi kuhusu mwenyewe kabla ya kuwa na wasiwasi kuhusu nini wengine wana kufikiria. Kama unaamini kwa dhati katika kitu, wala hupaswi kuwa na hofu ya kupambana kwa ajili yake. Nguvu kubwa inatokana na kushinda kitu ambacho wengine walifikiria hakiwezekani.


Utani wote weka pembeni, maisha yako yanakuja mara moja tu. Huo ndio ukweli. Hivyo kufanya kitu kinachokupa furaha ndio kinapaswa kuwa kipaumbele chako.



Ukikutana na mtafuta ajira kilio chake kikubwa ni nimefanyiwa usaili mara nyingi ila baada ya hapo sijaitwa tena.

Waajiri huwa wanatumia vigezo gani katika kujaza nafasi za kazi katika ofisi zao? Kama unadhani una jibu moja litakalo wawakilisha waajiri wote kutokana na swali hilo, naomba nikwambie tafakari Zaidi.


Waajiri wote si sawa, anachokitafuta mwajiri mmoja kinaweza kuwa tofauti na mwajiri mwengine. Sababu inaweza kuwa ni kuwa mazingira ya kazi ya mwajiri mmoja yanatofautiana na mwajiri mwengine, kwahiyo watakapokuwa wanakusaili watakuwa wanaangalia vitu tofauti kutoka kwako.

Kila mwajiri anatafuta stadi za mwombaji zitakazoendana na kazi alizonazo katika ofisi yake ili kuboresha ufanisi wa kazi ili kutoa bidhaa au huduma nzuri kwa wakati na ubora unaotarajiwa na mteja. Lakini nje ya stadi kuna vitu ambavyo waajiri wengi wanafanana katika kuviangalia kutoka kwa mwombaji wa ajira.


Habari nzuri ni kuwa watafuta ajira wengi wanazo hizo sifa ila tu wanashindwa kuzionyesha wanapopata nafasi ya kuzionyesha. Na habari nzuri Zaidi ni kuwa kwa wale ambao hawana wanaweza kujijengea tabia hizi na zikawapa nafasi nzuri ya kuajiriwa kwa kupata mtu sahihi wa kuwaelimisha.

Na habari nzuri Zaidi ni kuwa utakapozijua hizi tabia utaweza kuboresha mfumo wako wa uombaji kwa kuelekeza moja kwa moja katika wasifu wako kile anachotafuta mwajiri katika kazi husika. BAdala ya kujaza masifa kibao katika wasifu wako utajua namna ya kuweka zile za muhimu.


   1. UWEZO WA KUWASILIANA



Uwezo wa kuwasiliana upo katika pande tatu moja ni uwezo wa kusikiliza, pili ni uwezo kuongea na tatu ni uwezo wa kuandika. Na kama unavyojua lugha yetu ya kiofisi ni kiingereza sasa ukiwa vizuri katika pande hizo tatu utajiweka katika nafasi nzuri katika soko la ajira. 

Unapokuwa na uwezo wa kupokea maelekezo kwa haraka na kuyahamishia katika maandishi na ukaweza kueleza matokea yake iwe kwa maandishi au mdomo ufanisi kazini utakuwa juu. 

Utajisikiaje unampa maelekezo mfanyakazi wako jinsi ya kufanya kazi Fulani na akashindwa kufanya kama ulivyomuelekeza kisa hamuelewani lugha?

  2.UWEZO WA KUTUMIA KOMPYUTA



Hapa tuelewane vizuri, kujua kompyuta haimaanishi lazima uwe umesomea kozi yake miaka kadhaa chuo labda kama kazi unayoomba inahusiana moja kwa moja na uweledi wa kompyuta kwa kusomea kozi husika. Ila kama unaomba kazi ambazo hazina uhusiano wa moja kwa moja na masomo ya kompyuta, nataka nikwambie haimaanishi ndo usijue kitu kuhusu kompyuta. 

Dunia hii ya utandawazi kila kazi kwa namna moja ama nyingine ili kuikamilisha lazima kompyuta itaingia kati sasa kama hujui kuitumia kabisa utakuwa unajipunguzia soko. Mathalani uweze kutuma barua pepe (E-mail), programu ya maandishi (Microsoft word) na program ya namba na maandishi (Microsoft Excel)

  3.UWEZO WA KUBADILIKA/KUFANYA KAZI ZAIDI YA MOJA


Katika dunia hii ambayo ukuaji wa teknolojia na ushindani wa huduma na bidhaa umekuwa mkubwa ofisi nyingi hupunguza gharama kwa kuajiri watu wachache wenye uwezo wa kufanya kazi Zaidi ya moja ili gharama za kuzalisha ziwe ndogo na wao waweze kushusha bei kupunguza ushindani na kuliteka soko. 

Hivyo ukiwa na sifa ya uelewa wa kazi Zaidi ya moja utajiongezea nafasi katika soko la ajira.


  4.UWEZO WA KUCHANGANYIKA NA WENGINE



Katika mazingira ya ofisi ambayo binadamu Zaidi ya mmoja wanashirikiana kufanikisha lengo moja  la ofisi, uwezo wa mfanyakazi mmoja kuchangamana na mwengine bila tatizo ni jambo la muhimu sana. 

Ofisi inaweza kuruhusu mtofautiane kwa hoja ili kupata kitu kizuri lakini si kugombana sababu wazo la mmoja limepingwa na wengi na kuwanunia, hii italeta utengano na kushusha ufanisi mahali.

Ukiwa na uwezo wa kuchangamana na wengine mathalani katika wasifu wako ukaweza kuonyesha kwamba uliwahi kufanya kazi na watu Fulani na kufanikisha jambo Fulani.

  5.UWEZO WA KUONGOZA




Sehemu yoyote ambayo wanakutana watu Zaidi ya wawili lazima kuwe na kiongozi na lazima ujue miongoni mwenu lazima atoke kiongozi.

Waajiri wengi wanapenda mtu mwenye uwezo wa kuongoza sababu wenye tabia hii huwa na uwezo wa kufanya maamuzi ya kibunifu hivyo wanatarajia hata wakati wa utendaji wako utakuwa unafanya kwa ubunifu na kuwaongoza wengine  na si kufuata njia zile zile zilizopitiwa na wengine na hivyo kuongeza ufanisi kazini.

HAUJACHELEWA KUFANYA MAREKEBISHO PALE AMBAPO UNAONA UNA MAPUNGUFU ILI KUONGEZA UWEZO WAKO WA KUAJIRIKA KATIKA SOKO LA USHINDANI WA AJIRA.

HAKUNA ALIYEZALIWA NA SIFA ZOTE HIZO BALI WENGINE WAMEZITENGENEZA NA WAKAWEZA KUZIFANYA KUWA SEHEMU YA MAISHA YAO NA MATOKEO MAZURI WAKAYAPATA.

ANZA SASA KUPIGA HATUA...


 Laurie Notaro aliwahi kusema;

“If you really believe in what you're doing, work hard, take nothing personally and if something blocks one route, find another. Never give up”.

Kauli hii ikimaanisha;

 “Kama unaamini katika kile unachofanya, fanya kwa bidii, usifanye ubinafsi na kama kuna jambo litajitokeza kufunga njia moja, tafuta njia mbadala. Usikate tamaa”.

Kukata tamaa ni kitendo cha kuishiwa mbinu mbadala za kukamilisha jambo Fulani ulilokuwa unalifanya kwakuwa tu umekumbana na ugumu. Katika kila jambo tunalofanya huwa tuna matarajio ya kufanikiwa ila pia changamoto haziwezi kuepukika.


Maneno “Kata” na “Tamaa” hayatakiwi kuwa pamoja. Hata neno hapana halipaswi kuwa sehemu ya neno katika kamusi yako. Kuwa sehemu ya jamii ya watu Fulani katika dunia unakuwa ni kiumbe wa pekee kuwahi kutembea juu ya ardhi hii.

SABABU 8 ZA KWANINI HUTAKIWI KUKATA TAMAA

      1.UPO HAI,NA UNAWEZA



Yaani ilimradi una pumua pumzi ya uhai, hakuna uhalali wa wewe kusema kuna jambo limekushinda na unalikatia tamaa. Kama ukiweka akili na mawazo yako katika hilo jambo lazima utaweza kufanya japo kufanikisha sehemu yake. Hakuna lisilowezekana chini ya jua.

Christopher Reeve aliwahi kusema;
So many of our dreams at first seem impossible, then they seem improbable, and then, when we summon the will, they soon become inevitable.

Ikimaanisha; “Ndoto zetu nyingi kwa mara ya kwanza huonekana haziwezi kuwa kweli, baadae huonekana haziwezekani kabisa, ila, tunaipoita utayari wa kufanya ndani yetu, punde zinakuwa haziwezi kuepukika”

Udhuru pekee unaoweza kuutoa kwa kutoweza kutimiza ndoto zako ni ikiwa umekufa ila kama unaweza kusoma hapa, hakuna cha kukuzuia.

       2. AMINI KATIKA NDOTO ZAKO


Ukikata tamaa, unajikatia tamaa mwenyewe na si mtu mwengine yeyote. Usijiuze mwenyewe wala kuruhusu mtu mwengine akurudishe nyuma. Kama unaweza kuwa na ndoto zako mwenyewe basi hata uwezo wa kutimiza unao.

Kuna mamilioni ya watu wa kale waliokuwana na ndoto zao katika ulimwengu huu, kama na wao wangekata tamaa hapo mwanzo hii dunia isingekuwa hivi unavyoiona leo.

Chukulia mfano ndugu wawili kutoka katika familia ya Wright waliokuwa wana ndoto za kutengeneza ndege jinsi walivyokumbana  na vikwazo vya kuifanya ndogo yao kuwa kweli huku hakuna aliyedhani kama ndoto inawezekana kwa kuwacheka na kejeli. Hawakukatishwa tamaa ila walipambana kuifanya ndoto yao kuwa kweli na walifanikiwa, je usafiri wa ndege si kiunganishi muhimu katika dunia ya leo?

Langston Hughes aliwahi kusema;
“Hold fast to your dreams, for without them life is a broken winged bird that cannot fly.

Ikimaanisha;
“Shikamana na ndoto zako, kwakuwa bila ya hizo maisha ni sawa na ndege aliyevunjika mabawa asiyeweza kuruka”

      3.UNA KILA KITU UNACHOTAKA

Kila unahohitaji ili kufikia malengo yako, kimewekwa tayari ndani yako. Usiwe mtu wa kutoa udhuru, kama inawezekana kuwa na wanamichezo walemavu wenye uwezo wa kushiriki michezo katika kiwango cha olimpiki,mapungufu yako hayawezi kukuzuia kutimiza ndoto yako. Mshukuru Mungu na tumia uwezo aliokupa kufanikisha ndoto zako.

      4. HAUHITAJI KUJA KUJUTA

Majuto ni hisia mbaya sana mtu kuwa nayo. Usiruhusu nafsi yako ijiweke katika mazingira ya kuja kujuta ila unapaswa ufanye unachotakiwa kufanya sasa.

Rory Cochrane alisema;
“I do not regret the things I've done, but those I did not do

Ikimaanisha;
“Sijutii kwa vitu nilivyofanya, ila kwa yale yote ambayo sikuyafanya”

      5.UNATAKIWA UJITHIBITISHIE MWENYEWE


Unatakiwa uje ujithibitishie mwenyewe na ulimwengu mzima kwamba unaweza kufanya jambo. Usiruhusu jambo au kitu chochote kikuzuie kutimiza ndoto zako.

Kushindwa kwa kweli si kule kujaribu na kukosa, bali ni kule kutojaribu kabisa.
Wewe unaweza kutimiza ndoto zako, sababu wanaoshindwa ni watu wasiofanikiwa daima.

      6.UTAPATA MABADILIKO MAZURI


Inawezekana kabisa unapitia wakati mgumu sasa, lakini ukishikilia kwa muda utapata mabadiliko ya haraka na mazuri. Kama utaendelea kupambana hutakiwi kukata tamaa sababu huwezi jua lini ndio siku yako ya kutoboa.

Usiwe kama mtu anayechimba kisima ambaye hadi anafika mita 50 hajapata maji, anakata tamaa na kuacha lakini anakuja mwengine anachimba mita 1 tu toka pale alipoishia yeye anakutana na maji. Kama umeamua fanya kweli mpaka upate matokeo.

      7.UNAPASWA KUTIMIZA

Si kila mtu anaweza kusikia sauti ya ndani inayomwambia afanye jambo Fulani, ila kama wewe umeweza kuisikia ikikwambia timiza jambo Fulani, nakwambia usiachie bila kutimiza sababu umeumbwa ili kufanikisha hilo.

      8.HAMASISHA WENGINE

Katika maisha yetu lazima kuna watu uliowazidi watakuwa wanakuangalia kama mtu wao wa mfano, mathalani wadogo zako au hata watu wa karibu na majirani. Sasa wanapokuona wewe umekata tamaa inawakatisha tama hata wao. 

Ndio maana hutakiwi kukata tamaa sababu hujui wangapi wanakuangalia, ushindi wako utawapa hata wao nguvu ya kupambana katika safari yao kwa kuwa walishawahi kuona Fulani aliweza.



Kuna idadi ya kutosha ya mitazamo chanya ndani yako ambayo pengine haujaweza kuitambua na inasubiri kuamshwa. Na kila wakati unapopoteza motisha unapaswa kujikumbusha kwa haraka uwezo wako. 

Daima kumbuka kwamba ladha ya mafanikio daima inakabiliwa na kushindwa kwa muda. Kama wewe utakata tamaa kutokana na magumu ya muda utakuwa unajiandaa kushindwa, lakini kama wewe utaendelea kupambana utakuwa na mafanikio.

Si kila mwenye mafaniko leo hii,
 aliyapata kwa mara ya kwanza
 alipojaribu.
Mara nyingi ni watu ambao walijaribu mara nyingi bila mafanikio,
 kabla hawajapatia na 
kufanikiwa.

Na wengi wao ni wale,
 waliokuwa wamejitolea kupambana 
na vikwazo 
kutoka kwa watu
 mbali mbali na mifumo.

Wanapovuka hatua hii ya vikwazo,
 wengi wao 
wanakosa majibu ya moja kwa moja wamefikaje hatua hiyo
 ya mfanikio pamoja na vikwazo vyote walivyokutana navyo.

Kuna siri imejificha hapa?
Ndio, 
kushindwa mara nyingi na bado kuendelea kunga'ang'ania mpaka unashinda,
 inaonyesha kuna kitu
 alikiona hapo.

Ni kipi hicho?
Nadhani,
 tunahitaji makala itakayojitegemea, 
kuelezea siri iliyopo 
hapa kwa watu wengi
 waliofanikiwa.

Unapopatwa na wakati mgumu,
 iwe katika masomo au kazini 
hupaswi kukata tamaa mapema 
bali 
tumia historia fupi za watu hawa kujitia 
nguvu ya kusonga 
mbele.

Watu hawa waliofanikiwa wapo katika makundi makuu 8.
Leo tunaanza na kundi la kwanza la 
wafanya biashara.

1.Henry Ford:

Huyu ni mfanyabiashara raia wa Marekani,
alizaliwa 
30 julai 1863 katika familia ya wakulima wadogo,
 na kufa 7 Aprili 1947.
Ndiye aliyeanzisha
 kampuni kubwa ya magari aina ya Ford.
 Aliondoka kwao,
 akiwa na miaka 16 tu
 na kwenda kutafuta 
ajira ya umakenika.
Kabla hajafanikiwa,
 alifilisika kibiashara mara tano.
 Alianza kuonja mafanikio baada ya kubuni 
gari la kwanza kutengenezwa 
Marekani aina ya 
Ford Model T.


2.R. H. Macy:

Ni raia wa Marekani
 ambaye alikuja kuanzisha 
biashara ya idara ya stoo kubwa za biashara
 katika jiji la
NewYork.
Alizaliwa 30 Agosti 1822 na 
kufariki 29 machi 1877.
Kabla hajafanikiwa katika wazo hili alifeli mara saba.

3.F.W. Woolworth:
Huyu ni raia wa Marekani ambaye alifanya kazi katika stoo ya bidhaa ya 
mfanyabishara mwengine,
ambako alipokea manyanyaso 
mengi hadi yakamfanya 
aamue kukaa chini na 
kupata wazo la yeye kufungua stoo zake mwenyewe za biashara.
Alizaliwa 13 Aprili 1852 na
kufa 8 Aprili 1919. 
Hata huku Tanzania kuna maduka yenye hili 
jina lake moja 
maeneo ya Posta PPF Tower.

4.Soichiro Honda:
Ni raia wa Japan,
na muanzilishi wa kampuni ya Honda.
Aliwahi mara kadhaa kuomba 
kazi katika kampuni ya
 Toyota kama injinia,
lakini alikosa baada ya 
kufanyiwa usaili na 
kuonekana hana vigezo.
Alikaa muda mrefu sana bila kuwa na 
kazi,
 kitu kilichomfanya 
akae chini kufikiria na kuibuka na 
wazo la 
kampuni ya Honda.
Alizaliwa 17 Novemba 1906 na
 kufa 5 Agosti 1991.
 Ambayo imekuja kuwa mpinzani wa kampuni iliyomkataa.

5.Akio Morita:
Ni raia wa Japan,
na muanzilishi wa
 kampuni ya Sony.
Bidhaa yake ya kwanza,
 kuanzisha ilikuwa ni 
jiko la kupikia mchele(Rice cooker) 
ambayo ilikuwa inaunguza sana wali hivyo watu waliacha kununua bidhaa hiyo.
Lakini,
 hakukata tamaa mpaka 
alipokuja kuboresha na 
kuja kukubalika tena na bidhaa 
nyingi tofauti tofauti
 za vifaa vinavyotumia umeme.
Alizaliwa 26 Januari 1921
na kufa 3 Oktoba 1999.

6.Bill Gates:

Ni raia wa Marekani,
alizaliwa 28 Oktoba 1955 mpaka leo bado anadunda.
Alianza na mkosi wa kufukuzwa
 chuo cha Harvard
ambapo aliamua kuanzisha biashara 
na mwenzake kwa jina la kampuni 
iliyoitwa Traf-O-Data 
ambayo 
haikufanikiwa kabisa.
Alipopata wazo la kutengeneza kompyuta alilipeleka katika kampuni moja ambapo lilikataliwa.
Hakukata tamaa na mwisho wa uvumilivu wote akaja na kampuni ya 
Microsoft ambayo imempa utajiri 
usioelezeka.

7.Harland David Sanders:
Ni raia wa Marekani,
na muanzilishi wa kampuni ya kukaanga kuku ya Kentucky Fried Chicken(KFC).
Alipoanza hii biashara alikataliwa mara 1,009 na migahawa ya Marekani kumpa 
oda ya kuku anaouza.
Lakini uvumilivu wake ukaja kumpa mafanikio makubwa katika biashara hiyo hiyo.
Alizaliwa 9 Septemba 1890 na 
kufa 16 Desemba 1980.

8.Walt Disney:
Kwa wale wapenzi wa 
filamu na katuni,
huyu ndio mtu aliyewaingizia 
hiyo burudani kwa mafanikio sana.
Alianza kwa kufanya kazi ya 
uhariri wa gazeti 
ambapo alifukuzwa kwa 
kuonekana hana ubunifu.
Na alikuja kuanzisha miradi 
 mbali mbali ambayo haikuweza kudumu muda mrefu na kumfilisi kabisa.
Lakini mwisho wa uvumilivu wake akaja kufanikiwa katika 
kampuni yake ya Disney ambayo 
inajihusisha na filamu na katuni.
Alizaliwa 5 Desemba 1901 na 
kufa 15 Desemba 1966.

USIOGOPE KUSHINDWA,
KILA KITU USIPOJARIBU
 HAUTAWEZA KUKIJUA KAMWE.

KAMA WEWE UNATAKA KUFANYA BIASHARA 
AU 
ULISHAANZA,
 UKISHIDWA USIKATE TAMAA.
 ENDELEA KUNG'ANG'ANIA KAMA 
UNAJUA NDICHO KITU PEKEE UNACHOWEZA KUFANYA 
KATIKA MAISHA YAKO.

USIKATISHWE TAMAA NA WAFANYABIASHARA AMBAO WANADHANI WANAFAHAMU KILA KITU ,
KWA KUKOSOA WAZO LAKO.
 NAO PIA KUNA VITU HAWAJUI HATA KAMA WAMESHAFANIKIWA KWA HIYO PIGANIA ULICHONACHO.

 
Copyright 2013-2017 Lisha Ubongo
| Branded by www.pixelbase.co.tz